Rojastine Failoc
5 posts


@Sirjeff_D Mtu haniambii kitu kwamba huyu master ni mpigaj, kwasababu nina evidence 😂😂😂😂
Indonesia

@Sirjeff_D Ila bn sir Jeff, nilikuwa namkubali sana, Baada ya kutupiga 60k zetu last year za forex trading ndio bas tena
Filipino

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba leo June 15,2023 amewasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 Bungeni Jijini Dodoma ambapo moja ya mambo aliyoyasema kwenye hotuba yake ni kwamba Serikali inatarajia kuanzisha mfumo wa kidijitali wa kufuatilia na kuhakikisha kodi husika za Serikali zinalipwa kwa wakati kwa matangazo ya mitandaoni, hii itajumuisha matangazo ya biashara ambayo huwekwa na Watu maarufu (digital influencers) na biashara za mtandaoni zinazofanyika nchini.
“Kutokana na ukuaji wa teknolojia, Dunia inashuhudia mabadiliko makubwa katika tasnia ya matangazo ya kibiashara (Advertisment) ambapo sasa matangazo mengi yamekua yakifanyika kupitia mitandao (online advertisement) hasa mitandao ya kijamii kama vile Instagram, Facebook, twitter na Blogs mbalimbali”
“Kwa kushirikiana na Sekta binafsi, Serikali inatarajia kuanzisha mfumo wa kidijitali wa kufuatilia na kuhakikisha kodi husika za Serikali zinalipwa kwa wakati, hii itajumuisha matangazo ya biashara ambayo huwekwa na Watu maarufu (digital influencers) na biashara za mtandaoni zinazofanyika nchini”
#MillardAyoBUNGENI #BAJETI2023

Indonesia




