
Habari watanzania....
Chief Suleimān M. M. Baitani
22.1K posts

@MBaitani
PCVE Expert|Views are mine😉|Justice Lover ⚖️|Quran is my 📖|+259 (Zanzibar)|Ibwera my roots|Co-Founder @kijana_hai| Zanzibar National Coordinator - THRDC

Habari watanzania....








Matokeo ya Urais yametoka kabla ya matokeo ya ubunge? And how did they manually count 30+ million votes in 3 days? This level of rigging will be studied in years to come.




*Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umefanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania* Leo Mei 05, 2025 Mratibu wa Kitaifa THRDC, Wakili Onesmo Olengurumwa na Wakili Paul Kisabo Mkuu wa Idara ya Utetezi THRDC wamefanya ziara ya kimkakati na kukutana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson. Ziara hiyo imefanyika katika Ofisi ndogo ya Bunge iliyopo jijini Dar es Salaam. Lengo kuu la ziara hiyo lilikuwa ni kueleza shughuli ambazo THRDC na Washirika wake ambao ni Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika Mashariki (EALS), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) na Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika (PALU) wamepanga kuzifanya kwa kushirikiana na wadau wa masuala ya haki za binadamu, taasisi zinazohusika na utawala wa Sheria nchini ili kuimarisha mchango wa Bunge katika masuala ya utawala wa sheria na haki za binadamu nchini. Vilevile, THRDC imewasilisha ombi kwa Mhe. Spika la kuanzishwa kwa Kamati Maalumu ya Bunge ya Masuala ya Haki za Binadamu ambayo wabunge watashirikiana na Watetezi wa haki za binadamu na Mashirika ya haki za binadamu katika kufanya kazi kwa pamoja. Mhe. Dkt. Tulia amepongeza jitihada zinazofanywa na THRDC na washirika wake katika kuimarisha ushirikiano na taasisi zinazohusika na masuala ya haki za binadamu na utawala wa sheria nchini. Ameahidi kuwa ofisi yake itatoa ushirikiano katika shughuli ambazo THRDC na washirika wake wanazifanya. Ziara hii ni sehemu ya utekelezaji wa mradi ambao Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika Mashariki (EALS), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) na Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika (PALU) wanafadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) unaolenga “Kuboresha Utawala wa Sheria, Utawala Bora, Nafasi ya Kiraia, na Uwajibikaji nchini Tanzania kupitia Ushirikiano Ulioimarishwa.” *Imetolewa na:* *Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC)* *05 Mei 2025*












