ROYAL TELEVISION PLUS

25.4K posts

ROYAL TELEVISION PLUS banner
ROYAL TELEVISION PLUS

ROYAL TELEVISION PLUS

@Royaltv_plus

Media Coverage

Dar es Salaam, Tanzania Katılım Haziran 2015
0 Takip Edilen781.5K Takipçiler
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
VIDEO: "Tukutane Kesho", ndio kauli iliyotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa Tundu Lissu wakati 'akiondoka' kwenye chumba Namba 1 cha Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam leo, Jumatatu Julai 20.2026 Lissu amekuwa Mahakamani hapo leo, kwaajili ya kusikiliza shauri la Kikatiba Na. 7300/2026 lililofunguliwa na Mawakili Kulwa William Maduhu, Nashon Nkung na Paul Kisabo dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP), Mkuu wa Gereza la Ukonga, Tundu Lissu na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Shauri hilo lililofunguliwa kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma, vikao vyake vinasikilizwa Mahakamani hapo mbele ya jopo la Majaji watatu (3) ambao ni Amir Mruma, Dkt. Angelo Rumisha na Dkt. Evaristo Longopa Ikumbukwe kuwa, katika shauri hilo waleta maombi ambao wamejitambulisha kuwa ni Mawakili wa Tundu Lissu aliyeko gerezani kutokana na kesi ya uhaini inayomkabili, wanadai kwamba wanakosa faragha ya kuwasiliana na mteja wao wakienda gerezani kumuona jambo ambalo linakiuka misingi ya kisheria na Kikatiba.
Indonesia
0
2
5
362
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema meli ya MV Liemba inatarajiwa kuanza kutoa huduma mapema mwezi Agosti mwaka huu baada ya ukarabati wake kukamilika ambapo kwa sasa umefikia asilimia 99, hatua inayotarajiwa kuimarisha usafiri na usafirishaji katika Ziwa Tanganyika. Profesa Mbarawa ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Julai 20, 2026 mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa meli nne za mizigo katika Bandari ya Kigoma. Amesema MV Liemba ilisimama kutoa huduma mwaka 2018, huku kazi ya kuifufua ikianza mwaka 2023 na sasa meli hiyo ipo kwenye cherezo kwa hatua za mwisho za ukarabati. Ameeleza kuwa matarajio ni kuitoa ifikapo mwisho wa mwezi Julai kabla ya kuanza safari zake mapema Agosti. Akizungumzia mradi wa ujenzi wa karakana ya kujengea meli ya Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO), Profesa Mbarawa amesema mkandarasi tayari amepatikana na amelipwa malipo ya awali ya dola za Marekani milioni 8.8, huku kiasi kingine cha dola milioni 8.8 kikisubiri kutolewa ili kuharakisha utekelezaji wa mradi. Amefafanua kuwa kazi imeanza lakini inaendelea kwa kasi ndogo kutokana na mkandarasi kutokupokea malipo yote ya awali, huku Wizara ya Uchukuzi ikiendelea kushirikiana na Wizara ya Fedha kuhakikisha fedha zilizobaki zinapatikana kwa wakati. Aidha, amesema Serikali inaendelea na maandalizi ya miradi miwili mikubwa ya usafiri majini inayohusisha ujenzi wa meli mpya ya abiria kwa ajili ya Kigoma na meli ya mizigo yenye uwezo wa kubeba tani 3,000 kwa safari kati ya Kigoma na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Amesema wakandarasi wa miradi hiyo tayari wamepatikana, lakini utekelezaji unasubiri upatikanaji wa malipo ya awali.
