AyoTV

34.1K posts

AyoTV banner
AyoTV

AyoTV

@ayotv_

Official Video Twitter page for @millardayo | We tell the best news and stories from East Africa | from the Most Subscribed to Journalist on YouTube in Africa.

Katılım Mayıs 2014
61 Takip Edilen140.2K Takipçiler
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Ndege ya Shirika la Ndege la Air Canada imegongana na Gari la Kikosi cha Zimamoto katika Uwanja wa Ndege wa LaGuardia, New York Nchini Marekani usiku wa kuamkia leo na kusababisha vifo vya Marubani wote wawili huku Watu wengine kadhaa wakijeruhiwa. Wakati huu Mamlaka zikisema zinachunguza chanzo cha ajali hiyo, taarifa za Mashuhuda zimesema kuwa Ndege hiyo ilikuwa ikikimbia kwa kasi ya takribani maili 130 kwa saa kabla ya kugonga gari hilo ambapo mawasiliano ya mnara wa kuongozea Ndege yameonesha kuwa gari hilo lilikuwa limepewa ruhusa kuvuka barabara ya Ndege. Baada ya tukio hilo, shughuli zote za Uwanja wa Ndege zimesimamishwa kwa muda ili kuruhusu huduma za dharura na uchunguzi kufanyika huku Mamlaka ya Anga ya Marekani (FAA) na National Transportation Safety Board wakianza uchunguzi kubaini chanzo halisi cha ajali hiyo. #MillardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
5
7
117
11.8K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Mvua kubwa inayoendelea kunyesha Nchini Kenya imesababisha mafuriko makubwa yaliyochukua maisha ya watu wasiopungua 81 hadi sasa, ndani ya mwezi huu, kwa mujibu wa Mamlaka za Nchi hiyo. Hali inaendelea kuwa tete huku mvua ikinyesha katika maeneo mengi, na kuongeza hofu ya kuongezeka kwa madhara zaidi. Maeneo yaliyoathirika zaidi ni pamoja na Mji Mkuu Nairobi, ambapo vifo 37 vimeripotiwa, ambapo Mafuriko hayo yamesababisha uharibifu mkubwa wa mali, hususan katika eneo la Grogan, huku Wakaazi wa maeneo ya Mabondeni na karibu na Mito wakikabiliwa na hatari kubwa zaidi. Katika Kaunti ya Kisumu, hasa eneo la Nyakach, hali ni mbaya zaidi ambapo mafuriko ya ghafla yamefunika Vijiji na kuharibu takriban ekari 3,000 za mashamba yenye mazao, huku zaidi ya Familia 3,000 zikilazimika kuyahama makazi yao, na baadhi yao wakihifadhiwa katika Vituo vya Muda vya Uokoaji kutokana na kuongezeka kwa Maji ya Mto Mirui. Maafisa wa Serikali wamewataka Wananchi wanaoishi katika maeneo hatarishi kuhama haraka, wakionya juu ya uwezekano wa kuongezeka kwa mafuriko, hasa karibu na Bwawa la Nairobi. Wakati huo huo, Idara ya Hali ya Hewa imetahadharisha kuwa mvua itaendelea kunyesha hadi Jumanne ijayo, hali inayoweza kuzidisha zaidi athari zilizopo. #millardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
2
6
94
4.8K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Mkuu wa Shirika la Nishati la Kimataifa - IEA Fatih Birol amesema kwamba Uchumi wa dunia uko chini ya "tishio kubwa" kutokana na mgogoro wa Nishati unaosababishwa na vita vya Mashariki ya Kati. Akiongea katika hafla ya Waandishi wa Habari katika Mji Mkuu wa Australia, Birol ameulinganisha mgogoro wa sasa wa Nishati na ule wa miaka ya 1970, na athari za uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine mwaka wa 2022. Mkuu huyo wa IEA amesema takribani vituo arobaini vya Nishati vimeharibiwa kwa kiasi kikubwa huko Mashariki ya Kati kutokana na vita katika eneo hilo. Amesema mambo yalivyo sasa ni kuwa kuna migogoro miwili ya mafuta na mmoja wa gesi, ambayo imeunganishwa pamoja, na kuongeza kuwa anatumai hali hiyo itatatuliwa haraka iwezekanavyo akiongeza kuwa IEA inashauriana na Serikali za Asia na Ulaya kuhusu kutolewa kwa mafuta ya akiba kama itahitajika. Hata hivyo, Mataifa Wanachama wa IEA walikubaliana Machi 11 kutoa mapipa milioni 400 ya mafuta kutoka kwenye hifadhi za kimkakati ili kupambana na kupanda kwa bei za mafuta ghafi duniani. #MillardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
0
4
72
