laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒
3.2K posts

laUrentmIlleR👨🏿🚒
@TaleebMillernz_
aduI🧠 be smart | efforts never lie | smart work pays …. mucho pLata💰 amigo... there's death don't forget it ✍️🏾🧠 allahuma Inn as alukal a'afiya🤲🏾🫀
Dar es Salaam, Tanzania Beigetreten Haziran 2023
76 Folgt95 Follower
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet

laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet

Kabla hamjalala.
Tambueni kwamba.
Kuji associate na watu waliofeli mambo yao.
Watu waliojikatia tamaa.
Watu waongo.
Watu wa maigizo.
Watu wenye mawazo finyu.
Ni kujitia ukilema.
Heri uonekane unajiona ukisimamia mambo ya maana
Kuliko
Uonekane wa maana kwa kusimama na mambo ya hovyo ili uonekane haujioni.
Wengi walishaumia sana kwa ku impress kundi fulani la watu.
Ishi kwa malengo ambayo yako ndani yako.
Pombe, uzinzi, tamaa na marafiki wajinga ni hatua kumi katika kuporomoka kimalengo.
Indonesia
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet

UKIFA, Mke,watoto, na wazazi wako watalia sanaaaa...
Marafiki watalia lakini baada ya siku 40 watakusahau na kuendelea na kazi zao...
Hii familia yako itaingia kwenye Umasikini mkubwa mno kama utakua hujafanya hata mambo yafuatayo....
UKWELI MCHUNGU
Familia nyingi haziporomoki kwa sababu ya kifo chenyewe
👉 zinaporomoka kwa sababu ya maandalizi duni.
Kifo hakiharibu familia.
Kutokuwa na mfumo ndiko kunaharibu.
1. JENGA KIPATO KISICHOKUFA PAMOJA NA WEWE
Usijenge maisha yanayokufa ukifa.
• Mshahara hufa na wewe
• Kibarua hufa na wewe
• Biashara inayokutegemea 100% → hufa na wewe
Suluhisho: 👇
• Jenga biashara yenye mfumo
• Mapato yanayoendelea (rent, dividends kupitia hisa, biashara inayoendeshwa na watu wengine)
✍️ Kama kipato hakipo bila uwepo wako → familia yako iko hatarini.
⸻
2. WEKEZA (SIO KUHIFADHI TU)
Akiba ni ya muda mfupi.
Uwekezaji ni ulinzi wa vizazi.
• Ardhi inayolima au kukodishwa au kuuzwa baadae
• Nyumba ya pango
• Hisa, mifuko ya uwekezaji kama UTT_Amis
• Biashara inayokua na ya uhakika
👉 Kosa kubwa wanalofanya watu wengi ni kuacha pesa, si mfumo wa pesa kuendelea kuingia.
Kanuni:
Mtoto hawi tajiri kwa kurithi pesa — anakuwa salama kwa kurithi uwekezaji.
⸻
3. USIACHE FAMILIA BILA UJUZI (SKILLS)
Hiki ndicho kipengele kinachopuuzwa zaidi.
Hasa wanaume, suala la kuacha mke wako nyumbani hajui chochote kuhusu biashara ni hatari…
• Mke asiye na skill → ataanguka
• Watoto wasio na skill → watakuwa maskini hata wakipewa mali
👉 Uliza sasa:
• Je mke wako ana skill ya kuingiza kipato?
• Je watoto wako wanafundishwa ujuzi au darasani tu?
Ujuzi muhimu:
• Biashara
• Digital skills
• Usimamizi wa fedha
• Mawasiliano & mauzo
Skill ni bima ambayo haiwezi ku-expire.
⸻
4. ANDIKA NA WEKA WAZI TAARIFA ZA MALI
Familia nyingi hupoteza kila kitu sio kwa sababu hawakuwa nacho, bali hawakujua.
• Mali hazijulikani
• Akaunti hazijulikani
• Hati zimefichwa kichwani mwako
👉 Matokeo:
• Migogoro
• Mali kugawiwa vibaya
• Watu wa nje kunufaika
Fanya hivi:
• Orodhesha mali zako
• Eleza mapato yanatoka wapi
• Weka mtu wa kuaminika ajue
✍️ Siri zako zikifa na wewe, familia yako italipa gharama.
⸻
5. JENGA MFUMO, SIO MIMI
Familia nyingi hufa kiuchumi kwa sababu kila kitu kilikuwa:
“Uliza baba”
“Baba anajua”
“Baba atafanya”
Ukiwaondoa baba → mfumo unaondoka.
👉 Badilisha:
• Wewe → mfumo
• Wewe → taratibu
• Wewe → watu
Wewe sio mpango. Mfumo ndio mpango.
⸻
6. USIFUNDISHE KUTEGEMEA — FUNDISHA KUJITEGEMEA
Upendo mwingi usio na hekima huua familia.
• Kumlipa kila kitu mke
• Kumlinda mtoto asihangaike
• Kuwaficha ukweli wa pesa
👉 Matokeo:
Ukiwaondoka → wanaanguka vibaya.
Fanya hivi:
• Wape majukumu
• Waelewe pesa zinatoka wapi
• Waone changamoto kabla hazijawaangamiza
✍️ Usiwaandalie maisha rahisi — waandalie uwezo.
⸻
7. PANGA KIFO CHAKO KAMA UNAVYOPANGA MAISHA
Hili ni gumu kusikia, lakini ni la kiume na la kiongozi.
• Nani ataendesha nini?
• Nani atasimamia nini?
• Nani atatoa maamuzi?
👉 Kifo hakisubiri uivae ujasiri.
Mtu anayepanga kifo chake vizuri, anaishi kwa heshima.
⸻
MWISHO
Familia yako haitakumbuka:
• Ulichosema
• Ulichowaahidi
Watakumbuka:
• Ulichowaachia
• Ulichowafundisha
• Ulichowajengea
👉 Urithi sio pesa.
👉 Urithi ni mfumo wa kuendelea