Indonesia
0
0
2
683
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Mhandisi Machibya Shiwa amesema ujenzi wa kipande cha Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Tabora hadi Kigoma utagharimu dola za Marekani bilioni 2.7, sawa na takribani Sh. trilioni 6.3, na unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 48. Mhandisi Shiwa ametoa taarifa hiyo leo Jumatatu Julai 20, 2026 mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo. Amesema mradi unahusisha ujenzi wa kilometa 411 za njia kuu za reli na kilometa 95 za njia za kupishana. Utekelezaji wake umegawanywa katika sehemu mbalimbali ili kuongeza kasi ya ujenzi kwa kutumia timu nyingi za wakandarasi. Ameeleza kuwa mkandarasi wa mradi ni kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) huku Mhandisi Mshauri akiwa kampuni ya Dar Al-Handasah. Mradi pia utajumuisha madaraja makubwa 27, madaraja madogo 75 na box culverts 475. Kwa mujibu wa Mhandisi Shiwa, reli hiyo itajengwa kwa viwango sawa na vipande vingine vya SGR kutoka Dar es Salaam, ili kuhakikisha kunakuwa na mfumo mmoja wa reli ya kisasa hadi Kigoma. "Treni za abiria zitakuwa na uwezo wa kukimbia kwa kasi ya kilometa 160 kwa saa, huku treni za mizigo zikikimbia kwa kasi ya kilometa 120 kwa saa." alisema Mhandisi Machibya Ameongeza kuwa kwa kuzingatia usalama wa wananchi, kutajengwa maeneo maalumu ya kuvukia reli katika njia yote kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma. Pia kutakuwa na stesheni za Urambo, Uvinza na Kigoma, ambapo Stesheni ya Kigoma itakuwa ya nne kwa ukubwa nchini baada ya Dodoma, Dar es Salaam na Mwanza. Aidha, amesema ujenzi wa daraja la Mto Malagarasi umefikia hatua nzuri, ambapo nguzo zake tayari zimekamilika, hatua itakayochochea kasi ya utekelezaji wa mradi mzima.
Indonesia
0
0
3
1K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza uwekezaji mkubwa katika sekta ya uchukuzi unaolenga kuifanya Kigoma kuwa kitovu cha usafirishaji na biashara kinachounganisha Tanzania na nchi za Afrika Mashariki na Kati. Profesa Mbarawa amesema hayo leo Jumatatu Julai 20, 2026 katika hafla iliyohudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa uzinduzi wa meli nne za mizigo, uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa gati la abiria na mizigo Bandari ya Kigoma pamoja na uzinduzi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Tabora–Kigoma. Amesema chini ya uongozi wa Rais Samia, Serikali imewekeza kwa kiwango kikubwa katika reli ya kisasa, bandari, viwanja vya ndege na usafiri wa majini kwa lengo la kuunganisha mikoa yote ya Tanzania pamoja na nchi jirani kupitia mfumo jumuishi wa uchukuzi. Kwa mujibu wa Profesa Mbarawa, meli nne mpya za mizigo zitaongeza usalama wa usafirishaji katika Ziwa Tanganyika, kupunguza gharama za usafirishaji wa mizigo, kukuza biashara kati ya Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Burundi, pamoja na kufungua fursa mpya za ajira na uwekezaji. Aidha, amesema maboresho yanayoendelea Bandari ya Kigoma pamoja na ujenzi wa Reli ya Kisasa kutoka Tabora hadi Kigoma yataongeza ufanisi wa usafirishaji wa abiria na mizigo, huku yakiiunganisha Bandari ya Dar es Salaam na masoko ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Profesa Mbarawa pia amesema Serikali inaendelea na maboresho ya uwanja wa ndege wa Kigoma kwa gharama ya Sh. bilioni 51.4, yanayojumuisha ujenzi wa jengo jipya la abiria, mnara wa kuongozea ndege, njia za ndege, taa za kuongozea ndege na miundombinu mingine muhimu. Ameongeza kuwa miradi hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kujenga mfumo wa uchukuzi unaounganisha reli, bandari na usafiri wa anga ili kuharakisha maendeleo ya uchumi wa Taifa.