5.4K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Bunge la Korea Kaskazini, linalojulikana kama Bunge Kuu la Watu (Supreme People's Assembly), limefuta mashaka yote kwa kumteua upya Kim Jong Un kuwa Rais wa Masuala ya Jimbo, jukumu linalompa Mamlaka ya juu ya Kiongozi wa Taifa. Televisheni ya taifa hilo (Korean Central Television), imeripoti kufanyika kwa uteuzi huo katika kikao cha Bunge kilichofanyika Jumapili Machi 22, 2026, Mjini Pyongyang, ambapo pia ilitangazwa kuwa Mshirika wake wa karibu, Jo Yong Won, amechukua nafasi ya Choe Ryong Hae kama Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge. Karibu 40% ya Mawaziri katika Serikali wameteuliwa upya, hatua inayoashiria mabadiliko ya Viongozi kufuatia Mkutano wa Chama Tawala cha Workers' Party mwezi uliopita, huku Ajenda ya kikao hicho ikiwa ni pamoja na marekebisho ya Katiba, mpango wa maendeleo ya kiuchumi uliotangazwa katika mkutano na Bajeti ya Taifa, ingawa maelezo kamili hayajafahamika. Kikao cha Bunge kimepangwa kuendelea, huku macho ya wengi yakiwa yamelenga kama Kim Jong Un ataeleza mtazamo wake kuhusu uhusiano na Marekani. #MillardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
5
9
299
14.3K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza kuahirisha mashambulizi yaliyokuwa yamepangwa kufanywa dhidi ya mitambo ya umeme na miundombinu ya nishati nchini Iran kwa kipindi cha siku tano. Kupitia taarifa yake, Trump amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya mazungumzo yaliyofanyika kwa siku mbili kati ya Marekani na Iran, ambayo ameyataja kuwa yalikuwa mazuri, yenye tija, na yenye kujenga mwelekeo wa kumaliza kabisa uhasama kati ya pande hizo katika ukanda wa Mashariki ya Kati. Ameeleza kuwa mazungumzo hayo yataendelea katika siku zijazo, huku akisisitiza kuwa hatua ya kuahirisha mashambulizi inalenga kutoa nafasi kwa diplomasia kufanikisha suluhisho la kudumu. Trump ameongeza kuwa hatua hiyo itategemea mafanikio ya mazungumzo yanayoendelea, akieleza matumaini kuwa pande zote mbili zinaweza kufikia makubaliano yatakayomaliza mivutano iliyokuwepo kwa muda mrefu. Hatahivyo, Rais huyo aliwashukuru wote wanaofuatilia maendeleo hayo na kusisitiza umuhimu wa juhudi za amani katika eneo hilo. #MillardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
30
11
263
20.4K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi ameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kuhakikisha kuwa, hakuna Mfanyabiashara anayeficha mafuta kwa kisingizio cha kusubiri bei za mafuta zipande kutokana na mgogoro unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati ambao umepelekea baadhi ya Nchi kukumbana na changamoto za upatikanaji wa mafuta. Akiongea Jijini Dodoma leo Machi 23,2026 katika Kikao na Taasisi za Wizara zinazosimamia Sekta ya Mafuta, Ndejembi ameeleza kuwa Nchi ina usalama mkubwa wa mafuta na kwamba Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha Wananchi katika maeneo yote wanapata huduma bila vikwazo hivyo EWURA anapaswa kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa katika maghala ya kuhifadhi Mafuta. #MillardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
0
6
111
5.3K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia, Dkt. James Mataragio, amewahakikishia Watanzania kuwa Nchi ya Tanzania ina akiba ya kutosha ya mafuta hadi Mwezi July 2026. Akiongea leo March 23,2026 Jijini Dodoma mbele ya Waziri wa Nishati, Deo Ndejembi, Mataragio amesema Serikali ilichukua hatua za mapema kwa kushirikiana na Taasisi zake, ili kuhakikisha kunakuwa na uhakika wa upatikanaji wa mafuta na kwa gharama himilivu. Amesema Wizara itaendelea kusimamia Taasisi zake ili kuhakikisha mafuta yaliyopo njiani yanafika kwa wakati, pamoja na kuwadhibiti Wauzaji ili wasitumie changamoto iliyopo kama fursa ya kupandisha bei. #MillardAyoUPDATES.
