Samia Suluhu

1.8K posts

Samia Suluhu banner
Samia Suluhu

Samia Suluhu

@SuluhuSamia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. President of the United Republic of Tanzania

Dodoma, Tanzania Katılım Haziran 2014
29 Takip Edilen1.8M Takipçiler
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bi. Khadija Said Salmin, Mtangazaji wa Habari wa Kwanza Mwanamke nchini Tanzania, kilichotokea leo mkoani Dar es Salaam. Tutamkumbuka na kumuenzi Bi. Khadija kwa uthubutu, weledi, nidhamu, umahiri katika kazi na mchango wake, kama mmoja wa waanzilishi wa tasnia ya habari na utangazaji nchini, uliofungua njia kwa wanawake wengi kuingia katika tasnia hiyo. Ninatoa pole kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, familia, ndugu, jamaa, marafiki, wanahabari na Watanzania wote kwa msiba huu. Inna Lillahi wa inna ilayhi raji'un.
Samia Suluhu tweet media
Indonesia
51
52
183
35.6K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Kigali, Rwanda, 19 Mei, 2026. Nimeungana na viongozi wenzangu, mashirika ya kimataifa, wawekezaji na wataalamu wa masuala ya nishati katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA). Tanzania tumepiga hatua kubwa katika uzalishaji na umeme, na sasa Dira ya Taifa inatuelekeza tufikie uzalishaji wa megawati 70,000 ifikapo mwaka 2050. Kwa muktadha huo, tunaunga mkono uendelezaji wa nishati ya nyuklia katika kuongeza kasi ya kufikia lengo hilo, ambayo pia inaendana na lengo letu la matumizi ya nishati safi na salama. Ili kufikia malengo ya uendelezaji wa nishati ya nyuklia Afrika, nimesisitiza umuhimu wa kuimarishwa ushirikiano kati ya wadau wanaohusika ili kuwezesha upatikanaji wa fedha, rasilimali watu na teknolojia. Sambamba na hayo, ni muhimu wananchi wakapewa elimu kuhusu uendelezaji nishati ya nyuklia ili wawe sehemu ya mageuzi haya.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
80
467
1.8K
57.2K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Ninaipongeza Timu ya Taifa ya Vijana ya Mpira wa Miguu chini ya miaka 17 (Serengeti Boys), kwa kufuzu kushiriki Kombe la Dunia mwaka 2026. Mafanikio haya ni fahari kubwa kwa taifa letu na ni ushahidi wa vipaji, juhudi na nidhamu ya vijana wetu katika kuipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa. Ninawatakia kila la kheri katika Mashindano ya Mataifa ya Afrika yanayoendelea. Nimeielekeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na mamlaka zote zinazohusika kuhakikisha maandalizi bora yanafanyika ili muiwakilishe vyema nchi yetu.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
31
100
280
10.5K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Ikulu, Dar es Salaam, 16 Mei, 2026. Nimekutana na kufanya mazungumzo na Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na ujumbe wake. Alhaji Dangote ni mmoja wa wawekezaji wakubwa Tanzania ambapo kiwanda chake cha saruji (Dangote Cement) mkoani Mtwara kinakuza uchumi wetu kupitia biashara ya saruji, ajira kwa Watanzania na kukuza sekta fungamanishi.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
90
245
1.1K
104.8K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Ninaipongeza Timu ya Taifa ya Wanawake ya Mpira wa Miguu chini ya miaka 20 (Tanzanite Queens), kwa kufuzu kushiriki Kombe la Dunia mwaka 2026. Ushindi wenu ni historia na heshima kubwa kwa nchi yetu, ikiwa ni mara ya kwanza Tanzania kufuzu kushiriki mashindano hayo. Ninaielekeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na mamlaka zote zinazohusika kufanya maandalizi bora yatakayoiwezesha timu yetu kuiwakilisha vyema Tanzania na Afrika Mashariki katika mashindano hayo.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
42
91
246
10.7K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Leo nimepata heshima ya kufunga Mafunzo ya Uongozi Ngazi ya Juu Kozi Namba 28 na Uongozi Daraja la Pili Kozi Namba 48 kwa Mwaka 2025/26 katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCT) cha Jeshi la Magereza jijini Dar es Salaam, ambapo wanafunzi 657 wamehitimu. Jeshi la Magereza lina nafasi muhimu katika mfumo wa haki jinai nchini. Hivyo, pamoja na kuwapongeza wahitimu, nimewasihi kuwa maarifa waliyoyapata yawe nyenzo ya mabadiliko ya kiutendaji, mathalan katika urekebishaji tabia za wafungwa, na uboreshaji taswira ya jeshi hilo, sawa sawa na mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai na maelekezo ya Dira 2050. Ili kuhakikisha wafungwa wanaoachiwa hawarudi magerezani, serikali itaweka utaratibu wa kuwapatia mitaji ili watumie ujuzi wanaoupata magerezani kujiendeleza. Aidha, nimelielekeza Jeshi la Magereza kuwa na mfumo wa TEHAMA utakaowezesha kuwafuatilia na kuwafanyia tathmini wafungwa walioachiwa, kujua walipo na shughuli wanazofanya.
Indonesia
22
83
174
8.4K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
I am deeply saddened to learn of the passing of the former President of the Republic of Botswana, His Excellency Festus Mogae. On behalf of the government and the people of the United Republic of Tanzania, I extend our heartfelt condolences to the President of the Republic of Botswana, His Excellency Duma Boko, President Mogae’s family, and the people of Botswana. May his soul rest in peace.
Samia Suluhu tweet media
English
28
83
260
