Dr Philbert
25.9K posts

Dr Philbert
@alphaLiquidsoap
Doctor in Dental Surgeon



EX-JAJI WARIOBA NI SEHEMU YA MPANGO WA MAPINDUZI YA OCT 29. Mzee Joseph Warioba,Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ananikumbusha "story" ya Waziri Mkuu wa zamani wa Nchi ya Burundi,Mh. Generali Alain Bunyoni ambaye alishiriki kuunda na kutekeleza njama za kutaka kumpindua Rais wa sasa wa Nchi ya Burundi,Mh Evarist Ndayshimiye. Haya sio mambo mageni kwa viongozi wengi wa bara la Afrika,yalikuwepo na yataendelea kuwepo. Upo ushahidi wa wazi kabisa kuwa,Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mzee JAJI mstaafu Sinde Warioba alikuwa sehemu ya waratibu wakuu wa mpango wa kuipindua Serikali ya Tanzania wa Oct 29. Kupatikana kwa taarifa hii sio tu kwamba kunastua anga la siasa la Tanzania lakini PIA kuhoji maswali magumu kuhusu nafasi ya Viongozi wakuu wastaafu katika ulinzi wa Amani na Usalama wa Taifa hili. Kwa kutambua hilo,☝🏽☝🏽Jaji Warioba ameungana na waratibu wengine wa Mapinduzi ya Oct 29 kuipinga(I)Tume ya Taifa ya Uchaguzi(II)Ripoti ya Tume ya Jaji Mkuu Mstaafu Mzee Chande na(III) kukataa pendekezo la kuundwa kwa tume ya KIJINAI kuwahoji wahusika wakuu wa mapinduzi yale. Jaji Warioba anafahamu kabisa kuwa ni lazima Tume hiyo itamwita na kumuhoji ushiriki wake kutokana na uwepo wa vikao vingi vya SIRI na Uongozi wa Juu wa Chadema Kabla ya Uchaguzi Mkuu akiwemo Mwenyekiti Tundu Lissu ambaye anashitakiwa kwa kesi ya UHAINI. Jaji Mstaafu Sinde Warioba kwa kutambua hilo☝🏽☝🏽ni kama kapigwa na "UBARIDI" na sasa kwa kushirikiana na Generali Ulimwengu ambaye mara kadhaa ameshiriki katika kamati mbalimbali za Chadema ikiwemo ile kamati iliyokutana na Mh Rais Mstaafu wa Malawi Lazarius Chakwera mwezi jana, ameanza kuratibu shutuma za Uongo dhidi ya👇🏽👇🏽 Ripoti ya Tume ya Jaji Chande,dhidi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi na dhidi ya Mh Rais Samia Suluhu Hassan. Mpango huo maalum wa Chadema na "wadau" wao ulianza juzi baada ya Generali Ulimwengu kuandaa MAHOJIANO ya "mchongo" na Jaji Warioba wakitoa shutuma nzito ambazo kwa mtu mwenye hadhi ya Waziri Mkuu Mstaafu,mtu mwenye hadhi ya Jaji wa Mahakama Kuu na Wakili ni ngumu kuzitoa bila kuwa na ushahidi wa wazi. Mpango huu ☝🏽☝🏽wa Jaji Mstaafu Sinde Warioba na Mzee Generali ulimwengu unaenda sambamba na kuanza kwa mikutano ya hadhara ya Chadema Nchi nzima,pamoja na mradi wa kusambaza UONGO mitandaoni dhidi ya Mh Rais ambao nao umeanza sambamba na miradi hiyo mingine ya Chadema. Ni hatari kwa Jaji Mstaafu na Waziri Mkuu Mstaafu wa Nchi kuutangazia Umma kwamba Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ilipiga kura yenyewe na badae kumtangaza mshindi.Kauli hii inaleta sintofahamu kubwa ndani ya Taifa. Mh Rais hapaswi kukatishwa tamaa kuelelea kuundwa kwa Tume ya kuchunguza JINAI ya Oct 29 na kwa ushauri nadhani Mh Rais anapaswa kuitangaza Tume hiyo haraka. Kila mtu lazima avune alichopanda. #MustakabaliWaAmani #TumeYaUchunguziReport Ukweli Wa Ripoti
