Indonesia
0
0
1
447
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Tabora hadi Kigoma ni hatua muhimu katika kuimarisha usafiri na usafirishaji nchini pamoja na kuunganisha shughuli za kiuchumi za Mkoa wa Kigoma na masoko ya ndani na nje ya nchi. Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu Julai 20, 2026 mkoani Kigoma wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo na uzinduzi wa meli nne za mizigo katika Bandari ya Kigoma, akieleza kuwa Serikali imeanza kutekeleza ahadi ya kuifanya Kigoma isiwe mwisho wa reli bali kuwa sehemu ya kuunganisha fursa za biashara na uwekezaji. Amesema mradi wa SGR Tabora hadi Kigoma wenye urefu wa takribani kilometa 506 unagharimu dola za Marekani bilioni 2.74, sawa na Shilingi trilioni 7.4, na utakapokamilika utaunganisha Kigoma na mikoa ya Tabora, Dodoma, Morogoro hadi Dar es Salaam pamoja na mtandao wa reli unaoelekea Mwanza. Vilevile amesema, kukamilika kwa reli hiyo kutawezesha mizigo kutoka Bandari ya Dar es Salaam kufika Kigoma kwa haraka na kwa uhakika, huku wafanyabiashara na wajasiriamali wakinufaika kupitia kupungua kwa muda na gharama za usafirishaji. Ameeleza kuwa mnyororo wa shughuli zitakazochochewa na mradi huo utazalisha fursa za ajira kwa vijana wa Kigoma katika maeneo mbalimbali ikiwemo usafirishaji, maghala, huduma za hoteli, matengenezo ya mitambo na shughuli nyingine zitakazotokana na uwepo wa reli hiyo. Rais Samia amesema Serikali inaendelea kujenga miundombinu ya usafiri na usafirishaji kwa lengo la kuifungua Tanzania kibiashara na kiuwekezaji, huku akisisitiza kuwa kila reli, bandari, barabara na kiwanja cha ndege kinachojengwa kinaunganisha maeneo ya ndani na fursa za masoko. Amesisitiza kuwa SGR Tabora–Kigoma ni sehemu ya jitihada za kuimarisha nafasi ya Tanzania katika usafirishaji wa kikanda, huku Kigoma ikitarajiwa kunufaika kutokana na nafasi yake ya kimkakati inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani.
Indonesia
1
0
2
1K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema uzinduzi wa meli nne za mizigo pamoja na maboresho ya miundombinu ya bandari ni sehemu ya jitihada za Serikali kuimarisha usafirishaji wa majini, kukuza biashara na kufungua fursa za uwekezaji katika Mkoa wa Kigoma na maeneo ya jirani. Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu Julai 20, 2026 mkoani Kigoma wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi ujenzi wa reli ya kisasa kipande cha Tabora hadi Kigoma na uzinduzi wa meli nne za mizigo katika Bandari ya Kigoma zilizojengwa kupitia uwekezaji wa sekta binafsi wa kampuni ya Golden Logistic Company Ltd, akieleza kuwa meli hizo zitakuwa nyenzo muhimu katika kusafirisha shehena za mizigo kutoka Tanzania kwenda nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi na Zambia. Amesema uwepo wa meli hizo pamoja na ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) Tabora–Kigoma utakapokamilika utaongeza uwezo wa Kigoma kutumia nafasi yake ya kimkakati kama lango la biashara na uwekezaji linaloiunganisha Tanzania na nchi jirani. “Kigoma ina nafasi nzuri kijiografia na kimkakati. Meli za mizigo tulizozindua leo pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa vitakuwa nyenzo muhimu zitakazotuwezesha kufikia maono na matamanio yetu,” amesema Rais Samia. Aidha, Rais Samia amesema Serikali inaendelea kuboresha bandari mbalimbali nchini kwa lengo la kuongeza ufanisi wa huduma za usafirishaji na kurahisisha bidhaa kufikia masoko ya ndani na nje ya nchi. Amesema uwekezaji huo unatarajiwa