
Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bi. Khadija Said Salmin, Mtangazaji wa Habari wa Kwanza Mwanamke nchini Tanzania, kilichotokea leo mkoani Dar es Salaam.
Tutamkumbuka na kumuenzi Bi. Khadija kwa uthubutu, weledi, nidhamu, umahiri katika kazi na mchango wake, kama mmoja wa waanzilishi wa tasnia ya habari na utangazaji nchini, uliofungua njia kwa wanawake wengi kuingia katika tasnia hiyo.
Ninatoa pole kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, familia, ndugu, jamaa, marafiki, wanahabari na Watanzania wote kwa msiba huu.
Inna Lillahi wa inna ilayhi raji'un.

Indonesia






























