millardayo tweet media
Indonesia
20
9
219
10.7K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Mtoto Rajab Mohamed (12), Mkazi wa Kitongoji cha Kaloleni Kata ya Italagwe Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro amejinyonga hadi kufa kwa kutumia Mkanda. Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Alex Mkama amesema Mtoto huyo amejinyonga baada ya kugombwezwa na Wazazi wake aache tabia ya wizi. Kamanda Mkama amesema Mtoto huyo pamoja na wenzake wawili waliakamtwa wameiba mahindi mabichi baada ya kuambiwa aache tabia ya wizi ndipo akazunguka nyuma ya Nyumba usiku wa kuamkia leo machi 23 na kujinyonga kwa kutumia Mkanda wake. #MillardAyoUPDATES.
Indonesia
6
4
47
5.7K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Iran imechapisha video mpya kupitia Televisheni ya Taifa, Islamic Republic of Iran Broadcasting (IRIB) ikidai kuonyesha ghala kubwa la silaha lililofichwa chini ya ardhi. Video hiyo imeonyesha safu za Makombora yaliyohifadhiwa, huku maelezo yakisisitiza kuwa ni “sehemu ndogo tu” ya hifadhi halisi ya Kijeshi ya Taifa hilo. Hatua hiyo imekuja wakati mvutano ukiongezeka huko Mashariki ya Kati ukihusisha Marekani, Israel pamoja na Iran ambapo tahadhari kuhusu uwezo wa Kijeshi wa Iran ukiendelea kuchukua sura mpya. #MillardAyoUPDATES
Indonesia
23
27
308
30.1K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Rais wa Urusi Vladimir Putin amempongeza Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un kwa kuchaguliwa tena kuliongoza taifa hilo, akieleza matumaini ya kuimarika zaidi kwa uhusiano kati ya mataifa hayo mawili. Kwa mujibu wa Vyombo vya Habari vya Korea Kaskazini, Kim amethibitishwa tena katika wadhifa huo wa Rais wa Masuala ya Jimbo, jukumu linalompa Mamlaka ya juu ya Kiongozi wa Taifa, wakati wa kikao cha kwanza cha Bunge Kuu la Watu kilichofanyika Jumapili 22, 2026, hatua inayompa muhula wa tatu mfululizo tangu kuanzishwa kwa tume hiyo mwaka 2016. Katika ujumbe wake wa pongezi, Putin amesema Urusi inathamini mchango wa Kim katika kuimarisha ushirikiano wa kirafiki na kuahidi kuendeleza zaidi ushirikiano wa kimkakati kati ya Moscow na Pyongyang. Aidha, katika miaka ya hivi karibuni, Urusi na Korea Kaskazini zimeendelea kuimarisha mahusiano yao, ikiwa ni pamoja na kusaini makubaliano ya ulinzi mwaka 2024, huku Korea Kaskazini ikiripotiwa pia kuitumia Urusi msaada wa Kijeshi katika vita dhidi ya Ukraine. #MillardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
1
8
185
5.8K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Gesi ya TotalEnergies ni bei nafuu kwa nini wasijilambe? Jipatie mtungi wa kilo 13 pamoja na vifaa vyake vyote kwa bei nafuu katika vituo vya @totalenergies_tz vilivyopo Arusha, Dar es Salaam, Dodoma na Kilimanjaro. #TotalEnergiesTZ #GesiBingwaPishiPambe
millardayo tweet media
हिन्दी
0
3
18