kuvutia wawekezaji kuanzisha vituo vikubwa vya lojistiki na usafirishaji Kigoma, huku ukifungua fursa za ajira na kuongeza shughuli za kiuchumi katika mnyororo wa usafirishaji. Akizungumzia meli kongwe ya MV Liemba, Rais Samia amesema ukarabati wake umefikia asilimia 99 na ameitaka Wizara ya Uchukuzi pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kuhakikisha inakamilishwa kwa viwango vya juu ili iendelee kutoa huduma kwa miaka mingi ijayo. Pia ameitaka Wizara ya Uchukuzi kukamilisha ujenzi wa karakana ya kujengea meli Kigoma kwa kushirikiana na wawekezaji, ili iweze kutumika kwa pamoja katika kujenga na kuhudumia meli. Rais Samia amesisitiza umuhimu wa wananchi kulinda miundombinu ya usafiri na usafirishaji ikiwemo reli, barabara na bandari, akieleza kuwa ni mali ya Taifa yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Indonesia
0
0
2
722
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema amani na usalama ni msingi mkuu wa maendeleo ya Taifa, akiwataka wananchi kuendelea kulinda tunu hizo ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na mazingira bora ya ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii. Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu Julai 20, 2026 mkoani Kigoma wakati akizungumza mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Tabora hadi Kigoma na uzinduzi wa meli nne za mizigo katika Bandari ya Kigoma. Amesema Serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo miundombinu ya usafiri na usafirishaji, lakini mafanikio ya miradi hiyo yanategemea uwepo wa amani na usalama nchini. “Swala la amani na usalama wa nchi yetu ni kipaumbele cha kwanza na hatupaswi kulipuuza hata kidogo. Tukivuruga amani na usalama wa nchi yetu, maendeleo hayatashamiri na hayatakuwa na maana,” amesema Rais Samia. Amewataka wananchi wa Kigoma na Watanzania kwa ujumla kuwa na utamaduni wa kuweka usalama mbele, akisisitiza kuwa maendeleo yanahitaji mazingira yenye utulivu na mshikamano. Rais Samia pia amewataka wananchi kutokubali kushawishiwa au kutumiwa na watu wenye nia ya kuvuruga amani ya nchi, akieleza kuwa kulinda usalama ni jukumu la kila Mtanzania. “Amani na usalama ni maendeleo, na maendeleo ni amani na usalama. Sote tuwe macho na tuepuke kuwa wasaliti na maadui wa nchi yetu,” amesema Rais Samia. Ameongeza kuwa ulinzi wa amani na usalama utaendelea kuiwezesha Tanzania kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, kuvutia uwekezaji na kukuza uchumi kwa manufaa ya wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.
Indonesia
1
0
5
1.6K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
VIDEO: Shauri la Kikatiba lililofunguliwa na Mawakili Kulwa William Maduhu, Nashon Nkung na Paul Kisabo, dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini (CGP), Mkuu wa Gereza Ukonga, Tundu Lissu na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) linasikilizwa leo, Jumatatu Julai 20.2026, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma Kikao cha shauri hilo la Kikatiba kinaketi kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam mbele ya jopo la Majaji watatu (3) ambao ni Amir Mruma, Dkt. Angelo Rumisha na Dkt. Evaristo Longopa Kupitia shauri hilo, waleta maombi ambao wamejitambulisha kuwa ni Mawakili wa Tundu Lissu ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa aliyeko gerezani kutokana na kesi ya uhaini inayomkabili, wanadai kwamba wanakosa faragha ya kuwasiliana na mteja wao wakienda Mahakamani jambo ambalo linakiuka misingi ya kisheria na Kikatiba.