13.2K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Leo Mei 8, 2026 nimeungana na wajumbe wenzangu katika Kikao cha Shina Namba 1 la Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chamwino mkoani Dodoma kilichoitishwa na Balozi wa Shina, Bi. Paulina Mkasanga, kwa mujibu wa Ibara ya 21 na 24 ya Katiba ya CCM.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
41
71
228
14.1K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Mapema leo Mei 7, 2026 katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichofanyika jijini Dodoma.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
57
74
237
16.3K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Nimekuwa na wakati mzuri Ikulu jijini Dar es Salaam leo na Rais wa Jamhuri ya Kenya Mheshimiwa William Ruto, ambaye amefika nchini kwa Ziara ya Kitaifa ya siku mbili. Pamoja na mambo mengine, tumejadili na kukubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano kwa manufaa ya nchi zetu mbili. Tumeshuhudia utiaji saini wa jumla ya Mikataba na Hati za Makubaliano nane, ambazo zinagusa sekta za kilimo, gesi, reli, ulinzi na usalama, usafiri wa majini, usalama wa bidhaa na mazao na utumishi wa umma. Biashara kati ya nchi zetu imeendelea kukua ambapo ilifikia thamani ya shilingi trilioni 1.7 mwaka 2025. Ili kukuza zaidi biashara na uwekezaji na kuwanufaisha wananchi, tumeelekeza watendaji wetu kuhakikisha ifikapo mwisho wa mwezi huu (Mei 31, 2026) vikwazo vyote visivyo vya kikodi viwe vimetatuliwa.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
93
138
469
28K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Ninawatakia kila la kheri wanangu wanafunzi wa Kidato cha Sita na Vyuo vya Ualimu kwa ngazi ya Cheti na Stashahada mlioanza mitihani yenu ya kuhitimu leo. Ninawaombea kwa Mwenyezi Mungu awape utulivu wa akili na afya njema ili mfanye mitihani kwa uaminifu, kujiamini na mafanikio. Serikali inaendelea kuwaandalia mazingira mazuri kwa hatua zinazofuata ikiwemo kuongeza mikopo na ufadhili wa masomo, kujenga vyuo vikuu katika kila mkoa na vyuo vya ufundi kila wilaya, na kuboresha mitaala ili elimu iwe bora na nafuu zaidi, iwawezeshe kujiajiri na iendane na mabadiliko ya dunia.
Samia Suluhu tweet media
Indonesia
37
109
338
14.2K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Leo, Ikulu jijini Dar es Salaam, nimempokea Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mheshimiwa Paul Kagame, aliyewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja. Tanzania na Rwanda si tu ndugu na majirani, bali pia ni washirika wa kimkakati wenye uhusiano unaoendelea kukua kwa kasi. Takribani asilimia 70 ya shehena ya Rwanda inapitia katika bandari za Tanzania. Biashara kati ya nchi zetu mbili imefikia shilingi bilioni 644 mwaka 2025, na uwekezaji kutoka pande zote mbili unaendelea kuchochea ajira na ukuaji wa uchumi kwa wananchi wetu. Katika mazungumzo yetu, tumekubaliana kuongeza kasi ya ushirikiano kwa kuondoa vikwazo visivyo vya kikodi, kuimarisha biashara na uwekezaji, na kuwekeza zaidi katika miundombinu ya usafiri na usafirishaji, mawasiliano, pamoja na nishati ya uhakika. Aidha, tutaimarisha ushirikiano katika masuala ya ulinzi, usalama na ajenda za kikanda na kimataifa. Karibu tena Tanzania, Mheshimiwa Rais.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
219
763
3.1K
159.8K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Kheri ya Siku ya Wafanyakazi Duniani. Leo nimeungana na wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi mkoani Njombe katika maadhimisho ya siku hii kitaifa, ambayo mwaka huu imefungamanishwa na utekelezaji wa Dira ya 2050 unaoanza Julai 1. Hii ni hatua ya kimkakati inayolenga kuelekeza nguvu kazi ya Taifa katika kujenga uchumi shindani, jumuishi na endelevu. Ninampongeza kila mfanyakazi kwani mafanikio tunayojivunia leo ni matokeo ya juhudi za pamoja katika sekta zote. Serikali yenu itaendelea kuimarisha fursa za ajira, kupanua fursa za kiuchumi, kuboresha mazingira na maslahi ya wafanyakazi, pamoja na kurasimisha sekta isiyo rasmi ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata kazi yenye staha, inayozingatia haki, usalama na ustawi. Ili kufikia malengo hayo tunahitaji dhamira ya pamoja, kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na weledi wa hali ya juu, huku tukidumisha amani, umoja na mshikamano wa Taifa letu.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Indonesia
51
93
257
13.9K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Ninaipongeza Klabu ya Simba kwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Muungano mwaka 2026. Mbali na burudani, michezo imeendelea kuwa daraja imara linalotuunganisha. Pia, ninazipongeza klabu zote nane zilizoshiriki mashindano hayo kwa kuonesha ushindani wa kirafiki na hamasa inayozidi kuimarisha tunu ya Muungano wetu.
Samia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet mediaSamia Suluhu tweet media
Filipino
63
114
562
26.7K
Samia Suluhu
Samia Suluhu@SuluhuSamia·
Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha mwigizaji mkongwe wa filamu nchini, Hashim Kambi kilichotokea leo, Dar es Salaam. Taifa limepoteza kipaji adhimu kilichochangia kwa kiasi kikubwa kukuza na kuitangaza tasnia ya filamu nchini. Ninatoa pole kwa Shirikisho la Filamu Tanzania, Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), wasanii wa filamu nchini, familia ya marehemu, wadau wa filamu, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na msiba huu. Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un.
Samia Suluhu tweet media
Indonesia
82
80
495
29.9K