Goodluck Gabriel retweetledi

Tanzania Kupanda katika viwango vya nchi zenye mazingira bora ya uwekezaji Afrika ni ishara ya kuwepo kwa jitihada za maksudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.
Hatua mojawapo ni ya hivi karibuni tu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji), Profesa Kitila Mkumbo kukabidhi hati za ardhi kwa wawekezaji sita katika Mji Maalumu wa Kiuchumi wa Bagamoyo (BEMC SEZ)
Prof. Kitila alibainisha kuwa mwaka 2024 Tanzania ilikuwa nafasi ya 11 kwa uwekezaji Afrika na mwaka huu imepanda na kufikia nafasi ya tisa ikiongozwa na Kisiwa cha Shelisheli, Mauritius, Misri, Afrika Kusini, Morocco, Ghana, Algeria na Ivory Coast.
Profesa Kitila alisema Serikali ilianzisha programu za vielelezo saba kote nchini ambazo ni utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 na Eneo Maalumu la Kiuchumi la Bagamoyo ni mojawapo. Sambamba na hilo, imesema kwa mwaka 2025 miradi ya uwekezaji iliyosajiliwa imeongezeka na kufikia 915 yenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 10.95.
Aidha, katika eneo hilo lenye ekari 9,800 Serikali inatarajia kujenga Bandari ya Bagamoyo, ukanda maalumu wa ujenzi wa meli na kituo cha usafirishaji, kituo maalumu cha matumizi ya nishati safi na eneo litakojengwa mji mpya wa kisasa.
“Sisi ni wa tisa kwa kuwa na mazingira bora ya uwekezaji Afrika, na kabla ya mwaka 2021 Tanzania kwenye orodha ya nchi zinazovutia uwekezaji ilikuwa haionekani sasa hivi tumewazidi majirani,” alisema Profesa Kitila.
Prof Kitila amesisitiza kuwa eneo hilo lina maeneo 60 ya uwekezaji na Serikali imeanza na wawekezaji sita watakaowekeza katika ujenzi wa viwanda na chuo, akisisitiza wawekezaji kujitokeza. miradi hiyo itakapotekelezwa, Sh trilioni nane zinatarajiwa kuwekezwa katika eneo hilo ikiwa ni uwekezaji mkubwa kutoka ndani na nje ya nchi.

Indonesia