Indonesia
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet

Mbinu wanazotumia wafanyabiashara wenye mitaji midogo kariakoo kukuza biashara zao, kuwa magiant, kuongeza mauzo na kutawala soko…
Kama huzijui, utaendelea kufanya biashara local sana …
.
⸻
1. GROUP BUYING (NGUVU YA PAMOJA)
Wanakusanyika 3–5, wanaunganisha mitaji, wanakwenda kununua mzigo mkubwa China.
👉 Wanapata kwa bei ndogo sababu ya mzigo mkubwa, faida inapanda, ushindani unakufa.
Ndo ile unakuta Kariakoo nzima labda watu watatu tu ndo wanabishana fulani na bei ndogo wengine wote mnanunua hapo.
⸻
2. CHANNEL ZA WAFANYABIASHARA MIKOANI
Wana mtandao tayari mikoani. Mzigo ukishuka → unasambazwa siku hiyo hiyo.
👉 Hawategemei wateja wa dukani pekee.
Duka ni store tu.
Biashara halisi iko:
• WhatsApp, Mawinga, wasambazaji, mabasi, makontena
👉 Duka likifungwa, mauzo yanaendelea.
⸻
3. KUWA MBELE YA MUDA (FIRST MOVERS)
Hawasubiri design itambe Instagram.
👉 Wao ndio wanazindua trend, soko linawafuata.
Hii inawapa nafasi ya kujipangia bei na ku-control soko.
⸻
4. NI CHIMBO LA BIDHAA MOJA (PRODUCT DOMINATION)
Wengi huuza bidhaa moja tu.
Wengine hawaendi China ila mzigo ukishuka kwa Tajiri, wanachagua aina maalum
(mf. pochi ya muundo fulani wananunua yote wanakua nayo pekee yao).
👉 Kariakoo nzima → bidhaa hiyo iko kwao tu ndo wanauzia wengine.
Hii iko kwenye fashion sana.
⸻
5. WANACHEZA NA VOLUME, SIO FAIDA
Hawauzi kupata faida kubwa kwa bidhaa moja.
CASH FLOW > FAIDA KUBWA
Wanapendelea:
• kuuza haraka pesa irudi waendelee kuzungusha mzigo mara nyingi
👉 Faida ndogo × mara nyingi = pesa kubwa.
⸻
6. WANAPIMA SOKO KABLA YA KUSHUSHA MZIGO
Kabla ya kuagiza:
• Wanapiga simu kwa wateja wa mikoani
• picha WhatsApp
• preorder ndogo
👉 Hawashushi mzigo kwa kubahatisha.
Ndo maana mzigo ukishuka tu unashambuliwa.
⸻
7. WANA SUPPLIERS WAO WANAOAMINIANA
Kwa sababu:
• volume kubwa
• uhusiano na supplier
Mzigo kwa malikauli.
👉 Unapojaribu kushindana bei, tayari umechelewa.
WANAFICHA SOURCE YAO
Hawapigi kelele supplier wao ni nani.
👉 Wanajua taarifa = pesa.
⸻
8. WANACHEZA GAME NDEFU
Hawafikirii:
“Leo nipate faida kiasi gani?”
Wanafikiria:
“Nifunge soko, nitawatoa wote taratibu.”
Akili yao ni kuteka soko zima na wafanya biashara wote wa bidhaa hiyo.
👉 Ndiyo maana leo unaona mtu alianza na mtaji mdogo, leo ana maduka 5–10.
⸻
…
Kama huzielewi hizi mbinu:
• utaendelea kuuza local
• utachoka kuzungusha bidhaa chache
• utafurahia faida ndogo ndogo
Lakini ukizielewa:
👉 Biashara yako inaanza kucheza ligi ya Kariakoo.

