PT
10.4K posts

PT
@PaschalTemu
You can’t change people if you don’t change their environment 💭
🇺🇬 Katılım Ağustos 2022
3.6K Takip Edilen9.2K Takipçiler
PT retweetledi

RAIS SAMIA ATOA PUNGUZO LA KODI KWA WAFANYABIASHARA WA SOKO KUU LA KARIAKOO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. @SuluhuSamia ametoa punguzo la kodi kwa wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kuwapa nafuu na kuimarisha mazingira ya biashara.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa habari na Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA Ashraph Abdulkarim, wafanyabiashara wa vizimba wamepatiwa punguzo la kodi la asilimia 17, huku wafanyabiashara wa biashara nyingine ikiwemo maduka wakipata punguzo la kati ya asilimia 10 hadi 16.
CPA Abdulkarim ameongeza kuwa pamoja na punguzo hilo, Mhe. Rais pia ametoa msamaha wa kodi wa mwezi mmoja kwa wafanyabiashara wote wa soko hilo, kuanzia tarehe 8 Februari 2026 hadi tarehe 8 Machi 2026, tangu alipofungua rasmi Soko Kuu la Kariakoo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kariakoo, Bw. Ramadhani Kakandilo, ameishukuru Serikali kwa hatua hiyo akisema kuwa inaonesha namna inavyowajali wafanyabiashara.
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia


Indonesia

UMEME WA GRIDI YA TAIFA KUFIKA MKOA WA RUKWA MEI 2026
Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. @SuluhuSamia imejipanga kuhakikisha Mkoa wa Rukwa unaunganishwa na umeme wa gridi ya taifa ifikapo Mei 2026, kufuatia kukamilika kwa mradi wa kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 kutoka mkoani Iringa.
Wananchi wa Mkoa wa Rukwa wanatarajiwa kuanza kunufaika na umeme wa gridi ya taifa kuanzia mwezi Mei mwaka huu (2026), hatua itakayochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika mkoa huo.
Kupitia mradi huo wa kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 kutoka Iringa, Mkoa wa Rukwa utaunganishwa rasmi kwenye mfumo wa umeme wa taifa, jambo litakaloongeza uhakika wa upatikanaji wa nishati ya umeme kwa matumizi ya majumbani, biashara na viwanda.
Kwa sasa, Mkoa wa Rukwa unapata umeme kutoka nchini Zambia kupitia ushirikiano wa biashara ya umeme wa nchi za Ukanda wa Kusini mwa Afrika (SAPP), mfumo unaoruhusu nchi wanachama kuuza au kununua umeme ili kukidhi mahitaji ya wananchi wao.
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia


Indonesia

@DiraYaSamia Uwekezaji wa maana ulifanyika na sasa matunda yake yanaonekana
Indonesia

TANZANIA YASHIKA NAFASI YA NNE AFRIKA KWA UWEKEZAJI SEKTA YA MADINI
Tanzania imeendelea kuimarisha nafasi yake kama moja ya vivutio vikubwa vya uwekezaji katika sekta ya madini barani Afrika, baada ya kuorodheshwa miongoni mwa maeneo yanayoongoza kuvutia uwekezaji duniani, kwa mujibu wa ripoti ya Annual Survey of Mining Companies 2025 iliyotolewa na Taasisi ya Fraser.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Tanzania imeshika nafasi ya 34 kati ya maeneo 68 duniani yaliyotathminiwa kupitia Investment Attractiveness Index (IAI), kielezo kinachotumiwa na wawekezaji pamoja na kampuni za utafiti wa madini kuamua maeneo yenye mazingira bora ya kuwekeza katika utafiti na maendeleo ya miradi ya madini.
Katika muktadha wa bara la Afrika, Tanzania imeshika nafasi ya nne kwa mvuto wa uwekezaji katika sekta ya madini, ikitanguliwa na Botswana, Morocco na Zambia. Nafasi hiyo inaonesha ushindani mkubwa wa Tanzania katika kuvutia mitaji ya kimataifa kwa ajili ya utafiti, uchimbaji na maendeleo ya rasilimali za madini.
Ripoti hiyo pia inaonesha mwenendo mzuri wa kuongezeka kwa alama za Tanzania katika kigezo cha IAI. Mwaka 2025 Tanzania imepata alama 68.04, ikilinganishwa na alama 62.75 mwaka 2024 na 46.38 mwaka 2023. Ongezeko hilo linaashiria kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji pamoja na kuongezeka kwa imani ya wawekezaji wa kimataifa katika sekta ya madini nchini.
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia


Indonesia
PT retweetledi

ATCL YAWASAFIRISHA WATANZANIA WALIOKWAMA DUBAI KUREJEA NYUMBANI
Kufuatia machafuko yanayoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati yaliyosababisha viwanja kadhaa vya ndege kusitisha safari za ndege na hivyo kuwafanya abiria wengi kukwama, Serikali ya Tanzania imechukua hatua za haraka kwa Watanzania waliokuwa wamekwama katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai wakitafuta namna ya kurejea nyumbani.
Baada ya kupokea taarifa za uwepo wa Watanzania hao waliokwama, Serikali kupitia Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) iliratibu safari maalum ya ndege kwa ajili ya kuwarejesha nchini. Ndege kubwa ya ATCL aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, yenye uwezo wa kubeba abiria 262, ambayo iliondoka nchini tarehe 8 Machi 2026 majira ya saa tano usiku kuelekea Dubai.
Ndege hiyo iliondoka ikiwa na abiria 113 pekee, huku safari yake ya kurejea nchini ikibeba jumla ya abiria 230 chini ya uwezo wake wa abiria 262. Abiria wengine waliotarajiwa kusafiri hawakufika uwanjani.
Katika safari hiyo maalum, kipaumbele kilitolewa kwa abiria waliokuwa na tiketi za ATCL, huku nafasi zilizobaki zikitolewa pia kwa abiria wengine waliokuwa wamekwama katika uwanja wa ndege na walihitaji kurejea Tanzania.
Safari hiyo ilifanyika kwa kibali maalum baada ya ATCL kuomba ruhusa ya kufanya safari ya ziada, kwa kuwa haikuwa sehemu ya ratiba ya kawaida ya safari za shirika hilo. Hatua hiyo imewezesha Watanzania waliokuwa wamekwama kurejea nyumbani salama.
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia
Indonesia

