Mpale Mpoki
3.6K posts

Mpale Mpoki
@MpaleMpoki


"Sheria ipo wazi sana .Ukiondoka Uwanjani na kurudi tena tafsiri yake wewe tayari umepoteza mechi.Morocco wametumia sheria iliyopo kudai haki yao na wameipata.Hongera sana kwao kwa kuongeza Kombe lingine la AFCON " George Weah - Mchezaji wa zamani wa timu ya AC MILAN











Uamuzi wa Mahakama ya Afrika Juu ya Haki za Watu na Haki za Binadamu hapo jana kwenye kesi ya Ado Shaibu na Wenzake Dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka msingi wa kisheria kuwa matokeo ya urais yanapaswa kuhojiwa mahakamani. Hii ni hatua nzuri ya kuanzia.


Nchi hii hakuna sheria wala utaratibu wa polisi kupangia mtu aende wapi, au asiende wapi.. Polisi Tanzania hawana mamlaka kisheria wala kikatiba kuingilia uhuru wa watu kwenda wanapotaka wao wenyewe.. Polisi Nchi nzima wameweka barriers wanakamata viongozi na wanachama wa Bawacha waliokua wanaenda Musoma kusherekea Siku ya wanawake Duniani. Magari yaliyobeba viongozi hawa yanakamatwa na wanashikikiwa maeneo mbalimbali ya Nchi bila sababu… Dakawa, Mlandizi, Geita na maeneo mengine. Hili jaribio la kuzia watu kufanya movement ndani ya Nchi na kuzia watu kufanya shughuli zao halali, Wengine wanaweza kufikiri litaishia kwa Chadema.. Tukiruhusu madikteta wachache wao ndio waamue, wapi twende wakati gani, tule au tusile, tulale au tukeshe itakua hatari kubwa mno.. Uhuru uliopiganiwa na wazee wetu hauna maana tena katika mazingira haya.


Photographer of the year.📷🏆

#BreakingNews Wananchama na Viongozi wa Chadema wanaowasili katika Mahakama Kuu Masijala ndogo ya Dar es salaam, kufuatia maombi namba 28922/2025 ya Mhe Tundu Lissu akiomba kuunganishwa kwenye kesi ya msingi iliyofunguliwa na said issa Mohamed dhidi ya Bidi ya wadhamini wa Chama pamoja na Katibu Mkuu wa Chama, wamezuiwa na Jeshi la Polisi kuingia mahakamani kwa kile kinachodaiwa kuwa wanaoruhusiwa kuingia mahakamani ni wanahusika na shauri hilo ambao Katibu Mkuu Mhe. @jjmnyika, Bodi ya Wadhamani ya Chama na Mhe. @TunduALissu.

#HABARI Serikali imetoa msimamo ikisema Tanzania inayo mifumo ya kulinda haki za binadamu, ambayo ina vigezo vya kimataifa. Msimamo huo ulitolewa leo na Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Dk. Alli Possi, alipofanya mkutano wake na waandishi wa habari kwa njia ya mtandao. Balozi Possi ambaye anahudhuria kikao cha 61 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC), kinachofanyika Geneva, Uswisi, alisema mifumo ya haki za binadamu iliyopo leo ni tofauti na mwaka 1961 nchi ilipopata uhuru. Akifafanua zaidi uwepo wa mifumo hiyo, Balozi Possi alisema Katiba ya Uhuru ya Mwaka 1961 haikuwa na kipengele cha haki za binadamu, ulipofika mwaka 1988 Tanzania ilikiweka. Kwa mujibu wa Balozi Possi, tangu hapo Tanzania imekuwa ikipiga hatua katika kulinda haki za binadamu kwa watu kuzidai hadi mahakamani na kuwepo Tume ikiwemo ya Utawala Bora. "Naweza kusema ndiyo, tunayo mifumo ya kulinda haki za binadamu. Kwa mfano, Katiba yetu ya Uhuru ya mwaka 1961 haikuwa na vipengele vya haki za binadamu. Mwaka 1988 tuliviingiza. Tangu wakati huo wananchi wanazidai hadi mahakamani," alifafanua Balozi Possi. Katika kuonyesha Tanzania inazidi kuimarisha mifumo hiyo, Balozi Dk. Possi alisema Rais Dk. Samia Suluhu Hassan aliunda Tume ya Haki Jinai, ambayo ni sehemu ya kuboresha zaidi mifumo hiyo. "Ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliunda Tume ya Haki Jinai. Hii yote ni kufanya maboresho. Maboresho ni process. Hata hao walioemdelea zaidi hawajafika mwisho huwa wanafanya maboresho. "Leo hapa kwetu hali ni tofauti. Uhuru upo, tunazungumza kwa uwazi, maboresho yanaendelea na hiiyo ni process," amesisitiza Balozi Dk. Possi. #EastAfricaTV