Filipino
0
21
111
9.7K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Bei ya mafuta ghafi aina ya Brent imepanda na kuvuka dola 90 kwa pipa kutoka kiwango cha takribani dola 70 ilichokuwa imefikia baada ya makubaliano ya muda ya kusitisha mapigano kati ya Iran na Marekani, huku matumaini ya dunia ya kuona bei za mafuta zikishuka yakizidi kuyeyuka baada ya Iran kutangaza kuzilipua meli nyingine mbili za mafuta zilizokuwa zikijaribu kuvuka Mlango wa Hormuz ambapo tukio hilo limezidisha hofu ya kuvurugika kwa usafirishaji wa mafuta kupitia njia hiyo muhimu ya kimataifa na kuongeza presha katika soko la nishati duniani. Kupanda kwa bei ya mafuta kunatajwa kuwa pigo jipya kwa uchumi wa dunia kutokana na mafuta kuwa mhimili wa shughuli nyingi za kiuchumi huku wachambuzi wakisema ongezeko hilo linasababisha kuongeza gharama za usafiri wa anga, baharini na barabarani, uzalishaji viwandani, kilimo, ujenzi, uchimbaji madini na usafirishaji wa bidhaa, hali inayoweza kuchochea mfumuko wa bei, kuongeza gharama za maisha na kupunguza kasi ya ukuaji wa uchumi katika mataifa mengi yanayotegemea uagizaji wa mafuta. Kwa mujibu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran (IRGC), meli hizo mbili zililipuliwa katika njia ya kusini ya Mlango wa Hormuz, huku Iran ikidai zilikuwa zimekiuka taratibu zake za usafiri. Mlango wa Hormuz hupitisha takribani asilimia 20 ya mafuta yote yanayosafirishwa duniani kwa njia ya bahari, hivyo tukio lolote la kiusalama katika eneo hilo huathiri moja kwa moja upatikanaji wa mafuta na mwenendo wa bei katika soko la dunia. Hali inayoongeza taharuki kwa kampuni za usafirishaji wa mafuta, kampuni za bima na masoko ya fedha. Wataalamu wa sekta ya nishati wanaonya kuwa endapo mivutano kati ya Iran na Marekani itaendelea, upatikanaji wa mafuta unaweza kupungua zaidi na bei ya Brent kuendelea kupanda katika siku zijazo. Kwa nchi zinazoagiza mafuta kutoka nje, hali hiyo inaweza kuongeza matumizi ya fedha za kigeni, kupandisha gharama za uzalishaji na usafirishaji, kuongeza bei za bidhaa na huduma pamoja na kuathiri juhudi za mataifa mengi kudhibiti mfumuko wa bei na kuimarisha uchumi.
ROYAL TELEVISION PLUS tweet media
Indonesia
0
0
2
1.1K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi amesema hatokua tayari kuona kundi la watu wachache wenye maslahi binafsi wanachezea amani iliyopo kwa kujificha katika kichaka cha Haki za binadamu na Demokrasia huku akiwahakikishia jamii ya watanzania kuendelea kuwepo kwa Hali ya Utulivu nchini huku akisema yupo tayari kwenda mahakamani hata usiku ili jamii iweze kupata suluhu ya Wapotoshaji wanaotumika kuchochea chuki na kuhatarisha amani ya Nchi kwa maslahi yao binafsi na kundi. Ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti akizungumza Makundi ya Walinzi wa amani katika jamii, Polisi jamii, Wazee, Sungusungu, Wenyeviti wa Mitaa,Mabalozi na Wenyeviti wa Vitongoji Vitongoji,Shinyanga Mjini. “Wanajua wakiichafua Tanzania yetu amani ikapotea tutapoteza mvuto kwa watalii,Nchi iwekewe vikwazo, Miradi mikubwa ya maendeleo itasiama,kubomoa mahusiano ya kidiplomasia, kutisha wawekezaji, tutapoteza mapato ya bandari ambapo timu hiyo inayosema inanipeleka mahakamani ndiyo hiyo hiyo ilikua inapinga Mkataba wa Uwekezaji wa bandari lakini sasa hivi bandari inaingiza fedha nyingi sana na tumeanza kwenda mbele ikiwa ni hatua za Taifa kuanza kujitegemea,wameshindwa kuwapeleka mahakamani ambao wanachochea kuangamiza Taifa letu kwa kuchoma moto,zichomwe moto