2.7K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Mwanaume aliyefahamika kwa jina la Reuben Chedego (70) Mkazi wa Chalinze Mkoani Pwani amefariki Dunia muda mchache baada ya kushuka kwenye gari katika Kituo Kikuu cha Mabasi Msamvu Morogoro. Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoani Morogoro SACP, Alex Mkama amesema tukio hilo limetokea Machi 22, 2026 majira ya jioni katika kituo hicho cha mabasi ambapo mtu huyo alienda kujisaidia haja ndogo chooni ndipo akaishiwa nguvu na kudondoka. Kamanda Mkama amesema baada ya kudondoka alifikishwa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro alikuwa tayari ameshafariki kwa sasa mwili huo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro na amewataka ndugu wa Marehemu kufika Hospitali hiyo kwa ajili ya kuchukua mwili kwa ajili ya taratibu za mazishi. #MillardAyoUPDATES
Filipino
2
7
151
25.4K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Shilingi elfu mbili ndio ilimfanya aiwashe pikipiki yake ili kuishindania lakini leo tunazungumza naye akiwa hana mguu mmoja kutokana na ajali aliyopata katika ‘chalenji’ hiyo iliyopelekea kukatwa mguu wake wa kushoto. Jina lake ni Salehe Saidi (30), Mkazi wa Makoroea Mkoani Tanga ambaye alipata ajali na Rafiki yake wakishindania shilingi elfu mbili iliyoyageuza maisha yake kuwa ya tabu kwa sasa. #MillardAyoUPDATES
Filipino
5
10
119
21.3K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) imemtia nguvuni Waziri wa Zamani Nchini Kenya, Raphael Tuju, ambaye Familia yake ilidai ametekwa kabla ya kujitokeza na kukiri alikuwa mafichoni siku ya Jumamosi baada ya kuhisi kuwa kuna watu waliokuwa wakimfuata. Akizungumza baada ya Tuju kuonekana akiwa ndani ya Nyumba yake Kaumbu, Mkurugenzi wa DCI, Amin Mohamed, amesema uchunguzi wa kina wa kuthibitisha kuonyesha kwamba madai yake yalikosa ukweli. Amin amesema kuwa Tuju alikuwa amejificha ndani ya Makazi yake muda wote wa kutoonekana kwake, huku timu ya uchunguzi ikituma uchunguzi maalumu baada ya taarifa ya kutoweka kwake kuwasilishwa Jumamosi. Aidha, taarifa zinasema kuwa Waziri Tuju alifanya hivyo kutokana na kwamba alishindwa kulipa mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki, na sasa Benki hiyo inataka kuchukua mali zake, Tuju akituhumu baadhi ya Watu Mashuhuri Serikalini kwa kuhusika kwenye mzozo huo. #MilardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
8
5
131
9.3K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Serikali ya Zanzibar inaendelea na uaandaji wa mifumo kwa kushirikiana na vVombo vya Kimataifa kuhakikisha inapambana na janga la utakatishaji wa fedha haramu kutokea sehemu mbalimbali. Hayo yamejiri maara baada ya Kikao Kazi na Wadau wa Kimataifa pamoja na Wadau wa Sheria Zanzibar ambapo Kaimu Waziri wa Biashara Zanzibar Ambae pia ni Waziri wa Kazi na Uwekezaji Shariff Shariff, amesema hivi sasa Taasisi za Serikali zimeshaanza kutumia mifumo ya kidijitali Kwa upande wake, Mkurugenzi wa BPRA Khamis Juma Khamis, amesema taasisi hiyo ya Serikali ambayo ndio geti la Makampuni limejipanga kushughulikia kimifumo janga hilo la utakatishaji wa fedha haramu kwa kushirikiana na Taasisi za Kimataifa ikiwemo European Union. #MillardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
2
5
46