Indonesia
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet

HUWEZI KUHARAKISHA MAFANIKIO YAKO YA KIFEDHA KAMA UTAENDELEA KUTUMIA HIZI NJIA MBILI NA KUPUUZIA HII YA TATU.
Achana na ushauri wa kutengeneza utajiri kwa kutumia njia ya kawaida ya elimu, ajira, akiba, na kustaafu
Hapa nakupa njia ya uhakika ya kufikia uhuru wa kifedha haraka, inayoitwa “The Fastlane” (njia ya kasi)
Njia mbili za kuachana nazo ni....
1. The Sidewalk (Barabara ya Watembea kwa Miguu)
Hii ni njia ya watu wasiopanga maisha yao kifedha. Wanaishi kwa kutegemea mshahara wa mkono kwa mdomo bila akiba au mipango ya baadaye
2. The Slowlane (Njia ya Polepole)
Njia hii ndiyo inayohubiriwa na jamii: soma kwa bidii, pata kazi nzuri, weka akiba, wekeza kwenye mfuko wa kustaafu, na uishi maisha ya starehe ukiwa mzee
Tatizo ni kwamba hii inawafanya watu kuwa tegemezi kwa muda mrefu na kuwapa uhuru wa kifedha wakiwa wazee
.
Kwani wewe unapenda kuteseka miaka yote ufanikiwe baada ya kustaafu? Au ukiwa mzee?
Kama hapana, Tumia njia hii...
3. The Fastlane (Njia ya Kasi)
Hii ni njia ya wajasiriamali, Wafanyabiashara na wabunifu wanaojenga biashara zinazopanuka na kuzalisha kipato kikubwa siku kwa siku
Badala ya kuuza muda wao kwa mshahara, wanajenga mifumo inayowaingizia pesa hata wakiwa hawafanyi kazi moja kwa moja.
Misingi ya Njia ya Kasi (Fastlane)
1. Jenga Utawala (Control) – Usimwache mwajiri au mtu yoyote adhibiti maisha yako ya kifedha. Miiliki biashara yako au uwekezaji wako, Uwe na control
2. Angalia Hitaji la soko (Need) – Usifuate tamaa zako tu yaani unachokipenda tu, tengeneza thamani kwa kutatua matatizo ya watu
3. Kiwango (Scale) Biashara au uwekezaji wako uwe na uwezo wa kukua na kuwahudumia watu wengi.
4. Ubunifu (Time Independence) – Epuka biashara zinazokutegemea moja kwa moja kwa muda wako. Badala yake, unda mifumo unaoweza kufanya kazi hata bila wewe kuwepo.
5. Upanuzi (Magnitude) – Biashara yako iwe na uwezo wa kukua haraka kwa kutumia teknolojia, usambazaji wa wingi, na uwekezaji
Unasisitizwa, utajiri wa kweli hauji kwa kuweka akiba ndogo kwa miaka 40, Tumia mbinu hizo Tano.
.
Wewe bado uko kwenye njia hizo mbili au kwenye njia ya tatu tayari kuna points unazifanyia kazi?
Indonesia
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet

JINSI YA KUPUNGUZA MATUMIZI YA FEDHA YASIYO YA LAZIMA NA KUZIPANGILIA FEDHA ZAKO ILI UFANIKIWE KIUCHUMI..
...
Watu wengi hawafanikiwi kwa sababu hawapati pesa. NO
Ila kwa sababu hawajui kuzilinda, kuzipangilia, na kuzifanya ziwafanyie kazi.
Ukishindwa kudhibiti matumizi madogo, hata pesa nyingi zitakumaliza kimya kimya.
Nini ufanye sasa? 👉👉
1. TAMBUA UVUJISHAJI WA FEDHA (FINANCIAL LEAKS)
Fedha nyingi hazipotei kwa matumizi makubwa, zinapotea kwa madogo madogo ya kila siku.
Kulakula chakula nje bila mpango, data, subscription, anasa ndogo zisizo na mchango, shipping zisizo za mipango.
👉 Usipoviziba hivi vijishimo, mapato yako yatakuwa ni ya kupita tu, siyo ya kubaki.
2. TOFAUTISHA MAHITAJI NA TAMAA
Mahitaji = yanaongeza au kulinda maisha yako.
Tamaa = zinakupa hisia ya muda mfupi.
Simu mpya kila mwaka, kila toleo, kuishi maisha ya kushindana na kujionyesha.
👉 Watu maskini kifedha hununua kwa hisia. Wenye mafanikio hununua kwa mantiki.
3. JILIPIE WEWE KWANZA
Ukisubiri eti pesa ambayo inabaki ndio uwekeze, hutowekeza…
Fanya hivi:
•Pata pesa
•Weka pembeni akiba/uwekezaji kwanza
•Tumia kilichobaki
👉 Akiba siyo kile kinachobaki, ni kipaumbele no 1.
4. TUMIA BAJETI KAMA SILAHA, SIO KAMA OPTION TU
Hii ni ramani ya kukuongoza kifedha.
•Jua pesa inaingia kiasi gani
•Jua inaenda wapi
•Weka mipaka kwa kila kipengele
👉 Ukikosa bajeti, maisha ndiyo yatakuwekea bajeti kwa dharura na madeni.
5. ISHI CHINI YA KIPATO CHAKO
Hii ndiyo siri watu wengi hawapendi kusikia.
Acha kuishi nyumba inayokuzidi uwezo na vitu vinavyokuzidi uwezo.
•Ongeza mapato ✔
•Chelewesha anasa ✔
•Jenga msingi kwanza
👉 Utajiri hauonekani mapema. Umaskini hupiga kelele mapema.
6. GEUZA MATUMIZI KUWA CHOMBO
Kabla ya kutumia pesa jiulize:
Hii itanirudishia nini?
✔ Uwekezaji
✔ Biashara
✔ Vifaa vinavyoongeza kipato
👉 Fedha nzuri ni ile inayorudi na rafiki zake ☺️
7. JENGA NIDHAMU, SIO MOTISHA
Unaona walioanza na motivation mwaka huu, pumzi ishaanza kukata…
Motisha huisha. Nidhamu hubaki.
•Anza hata kama hujawa tayari 100%
•Wekeza hata kama ni kidogo
•Fuata mpango hata kama unakubana
👉 Nidhamu ndogo leo = Uhuru mkubwa kesho.
...
Huhitaji miujiza ili kufanikiwa kiuchumi.
Unahitaji:
•Udhibiti
•Mpango
•Subira
Fedha zikikuona unaziheshimu, nazo zitakuheshimu
Indonesia
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet

Namdai Alex pesa yangu, ananizungusha hataki kunilipa.
Anasema pesa hana, ila yeye anamdai pia Becka, so anangojea siku Becka akimlipa ndio nayeye anilipe na mimi!!
Jana kuna kazi tumefanya mimi na Becka, tukalipwa!!
Wakati tunalipwa ile pesa ya Becka nikaichukua tena na mimi!!
Nikamwambia mimi ninamdai Alex, na Alex anakudai wewe…
so nimekata juu kwa juu!!
Nikamwambia Alex usimdai tena Becka na mimi sikudai tena, na Becka hudaiwi tena na Alex…..tumemalizana
NIKO SAHIHI?
AU NIMEKOSEA WAPI?
Filipino
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet
laUrentmIlleR👨🏿🚒 retweetet