shule,vituo vya mafuta,ofisi za serikali,mali na biashara za watu binafsi zichomwemoto,wavamie vituo vya polisi. Kama wanauchungu kweli na haki za Binadamu ni lini na wapi mliwasikia wanakemea vitendo hivyo hatarishi kwa uhai wa watu na Taifa?” amesema Waziri Katambi “Wanachochea fujo lakini watoto wao,wake zao wako nje ya nchi, wanatembea na Pasport za kusafiria mfukoni,leo hii yakitokea machafuko wazee wangu mtaenda wapi? watoto, wanawake na wenyeulemavu si ndio wahanga mmewafikiria? Nchi yetu ni Tanzania hamna nchi nyingine,kuna nchi za Burundi,Rwanda na Kongo yalitokea machafuko tumehifadhi Wakimbizi kwa miaka mingi kutoka nchi hizo je wanataka na sisi tukawe wakimbizi? Mimi Katambi hilo siwezi kukubali litokee tumepewa dhamana ya kulinda amani ya nchi hii kwa viapo tutailinda kwa gharama zote.” aliongeza Waziri Katambi Amesema bado hajapokea wito wa kuitwa mahakamani lakini yuko tayari kwenda huko hata usiku wa manane akipokea wito huku akisisitiza mahakama ndio chombo pekee Huru na chenye mamlaka ya kusema Katiba imevunjwa na sio jukumu la mtu au taasisi fulani kusema Katiba imevunjwa hawana mamlaka wala usahihi huo.
Indonesia
3
1
7
2.3K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
VIDEO: "Tukutane Mahakamani hata kesho", ndivyo alivyojibu Habibu Mchange Mkurugenzi wa Jamvi media Group akigoma kuomba radhi kutokana na tuhuma alizozitoa kwa Mfanyabiashara Nilesh Suchack kuwa anawatumia wanasiasa wa upinzani John Heche wa CHADEMA na Luhaga Mpina wa ACT Wazalendo kwa ajili ya kufanya upotoshaji katika uagizaji wa mafuta nchini Mchange amesema ataitumia kesi hiyo kuufumbua macho umma wa watanzania juu ya michezo michafu inayofanywa na wafanyabiashara aina ya Nilesh akisema kuwa siku 14 alizopewa ni nyingi sana anamtaka aende mahakamani hata kesho. Ikumbukwe kuwa siku kadhaa zilizopita Nilesh alimuandikia barua Mchange ya kumtaka aombe radhi na kufuta kauli zake ndani ya siku 14 la sivyo atamburuza mahakamani na kumdai fidia ya Tsh Bilioni 12
Indonesia
4
8
63
13.1K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
VIDEO: Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Sheikh Abbas Ramadhan Abbas ametoa rai kwa watu wote 'kuacha' kutamani na kupigania nafasi za uongozi kwani ni miongoni mwa mambo hatari, yanayokufanya uache kwa asilimia kubwa mambo yako binafsi na kutumikia watu Sheikh Abbas ametoa rai hiyo, ikiwa ni sehemu ya nasaha zake za kwanza kabisa tangu aingie Ofisini kutumikia nafasi hiyo, baada ya kukabidhiwa rasmi Ofisi kutoka kwa mtangulizi wake Sheikh Walid Alhad Kawambwa.
Indonesia
3
3
63
7.7K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Royal TV Plus inakusogezea kuona kilichoandikwa kwenye kurasa za mbele za baadhi ya magazeti ya Tanzania yaliyochapisha habari za Siasa, Jamii, Uchumi, Michezo, Sanaa na Burudani leo, Jumapili Julai 19.2026
ROYAL TELEVISION PLUS tweet mediaROYAL TELEVISION PLUS tweet mediaROYAL TELEVISION PLUS tweet mediaROYAL TELEVISION PLUS tweet media
Indonesia
0
0
10
1.6K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
VIDEO: Kutoka Mkoani Tabora, tunakusogezea taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoani humo ACP Twaha Juma Lulengelule kuhusiana na Baba anayedaiwa KUMUUA mtoto wake wa kumzaa, ambapo inaelezwa kuwa baada ya kutekeleza UKATILI huo aliuchukua mwili wa mtoto huyo na kuuficha vichakani ACP Twaha Juma Lulengelule amemtaja mtuhumiwa ambaye kwa sasa yuko kwenye mikono ya Jeshi la Polisi kuwa ni Seleman Charles, Mkazi wa Kwihala.