3.4K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Ndege ya Kijeshi iliyokuwa imebeba Watu 125, wengi wao wakiwa Wanajeshi, imeanguka muda mfupi baada ya kupaa katika Mji wa Puerto Leguizamo Nchini Colombia, na kusababisha vifo vya Watu wasiopungua 66 huku wengine wengi wakijeruhiwa. Taarifa za awali zinaeleza kuwa ajali hiyo imetokea ghafla baada ya Ndege kushindwa kuendelea na safari yake. Naibu Meya wa eneo hilo, Carlos Claros, amesema kuwa takribani Watu 81 wamejeruhiwa katika tukio hilo, huku juhudi za uokoaji zikiendelea kwa haraka. Vikosi vya Uokoaji pamoja na Wakazi wa eneo hilo wamejitokeza kusaidia kuokoa manusura na kuwapeleka katika vituo vya matibabu. Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi Pedro Sanchez amesema Ndege hiyo ilikuwa ikiwapeleka Wanajeshi katika Jimbo la Amazon karibu na mipaka ya Ecuador na Peru, na kuongeza kuwa hadi sasa hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa ajali hiyo imesababishwa na shambulio kutoka kwa makundi ya Waasi yanayofanya shughuli zao katika eneo hilo. Jeshi la Anga linaendelea kufanya uchunguzi kubaini chanzo halisi cha ajali hiyo, huku taarifa zikieleza kuwa baadhi ya manusura wameokolewa wakiwa na majeraha mbalimbali. Wakati huo huo, video zinazosambaa zinaonyesha Wanajeshi wakiondolewa eneo la tukio kwa msaada wa Wakazi, huku wengine wakijitahidi kuzima moto uliosababishwa na Ndege hiyo. #MillardAyoUPDATES.
millardayo tweet media
Indonesia
1
4
80
4.9K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Un, ameionya Korea Kusini kwamba itaendelea kumchukulia kama adui yake mkubwa na kwamba Nchi hiyo haitawahi kuachana na Silaha za Nyuklia. Akizungumza mbele ya Bunge la Taifa hilo, Kim amesema Korea Kaskazini itaendelea kuimarisha nguvu zake za Nyuklia kama hatua ya kujilinda dhidi ya kile alichokiita vitisho kutoka nje, hasa Marekani na Washirika wake. Kim amesisitiza kuwa hatua yoyote kutoka Korea Kusini itakayochukuliwa kama uchokozi itajibiwa bila huruma wala kusita, akiongeza kuwa Pyongyang haitazingatia tena juhudi zozote za mazungumzo kutoka Seoul. Kauli hiyo inakuja wakati Rais wa Korea Kusini, Lee Jae Myung, akiendelea kusisitiza mazungumzo ya Amani bila masharti, jambo ambalo hadi sasa limepuuzwa na Korea Kaskazini. Kwa sasa, mvutano kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini unaendelea kuongezeka, hali inayozua wasiwasi mkubwa wa usalama katika eneo la Asia Mashariki. #MilardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Indonesia
10
11
434
26.6K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
China imesisitiza kuwa itaendeleza juhudi zake za kuwa mpatanishi wa Kidiplomasia katika mgogoro wa Mashariki ya Kati, licha ya kukiri kuwa haina uwezo mkubwa wa kumaliza mzozo huo. Mjumbe maalum wa China katika eneo hilo, Zhai Jun, amesema Beijing “haitapumzika” katika kutafuta suluhu ya Amani, akiongeza kuwa nguvu za Kijeshi hazipaswi kutumika kiholela dhidi ya Mataifa mengine. Akizungumza Jijini Beijing baada ya ziara katika Nchi kadhaa za Ghuba na Afrika Kaskazini, Zhai alizitaka Marekani na Israel kusitisha mashambulizi yao mara moja ili kutoa nafasi kwa mazungumzo ya kusitisha mapigano. Aidha, ameeleza kuwa China imefanya mazungumzo ya kina na Iran, lakini akasisitiza kuwa suluhu ya kweli inapaswa kuanzia kwa wahusika wakuu wa mgogoro huo. Katika kauli yake, Zhai alionya pia dhidi ya mashambulizi yanayolenga Raia na miundombinu muhimu, pamoja na kuhatarisha usalama wa njia muhimu za Biashara kama Mlango wa Bahari wa Hormuz. Kauli hiyo inaonyesha juhudi za China kujionyesha kama nguvu mbadala ya kidiplomasia katika eneo hilo, wakati mvutano ukiendelea kuongezeka kati ya Iran, Israel na washirika wao #MillardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Filipino
