Purity Magesa

3.1K posts

Purity Magesa

Purity Magesa

@purity1978

Beigetreten Kasım 2025
28 Folgt25 Follower
Purity Magesa
Purity Magesa@purity1978·
Uongozi bora hujengwa kwa uwazi, uwajibikaji na kusikiliza maoni ya wataalamu pamoja na wananchi. Kupokea ripoti ya uchunguzi kuhusu Ngorongoro Conservation Area, Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa mapendekezo yote yatafanyiwa kazi ili kuhakikisha kunapatikana suluhisho
Indonesia
0
1
1
13
Purity Magesa retweetet
PT
PT@PaschalTemu·
Ujenzi wa maduka 60 na vizimba 69 uliopo katika soko la Bukokwa Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza unatarajiwa kugharimu zaidi ya Sh milioni 577
PT tweet media
Indonesia
0
3
4
34
Purity Magesa retweetet
PT
PT@PaschalTemu·
Jumla ya vitongoji 724 vya Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa vimesambaziwa umeme sawa na asilimia 89 ya vitongoji vyote wakati vilivyosalia vitakuwa vimekamilishwa nishati hiyo ifikapo mwaka 2030.
PT tweet media
Indonesia
0
5
4
27
Purity Magesa retweetet
Mabrouk Mabrouk
Mabrouk Mabrouk@mabrouk0161·
Zaidi ya shilingi milioni 577 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa maduka 60na vizimba 69 katika soko la Bukokwa, Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza, mradi ambao unatarajiwa kuimarisha biashara ndogondogo na kuongeza mapato ya wananchi pamoja na halmashauri
Mabrouk Mabrouk tweet media
Indonesia
0
4
4
8
Purity Magesa retweetet
Dira Ya Samia
Dira Ya Samia@DiraYaSamia·
SERIKALI YATEKELEZA UJENZI WA KM 206.33 ZA BARABARA ZA LAMI NA MIRADI 76 YA MADARAJA Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. @SuluhuSamia kupitia Wizara ya Ujenzi inaendelea kuimarisha miundombinu ya barabara na madaraja nchini kwa lengo la kurahisisha usafiri, kukuza biashara na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi. Hadi kufikia Februari 2026, Wizara ya Ujenzi imefanikiwa kukamilisha ujenzi wa kilomita 206.33 za barabara kwa kiwango cha lami, hatua inayochangia kuimarisha mtandao wa barabara na kuboresha mawasiliano kati ya maeneo mbalimbali ya nchi. Aidha, wizara imekamilisha miradi 76 kati ya 81 ya dharura ya ujenzi wa madaraja yaliyoharibiwa na mvua kubwa za El-Niño pamoja na Kimbunga Hidaya katika mikoa 22 nchini, huku miradi mitano (5) iliyobaki ikiwa katika hatua za mwisho za kukamilishwa. Kwa upande wa maendeleo ya ujenzi wa madaraja makubwa yanayoendelea kujengwa nchini, utekelezaji wa miradi hiyo umefikia hatua mbalimbali ambapo Daraja la Pangani limefikia asilimia 70, Jangwani asilimia 26, Mbambe asilimia 44, Sukuma asilimia 76, Simiyu asilimia 73, Mirumba asilimia 50, na Mitomoni asilimia 85 ya utekelezaji. Hatua hizi zinaendelea kuonyesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuimarisha miundombinu ya usafiri nchini, kurahisisha huduma za kijamii na kuchochea maendeleo ya wananchi. @ikulumawasliano #KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia
Dira Ya Samia tweet mediaDira Ya Samia tweet media
Indonesia
9
25
31
1.2K
Purity Magesa
Purity Magesa@purity1978·
Kulinda rasilimali za taifa ni jukumu la kila MtanzaniaKupokea ripoti ya uchunguzi wa masuala ya Ngorongoro Conservation Area,Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito wa ushirikiano kutoka kwa wananchi wote ili kuhakikisha urithi huu wa kipekee unaendelea kuhifadhiwa kwa manufaa yetu
Indonesia
0
4
5
21
Purity Magesa retweetet
Mabrouk Mabrouk
Mabrouk Mabrouk@mabrouk0161·
Bwawa la Kidunda linatajwa kuwa moja ya miradi mikubwa ya kimkakati ya maji nchini. Kwa uwezo wa kuzalisha hadi lita bilioni 20 za maji kila siku, mradi huu utakuwa nguzo muhimu ya kumaliza changamoto ya maji na kuimarisha ustawi wa jamii katika mikoa ya Dar es Salaam
Mabrouk Mabrouk tweet media
Indonesia
0
3
3
7
Purity Magesa retweetet
Belinda Mutashobya
Belinda Mutashobya@BMutashoby6080·
Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akibainisha kuwa Serikali itaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maji nchini, huku akisisitiza matumizi ya mitambo ya kuchimba visima kama njia ya kuharakisha upatikanaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi.
Belinda Mutashobya tweet media
Indonesia
0
2
2
8
Purity Magesa retweetet
Antidote
Antidote@Mentidote·
Mabadiliko Chanya kwa Afya na Mazingira.Uamuzi wa shule 13 za msingi Temeke kuanza kutumia umeme kupikia ni hatua muhimu katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini. Mbali na kupunguza moshi unaosababishwa na kuni
Antidote tweet media
Indonesia
1
5
5
76
Purity Magesa retweetet
Mabrouk Mabrouk
Mabrouk Mabrouk@mabrouk0161·
Mhandisi Kundo Mathew (Mb): Miradi ya maji Karatu yakikamilika huduma ya maji itafikia asilimia 89 kwa wananchi.
Mabrouk Mabrouk tweet media
Indonesia
0
4
4
9
Purity Magesa retweetet
Belinda Mutashobya
Belinda Mutashobya@BMutashoby6080·
Ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya maduka 60 na vizimba 69 katika soko la Bukokwa Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza, unaogharimu zaidi ya shilingi milioni 577, unatarajiwa kuleta mabadiliko chanya katika shughuli za biashara na uchumi wa wananchi.
Belinda Mutashobya tweet media
Indonesia
0
4
4
15
Purity Magesa retweetet
Dira Ya Samia
Dira Ya Samia@DiraYaSamia·
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. @SuluhuSamia akizungumza kwenye hafla ya kupokea Taarifa za Tume ya Rais ya Kutathmini Mgogoro wa Ardhi katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma. Ameeleza kuwa kutokana na umuhimu mkubwa wa eneo la Ngorongoro, kuna mchanganyiko wa masuala mbalimbali yanayohitaji kuzingatiwa, ikiwemo uwepo wa wananchi na mifugo yao pamoja na wajibu wa kulinda urithi wa dunia uliopo katika eneo hilo. Ameeleza kuwa hali hiyo imekuwa ikiibua swali muhimu la namna bora ya kukabiliana na mahitaji hayo yote; kwa upande mmoja watu na mifugo yao ni sehemu ya jamii ya nchi, na kwa upande mwingine Ngorongoro ni rasilimali muhimu inayopaswa kulindwa kwa manufaa ya taifa na dunia kwa ujumla. Rais Samia amesema tume imefanya kazi kubwa na kutoa mapendekezo muhimu ambayo Serikali itayafanyia kazi kwa umakini ili kupata suluhisho endelevu kwa masuala ya eneo hilo. Aidha, ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wenyeviti pamoja na wajumbe wa tume hizo kwa kukubali kubeba jukumu hilo kubwa na nyeti kwa maslahi ya taifa. Ameeleza kuwa kazi waliyopewa haikuwa rahisi kutokana na wingi wa masuala yaliyohitaji kujadiliwa, mikutano mingi waliyofanya pamoja na maoni tofauti kutoka kwa wadau mbalimbali waliokutana nao. Rais Samia amewapongeza kwa kazi yao kubwa ya kizalendo waliyoifanya kwa bidii, uadilifu na weledi mkubwa ili kutimiza kwa mafanikio jukumu walilokabidhiwa kwa manufaa ya nchi. @ikulumawasliano #KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia
Indonesia
14
22
22
918
Purity Magesa retweetet
Dira Ya Samia
Dira Ya Samia@DiraYaSamia·
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. @SuluhuSamia akizungumza kwenye hafla ya kupokea Taarifa za Tume ya Rais ya Kutathmini Mgogoro wa Ardhi katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma Ameeleza kuwa katika miaka ya nyuma kulikuwa na mjadala mkubwa kuhusu suala la Ngorongoro, ukiambatana na taarifa mbalimbali katika mitandao ya kijamii, malalamiko ya wakazi wa eneo hilo, pamoja na mashtaka yaliyowasilishwa katika taasisi tofauti za kimataifa. Rais Samia amesema hali hiyo ilimfanya mwezi Desemba mwaka 2024 kutafuta nafasi ya kukutana na viongozi wa kimila wa kabila la Wamasai pamoja na wazee wa jamii ya Ngorongoro ili kuzungumza nao moja kwa moja na kusikiliza kwa kina changamoto zinazowakabili. Amesema katika mazungumzo hayo, viongozi hao walieleza changamoto zao hususan zinazohusiana na matumizi ya ardhi, uhifadhi wa mazingira pamoja na utekelezaji wa zoezi la uhamaji wa hiari kutoka ndani ya eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kwenda maeneo yaliyotengwa na Serikali. Rais Samia amefafanua kuwa zoezi la uhamaji wa hiari lilianzishwa na Serikali kwa lengo la kutoa fursa kwa wakazi wa eneo la hifadhi waliokuwa tayari kuhama, kwa kuwapatia maeneo mbadala ya makazi pamoja na mazingira bora ya kuendeleza shughuli zao za kijamii na kiuchumi. @ikulumawasliano #KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia
Indonesia
10
23
27
1.3K
Purity Magesa retweetet
PT
PT@PaschalTemu·
Kiwango cha upatikanaji wa bidhaa za afya nchini kimefikia asilimia 88.8 mwezi Februari 2026, kikilinganishwa na wastani wa asilimia 73 mwaka 2021/22.
PT tweet mediaPT tweet media
Indonesia
0
5
6
20
Purity Magesa retweetet
PT
PT@PaschalTemu·
Utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) umefikia asilimia 81 huku ujenzi wake ukitarajiwa kukamilika Julai 2026,
PT tweet media
Indonesia
0
5
5
31
Purity Magesa retweetet
Dira Ya Samia
Dira Ya Samia@DiraYaSamia·
SERIKALI YATOA RUZUKU YA SHILINGI BILIONI 1.63 KUTEKELEZA MRADI WA UMEME WA MAJI IJANGALA NJOMBE Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. @SuluhuSamia kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa ruzuku ya shilingi bilioni 1.63 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Maji wa Ijangala uliopo wilayani Makete, mkoani Njombe. Mradi huo wa Ijangala Mini Hydropower Plant wenye uwezo wa kuzalisha kilowati 360 tayari umeunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji na uimara wa nishati ya umeme hususan katika maeneo ya vijijini. Kupitia ruzuku hiyo, miundombinu muhimu ya mradi imejengwa ikiwemo transfoma chochezi yenye uwezo wa KVA 500 pamoja na njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolt 33 yenye urefu wa kilomita 0.6 inayounganisha mradi huo na Gridi ya Taifa. Aidha, mradi huo ulipata mkopo nafuu wa shilingi milioni 922 kupitia programu ya Tanzania Rural Electrification Expansion Program (TREEP) inayosimamiwa na REA, uliosaidia kugharamia baadhi ya shughuli za utekelezaji wa mradi. Mradi huu unatekelezwa na Dayosisi ya Kusini Kati ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kupitia Kituo cha Udiakonia cha Tandala, kwa kushirikiana na Serikali katika kukuza uwekezaji kwenye nishati jadidifu na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya vijijini. @ikulumawasliano #KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia
Dira Ya Samia tweet mediaDira Ya Samia tweet media
Indonesia
7
24
29
1.3K
Purity Magesa
Purity Magesa@purity1978·
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti za Tume za Rais zilizofanya tathmini ya mgogoro wa ardhi na utekelezaji wa zoezi la uhamaji wa hiari wa wakazi wa Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino, Dodoma, tarehe 12 Machi 2026.
Purity Magesa tweet mediaPurity Magesa tweet media
Indonesia
0
2
2
13
Purity Magesa
Purity Magesa@purity1978·
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti muhimu za Tume za Rais kuhusu tathmini ya mgogoro wa ardhi na zoezi la uhamaji wa hiari wa wakazi katika Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino, Dodoma, tarehe 12 Machi 2026.
Purity Magesa tweet mediaPurity Magesa tweet media
Indonesia
0
3
3
11
Purity Magesa retweetet
PT
PT@PaschalTemu·
Ujenzi wa Bwawa kubwa la Maji la Kidunda mradi wa kimkakati unaogharimu zaidi ya Sh bilioni 335 na utakuwa na uwezo wa kuzalisha hadi lita bilioni 20 za maji kwa siku na unaolenga kumaliza kabisa changamoto ya maji katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na baadhi ya maeneo ya Morogoro.
PT tweet media
Indonesia
0
5
6
54
Purity Magesa retweetet
Mabrouk Mabrouk
Mabrouk Mabrouk@mabrouk0161·
Hatua muhimu katika kuimarisha malezi bora ya watoto imeanza jijini Arusha ambapo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amon Mpanju, amefungua kikao kazi cha siku tano
Mabrouk Mabrouk tweet media
Indonesia
0
3
3
11