@DiraYaSamia @SuluhuSamia Dhamira ya Rais Samia iko wazi kabisa kwenye suala la mama na mtoto
Filipino

VITUO 36 KUTEKELEZA KITITA JUMUISHI CHA HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO DAR ES SALAAM
Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. @SuluhuSamia kupitia Wizara ya Afya imeanza utekelezaji wa Kitita Jumuishi cha Huduma za Afya ya Mama na Mtoto chenye lengo la kuimarisha ubora wa huduma za afya na kupunguza vifo vya mama na watoto wachanga nchini.
Mpango huo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuongeza kasi ya kupunguza vifo vya mama na watoto wachanga kwa kuboresha huduma zinazotolewa katika vituo vya afya.
Katika utekelezaji wa mpango huo, jumla ya vituo vya afya 36 katika Mkoa wa Dar es Salaam vimechaguliwa kuwa vituo vya mfano vitakavyoonyesha utekelezaji bora wa huduma za afya ya mama na mtoto.
Aidha, mpango huo unahusisha usambazaji wa vifaa tiba katika vituo vya kutolea huduma za afya pamoja na utoaji wa mafunzo na mafunzo elekezi kazini kwa watoa huduma za afya ili kuhakikisha huduma zinazotolewa zinaendana na viwango vya kitaifa na kimataifa.
Kitita hicho kinazingatia huduma muhimu zinazohusu afya ya mama na mtoto kuanzia huduma za wajawazito kabla ya kujifungua, huduma wakati wa kujifungua, huduma za watoto wachanga pamoja na huduma za mama baada ya kujifungua, hatua inayolenga kuhakikisha mama na mtoto wanapata huduma salama na bora kuanzia kipindi cha ujauzito hadi baada ya kujifungua.
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia


Indonesia

@DiraYaSamia @SuluhuSamia Tuone mabadiliko chanya katika ukanda huo sasa
Filipino

SERIKALI YAENDELEA KUIMARISHA HUDUMA YA UMEME LINDI NA MTWARA
Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. @SuluhuSamia imewekeza Shilingi milioni 704 kwa ajili ya kufunga transfoma ya ziada katika Kituo cha Kupooza Umeme cha Mahumbika mkoani Lindi, hatua inayolenga kupunguza changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
Kupitia uwekezaji huo, uwezo wa kituo hicho umeongezeka na kufikia takribani MVA 35, jambo litakalosaidia kuimarisha upatikanaji wa umeme na kuboresha huduma kwa wananchi pamoja na shughuli za kiuchumi katika ukanda huo.
Ufungaji wa transfoma hiyo ni sehemu ya jitihada za muda mfupi za Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara.
Sambamba na hatua hizo, Serikali inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya muda mrefu ya kuimarisha miundombinu ya umeme katika ukanda huo. Miongoni mwa miradi hiyo ni mradi wa kusafirisha umeme kutoka Songea kupitia Tunduru hadi Masasi na hatimaye kufika Mahumbika, ambao unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa umeme katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
Aidha, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa kusafirisha umeme kutoka Mkuranga kupitia Somanga na Kilwa hadi Lindi, ambao utaunganishwa na miundombinu ya usambazaji wa umeme katika mikoa ya Lindi na Mtwara, hatua itakayosaidia kuongeza uthabiti wa huduma ya umeme katika maeneo hayo.
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia


Indonesia

WANANCHI WAPONGEZA UONGOZI WA RAIS SAMIA KUPITIA PROGRAMU YA JENGA KESHO ILIYO BORA (BBT)
Wananchi wamepongeza juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. @SuluhuSamia kwa kuanzisha na kuendelea kutekeleza Programu ya Jenga Kesho iliyo Bora (Building a Better Tomorrow – BBT) kupitia Wizara ya Kilimo, inayolenga kuwahamasisha vijana na wanawake kujikita katika sekta ya kilimo.
Programu hiyo inalenga kuongeza uzalishaji wa mazao na kuboresha maisha ya vijana na wanawake kwa kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika kilimo biashara. Kupitia mpango huo, vijana na wanawake wanapatiwa fursa ya kupata ujuzi wa kisasa wa kilimo pamoja na matumizi ya teknolojia ili kuongeza tija katika uzalishaji.
Aidha, programu ya BBT inalenga kuongeza ajira zenye staha nchini kwa kuwahamasisha vijana na wanawake kutumia kilimo kama chanzo kikuu cha kipato na maendeleo ya kiuchumi.
Wananchi wameishukuru Serikali kwa kuweka mazingira yanayowawezesha vijana na wanawake kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo biashara, kwa kuwapatia utaalamu wa kilimo na kuwasaidia kuongeza mavuno pamoja na kipato chao.
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TabasamuLaUtu #MaendeleoEndelevu #DiraYaSamia
Indonesia













