Tweet fixado
ALLIIGATOR TEARS
10.8K posts

ALLIIGATOR TEARS
@SunKey1367
Identity is a joke
Dar es Salaam, Tanzania Entrou em Eylül 2017
521 Seguindo360 Seguidores

The Rolling Stone Review — @raye's 'This Music May Contain Hope'
"It’s one long pageant starring Raye as not just the main character, but the only character, piling on the Old Hollywood strings and juicy narrative detail."
⭐️⭐️⭐️⭐️ + 1/2

English

George Sanga, msaliti wa Watanzania, amezua mjadala mpana katika jamii kufuatia hatua yake ya kubadili msimamo na kuacha njia ya mapambano ya haki na demokrasia. Kitendo chake kinatazamwa na wengi kama usaliti mkubwa dhidi ya jitihada za pamoja zilizojengwa kwa muda mrefu kwa gharama na mchango wa wananchi waliomuamini na kumsimamia katika nyakati ngumu.
Kwa mujibu wa kumbukumbu za matukio yaliyoshuhudiwa na umma, George Sanga aliwahi kukumbwa na kesi nzito ya mauaji iliyokuwa na adhabu kali. Katika kipindi hicho kigumu, Watanzania waliinuka kwa pamoja na kumuunga mkono kwa hali na mali, wakimchangia fedha za chakula akiwa gerezani, kusaidia familia yake kwa mahitaji ya kila siku, pamoja na kugharamia ada ya elimu ya mtoto wake. Baada ya kutoka gerezani, wananchi hao hao walimchangia mtaji ili aweze kurejea katika maisha ya kawaida.
Vilevile, viongozi na wanachama wa CHADEMA walionyesha mshikamano mkubwa kwa kufunga safari kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania kwenda kumtembelea na kumtia moyo alipokuwa kifungoni. Hatua hizi zilidhihirisha wazi imani na matumaini makubwa yaliyowekwa juu yake kama sehemu ya harakati za kuleta mabadiliko ya kweli nchini.
Hata hivyo, katika hali inayozua masikitiko makubwa, George Sanga ameondoka katika chama hicho na kujiunga na CHAUMA, huku akianza kutoa kauli za kejeli na dharau kwa wapigania haki na demokrasia. Aidha, hatua yake ya kuonekana kuwatetea wale waliowahi kumuweka gerezani imeibua hisia kali za kusalitiwa miongoni mwa wananchi waliowahi kusimama naye.
Mabadiliko haya ya ghafla ya msimamo yanaibua maswali makubwa kuhusu uaminifu, uadilifu na dhamira ya kweli ya viongozi ndani ya harakati za kijamii na kisiasa. Jamii inatarajia uwajibikaji na msimamo thabiti kutoka kwa wale wanaopewa dhamana ya kuongoza na kuwakilisha sauti za wananchi.
Wito unatolewa kwa wadau wote wa haki na demokrasia kuendelea kuwa imara, kushikamana na kutetea misingi ya haki na ukweli bila kuyumbishwa na matukio ya mtu mmoja. Mapambano ya haki na demokrasia hayawezi kusimamishwa na mabadiliko ya msimamo ya mtu binafsi, bali yataendelea kwa nguvu ya umma.

Indonesia

VIDEO:
Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, amesema kuwa marehemu William Lukuvi alikuwa na moyo wa kujituma na kujitoa kikamilifu katika kazi, akibainisha kuwa hadi jana alikuwa ofisini licha ya kujisikia vibaya na kwenda hospitali kisha kurejea kazini kuendelea na majukumu yake.
Akizungumza leo Machi 25, 2026 msibani nyumbani kwa marehemu eneo la Area D, jijini Dodoma, Chongolo amesema taifa limepoteza mtu muhimu mwenye uzoefu, hekima na busara ambazo bado zilihitajika kulisaidia taifa pamoja na Bunge.
Marehemu William Lukuvi, aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Watu wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani tangu mwaka 1995, amefariki dunia leo Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma kutokana na mshtuko wa moyo.
Filipino




















