Anthony Mavunde
145 posts

Anthony Mavunde
@AnthonyMavunde
Mtumishi wa Watu "De Populo Servorum"
Dodoma Katılım Aralık 2011
77 Takip Edilen4.9K Takipçiler

Uzinduzi wa Kampeni ya Ugawaji wa Mipira Milioni moja kwa lengo la kuibua na kuviendeleza vipaji vya watoto wa Kitanzania#1mBallCampaign#



Indonesia

Leo nimeanza rasmi ziara ya siku mbili wilaya ya Chunya mkoani Mbeya. Chunya ni mkoa wa kimadini na kimkakati. Shughuli za uchimbaji madini katika Wilaya ya Chunya zinafanyika katika maeneo tofauti kama vile Itumbi, Makongolosi, Sangambi, Ifumbo, Matundasi na Mbugani. Uchimbaji huu umetawaliwa na Wachimbaji Wadogo kwa asilimia kubwa. Ajira zitokanazo na shughuli za uchimbaji katika Wilaya ya Chunya ni zaidi ya Watu 50,000.
Mwenendo wa Makusanyo ya Maduhuli ya Serikali Katika Mkoa wa kimadini wa Chunya umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka. Kwa mwaka Jana 2022/23 Chunya peke yake tumekusanya zaidi ya Shilingi 30 Bilioni na mwaka huu 2023/24 mpaka kufikia mwezi Mei tumeshakusanya zaidi ya Shilingi 34 Bilioni.
Mpaka sasa Chunya ina leseni za uchimbaji mdogo (Primary Mining Licence) na leseni za uchimbaji wa kati wa madini (Mining Licence) na haina leseni za uchimbaji mkubwa wa madini (Special Mining Licence). Tunahamasisha utafiti mkubwa ufanyike ili tufungue migodi mikubwa katika mkoa huu muhimu wa kimadini.
Mafanikio mengi yamepatikana kupitia soko la madini wilayani Chunya. Kabla ya kuanzishwa soko hili, dhahabu iliyokuwa ikionekana katika takwimu za Serikali ni 20kg tu na baada ya uanzishwaji wake wastani wa zaidi ya 250kg kwa mwezi zinapitia soko hili, hii sawa na ongezeko la mara 12.
Tunazipongeza taasisi za kifedha kwa ushiriki wao katika sekta ya madini kwa kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini ambapo hadi sasa wachimbaji zaidi ya 30 wa Chunya wamefaidika na mikopo toka Benki ya NMB na 20 toka Benki ya CRDB.
Katika salamu zangu kwa watumishi wa ofisi ya Chunya, nimewapa salamu mahsusi toka kwa Mhe. Anthony Mavunde Waziri wa Madini na Mhe. Steven Kiruswa Naibu Waziri wa Madini. Katika salamu hizo tumewahakikishia kutatua changamoto za vitendea kazi ndani ya mwaka ujao wa fedha. Pia tumepokea rai yao juu ya kuongeza uhamasishaji wa kuwatafutia mitaji wachimbaji wadogo, tumewaahidi kuja na mbinu mbadala za utafutaji mitaji (alternative financing).
Mwisho, nimewakumbusha kuongeza kasi ya makusanyo ya maduhuli, kutatua migogoro, kupiga vita utoroshaji madini na rushwa.
#MadiniYetu #MadiniNiMaishaNaUtajiri #Chunya #WachimbajiWadogo #TanzaniaMining @MadiniTanzania @GileadTeri @AnthonyMavunde @KiruswaS




Indonesia

Nimefanya ziara ya kukagua skimu za umwagiliaji Wilaya ya Manyoni,Mkoani Singida.Serikali itajenga bwala kubwa la kuhifadhi Maji eneo la Mbwasa kwa gharama ya Tsh 20bn na hivyo kupelekea kuwa na chanzo cha uhakika cha maji#Ajenda10/30#




Indonesia
Anthony Mavunde retweetledi

Makamu wa Rais @dr_mpango tarehe 1 Agosti 2022 akifungua Rasmi maonesho ya Nanenane 2022 yanayofanyika katika Uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya. @HusseinBashe @AnthonyMavunde @tzagriculture


Indonesia
Anthony Mavunde retweetledi

Malengo ya upanuzi wa bandari ya Mtwara uliofanywa na Mhe. Rais Samia Suluhu, ni pamoja na kurahisisha usafirishaji wa korosho.
#MamaAnafanikisha: Kampuni ya Sibatanza imetumia bandari ya Mtwara kusafirisha korosho tani 15,800 zilizokuwa zimesalia katika mavuno ya msimu uliopita

Indonesia



