Indonesia
2
0
12
3.8K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Misri zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya usafirishaji kwa kuunganisha bandari za nchi hizo, hatua inayotarajiwa kurahisisha biashara, kuongeza uwekezaji na kufungua masoko mapya barani Afrika na eneo la Ghuba. Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam leo Julai 18, 2026 mara baada ya kumpokea Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Abdel Fattah El-Sisi, Rais Samia amesema makubaliano hayo yanahusisha maendeleo ya Bandari ya Dar es Salaam pamoja na ujenzi wa eneo maalumu katika Bandari ya Bagamoyo litakalounganishwa na reli hadi Kwala kwa ajili ya kuhifadhi bidhaa na makontena ya Misri. Amesema nchi hizo pia zimehimiza kuendelea kwa majadiliano ya kuunganisha Bandari za Dar es Salaam, Bagamoyo, Safaga na bandari nyingine za Misri ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa, kuongeza ushindani wa biashara na kufungua fursa kwa bidhaa za Tanzania kuingia katika masoko ya Ghuba huku bidhaa za Misri zikifikia nchi za Kusini mwa Afrika. Rais Samia pia amesema ushirikiano huo unaenda sambamba na jitihada za kukuza biashara na uwekezaji, akibainisha kuwa Rais El-Sisi ameambatana na wafanyabiashara wakubwa 35 wanaoshiriki Jukwaa la Biashara Tanzania–Misri, hatua inayotarajiwa kuongeza biashara kati ya mataifa hayo mawili. Aidha, amesema Shirika la Ndege la Misri (Egypt Air) tayari inaendesha safari tatu kwa wiki kati ya Misri na Tanzania, huku akiitaka Air Tanzania kujipanga kuanzisha safari za moja kwa moja kuelekea Misri ili kuimarisha usafiri wa abiria, biashara na utalii. Rais Samia amesisitiza kuwa ushirikiano huo utaifanya Tanzania kuwa lango muhimu la biashara kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini, huku ukiimarisha uhusiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.
Indonesia
0
0
10
1.7K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Misri zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta za kilimo na mifugo, huku Misri ikionesha nia ya kuwekeza katika Ranchi ya Ruvu ili kuongeza uzalishaji na kuimarisha usalama wa chakula. Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam leo Julai 18, 2026 mara baada ya kumpokea Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Abdel Fattah El-Sisi, Rais Samia amesema viongozi hao walijadili namna ya kutumia teknolojia za kisasa za umwagiliaji na ufugaji ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao na mifugo. Amesema Afrika inaendelea kutumia fedha nyingi kuagiza chakula kutoka nje, hivyo Tanzania na Misri zimeona umuhimu wa kuimarisha uzalishaji wa ndani kwa kutumia rasilimali zilizopo. Amebainisha kuwa Tanzania ina takribani hekta milioni 29 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji, jambo linalotoa fursa kubwa kwa uwekezaji. Rais Samia amesema, Misri imeonesha utayari wa kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza Ranchi ya Ruvu, ambayo kwa sasa haitumiki ipasavyo, ili iwe kitovu cha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya mifugo. Aidha, amesema amewakaribisha wawekezaji wa Misri kushirikiana na taasisi za Serikali zenye maeneo makubwa ya uzalishaji ikiwemo Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Magereza na Shirika la Taifa la Ranchi (NARCO), pamoja na miradi ya kilimo Zanzibar. Rais Samia ameeleza kuwa, ushirikiano huo unalenga kuongeza uzalishaji wa chakula, kuvutia uwekezaji, kuzalisha ajira na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uzalishaji wa mazao na mifugo kwa soko la Afrika na maeneo mengine.
