BABA SAMIA retweetledi

KUONDOKA KWA MCHUNGAJI MSIGWA CCM:NI OCT 29 KWELI?
Moja ya sababu Kuu ambayo Mchungaji Peter Msigwa ameitaja kupelekea kuondoka kwake ndani ya CCM anasema ni matukio ya Oct 29,2025.HAUWEZI kubishana na Mdomo wake lakini ukweli anaujua yeye mwenyewe.
Hata nyakati zile alipokuwa anatoka Chadema kuja CCM mwaka jana baada ya kukosa Cheo cha Mwenyekiti wa Chadema kanda ya Nyasa dhidi ya SUGU,Peter Msigwa tena hakuwa mkweli mbele ya Umma ALIDANGANYA KAMA ANAVYODANGANYA SASA.
Ni miezi kama SABA HIVI TANGU Oct 29,2025 mpaka sasa May 24,2026 lakini Mchungaji Peter Msigwa akaendelea kusikilizia muda wote huu wa miezi saba akiendelea kula mshahara na posho pale Ofisi ya ITIKADI NA UENEZI kwa ndugu yangu KINANI KIHONGOSI.
YAPO MAMBO MAKUBWA MATATU HIVI AMBAYO YANAMUONDOA LEO CHAMA CHA MAPINDUZI.
I.MATARAJIO ya kupata CHEO/UTEUZI ndani ya Chama na Serikali hayapo tena.Hesabu za Mchungaji zilikuwa cleary kabisa kwani aliamini kuwa ujio wake ndani ya CCM ungempa uteuzi kama.ilivyokuws kwa wanachadema wengine ambao walikuja ndani ya Chama na kupata teuzi.
Kumbuka kuwa Msigwa angepata CHEO cha Mwenyekiti wa kanda ya Nyasa asingekuja CCM kamwe kwahiyo Msigwa alikuja CCM kwa hasira na bahati nzuri CCM walilijua hilo.
II.Kuundwa kwa TUME-JINAI kutokana na Matukio ya Oct 29
Kama.una akili nzuri ni rahisi kujua kuwa Msigwa alikuja CCM kwa missions kuu mbili hizi hapa(I)kutafuta Cheo na kuikomoa Chadema lakini bado moyo wake ulikuwa Chadema,CCM walikuwa wanafahamu hilo haswa.
Pili(II)Msigwa alikuja Chadema kufanya UKACHERO wa Kisiasa then badae arudi Chadema.Ni kwamba pamoja na kuwekwa idara ya Uenezi,Msigwa alikuwa chini ya "ukachero" mkubwa wa CCM akisomwa nyendo zake usiku mchana asubuhi.
Mchungaji inawezekana sana alikuwa sehemu ya Mpango wa NO REFORMS NO ELECTION ambao ndio ulizaa matukio ya Oct 29.
Ilibidi atafutwe mtu wa kumwingiza ndani ya mifumo ya CCM kuweza kuratibu mipango hiyo ya Chadema akiwa ndani ya CCM.KUMBUKA TUNDU lissu na Msigwa ni damu damu.Inawezekana sana Tundu Lissu alitaka kumtumia Peter Msigwa kutekeleza waliyotekeleza Oct 29.
USIJE ukashangaa Peter Msigwa akija kutajwa kwenye REPOTI YA TUME JINAI na kutiwa nguvuni mbeleni.Njia pekee sasa ni kuondoka CCM na kwenda kuungana na wana Oct 29 wenzake huko Chadema.
III.Sababu ya Tatu kubwa ni URAFIKI uliopo wa kufa na kuzikana wa ndugu Tundu Lissu na Mchungaji Peter Msigwa ambao unamfanya MSIGWA AJIONE NI MSALITI mbele ya jamaa yake Tundu kwa kuendelea kula mshahara wa CCM pale Dodoma.
Mtarajiio ya Msigwa yalikuwa ni kwamba uenda SERIKALI mbeleni ingemtema(Gerezani) Tundu Lissu baada ya Uchaguzi Mkuu kumalizika lakini anaona Serikali(Mahakama) IMEKAZA.HAINA MCHEZO KABISA NA ISHU YA LISSU.
JAPO watu wengi wanataka kuaminishwa kwamba Tundu Lissu yupo Magereza Ukonga KISIASA lakini ukweli unabaki kuwa jamaa ameshiriki kwa 70% kuratibu yale ya Oct 29 hata akiwa huko huko mahabusu..
Hii sio ishu kabisa kwani hata Muuza madawa ya kulevya wa MeXICO Olechampo aliweza kuratibu biashara zake za kuuza dawa za kulevya hata alipokuwa gerezani na baade akafanikiwa kutoroshwa na kundi lake hatari.
Tundu Lissu ni wazi alikuwa na mkono wake mkubwa tu kwenye Oct 29,niaminini.
Kama mnabisha nadhani tusubilie majibu ya Tume- Jinai,itasema ukweli kuhusu haya nisemayo.
Infact,Oct 29 kulikuwa na elements zote za UHAINI/MAPINDUZI NA BAHATI MBAYA SANA wapo hata wanaccm wanatajwa nao kushiriki kuwezesha matukio yale ya hovyo.
Ila tu cha kushangaza hata report ya Tume JINAI ambayo itakuja na purely ushahidi nayo wataipinga tena kwa nguvu kubwa zaidi.NASUBILIA KUONA WATAWEZAJE KUPINGA FACTS?,HUU ni Uchunguzi wa KIJAJI na sio bla bla tena.
Katika mazingira kama hayo Msigwa anabakije CCM?

Indonesia






