1
7
122
5.9K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amezema Wizara hiyo imeanza mazungumzo na UNESCO pamoja na Uongozi wa META, (Kampuni Mama inayomiliki Faceebok, Instagram na WhatsApp), ili Lugha ya Kiswahili kitambulike rasmi kwenye Majukwaa ya Kimtandao (platform), kote duniani ili Vijana wanaotengeneza maudhui kwa Kiswahili walipwe pesa. Akiongea Jijini Arusha wakati wa Kongamano la Idhaa za Kiswahili leo Machi 24, 2026, Makonda amesema. “Tumefanya mazungumzo Wizara yetu na tunaendelea kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa UNESCO pamoja na Viongozi wa META Duniani, Vijana wa Tanzania wanaotengeneza content wakipost kwa Lugha ya kiswahili kwakuwa Kiswahili bado hakijatambulika kwenye platform za mitandao ya kijamii malipo yao ni madogo” “Tunayo maudhui mazuri mengi lakini hatutengenezi pesa kama wenzetu wanaopost kwa Lugha ya Kiingereza, leo hii unamkuta Mtu wa Tanzania ana followers zaidi ya milioni 3, akipost wanaoview ni wengi ila hapati hela Instagram, Facebook, TikTok hawawalipi kwasababu Kiswahili bado Watu wa META na wenye platform ya mitandao Duniani hawajakitambua kama lugha rasmi” “Wizara yetu na UNESCO tumeanzisha mazungumzo na tuna Imani ndani ya mwaka huu Mungu akitujalia Kiswahili pia kitatambulika rasmi kwenye platform zote Duniani ili Vijana watengeneze pesa Tanzania” #MilardAyoUPDATES
millardayo tweet media
Filipino
30
9
249
16K
AyoTV retweetledi
millardayo
millardayo@millardayo·
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amezema Wizara hiyo imeanza mazungumzo na UNESCO pamoja na Uongozi wa META, (Kampuni Mama inayomiliki Faceebok, Instagram na WhatsApp), ili Lugha ya Kiswahili kitambulike rasmi kwenye Majukwaa ya Kimtandao (platform), kote duniani ili Vijana wanaotengeneza maudhui kwa Kiswahili walipwe pesa. Akiongea Jijini Arusha wakati wa Kongamano la Idhaa za Kiswahili leo Machi 24, 2026, Makonda amesema. “Tumefanya mazungumzo Wizara yetu na tunaendelea kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa UNESCO pamoja na Viongozi wa META Duniani, Vijana wa Tanzania wanaotengeneza content wakipost kwa Lugha ya kiswahili kwakuwa Kiswahili bado hakijatambulika kwenye platform za mitandao ya kijamii malipo yao ni madogo” “Tunayo maudhui mazuri mengi lakini hatutengenezi pesa kama wenzetu wanaopost kwa Lugha ya Kiingereza, leo hii unamkuta Mtu wa Tanzania ana followers zaidi ya milioni 3, akipost wanaoview ni wengi ila hapati hela Instagram, Facebook, TikTok hawawalipi kwasababu Kiswahili bado Watu wa META na wenye platform ya mitandao Duniani hawajakitambua kama lugha rasmi” “Wizara yetu na UNESCO tumeanzisha mazungumzo na tuna Imani ndani ya mwaka huu Mungu akitujalia Kiswahili pia kitatambulika rasmi kwenye platform zote Duniani ili Vijana watengeneze pesa Tanzania” #MillardAyoUPDATES
Filipino
4
5
40
3.7K