Indonesia
0
0
1
1.2K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Hosamu Hamza Juma maarufu kama Maopena kwa tuhuma za kuwaua baba yake mzazi, Hamza Juma Omari (48) na baba yake mdogo, Ally Juma Omari (37), kisha kufukia miili yao katika shimo ndani ya eneo la nyumba yao, Mtaa wa Sindano, Mwananyamala. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Julai 18, 2026 na Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Faustine Mafwele, mtuhumiwa alikamatwa Julai 17, 2026 majira ya saa 9:00 alasiri baada ya kuonekana akiwa na kisu kilichokuwa na damu pamoja na nguo zake zilizokuwa zimechafuliwa damu. Taarifa hiyo inaeleza kuwa wakati mahojiano na mtuhumiwa yalipokuwa yakiendelea, majira ya saa 4:00 usiku Polisi wa Kituo cha Oysterbay walipokea taarifa kutoka kwa wananchi kuwa kulikuwa na damu nyingi katika nyumba moja iliyopo Mtaa wa Sindano, Mwananyamala, huku watu watatu waliokuwa wakiishi katika nyumba hiyo wakionekana kutoweka. Baada ya uchunguzi wa awali uliohusisha wataalamu wa uchunguzi wa kisayansi, miili ya watu wawili iligunduliwa ikiwa imefukiwa kwenye shimo ndani ya eneo la nyumba hiyo. Miili hiyo ilithibitika kuwa ni ya Hamza Juma Omari na Ally Juma Omari. Polisi wamesema uchunguzi wa kina wa awali unaonyesha kuwa mtuhumiwa ndiye anayehusishwa na mauaji hayo. Hata hivyo, chanzo halisi au sababu iliyomfanya kutekeleza tukio hilo bado haijabainika na inaendelea kufanyiwa uchunguzi. Jeshi la Polisi limewashukuru wananchi pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kwa ushirikiano walioutoa, likisema taarifa walizotoa zimekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha uchunguzi wa tukio hilo. Aidha, Polisi wamewahakikishia wananchi kuwa uchunguzi unaendelea na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa mara utakapokamilika.
ROYAL TELEVISION PLUS tweet media
Indonesia
2
0
8
6.1K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
Mwenyekiti wa State Oil (T) Ltd Nilesh Suchak kupitia kampuni ya Uwakili ya Prime Attorneys amemtumia barua Mkurugenzi Mtendaji wa Jamvi la Habari Habib Mchange akimtaka kuomba radhi na kufuta mara moja kauli za kashfa zilizochapishwa na kurushwa kupitia vyombo mbalimbali vya Habari na Mitandao ya Kijamii Barua hiyo iliyotumwa Julai 14.2026 inaeleza kuwa machapisho hayo yamechafua jina na hadhi ya mteja wao Nilesh Suchak kwa kumuhusisha na vitendo vya udanganyifu Kupitia barua hiyo, inaelezwa kuwa maudhui yaliyochapishwa kwenye vyombo mbalimbali vya Habari na Mitandao ya Kijamii Julai 13 na 14.2026 pamoja na siku zilizofuata zimetoa taswira inayomuonyesha Nilesh Suchak na kampuni yake kwa ujumla kuwa wanajihusisha na vitendo vya kifisadi na udanganyifu, pia imeelezwa kuwa tuhuma hizo zimechapishwa kwa lengo la kuharibu sifa na heshima ya mteja wao mbele ya umma Kutokana na barua hiyo, Prime Attorneys imemtaka Mchange kusitisha mara moja kuchapisha taarifa za kashfa badala yake anapaswa kuchapisha taarifa ya kuomba radhi na marekebisho ya taarifa hizo kwa namna ileile iliyochapishwa awali, sambamba na kulipa fidia ya shilingi za Kitanzania Bilioni 12 kutokana na kuharibu sifa na hadhi ya mteja wao Aidha, Mchange ameonywa kwamba endapo hatatekeleza maelekezo hayo haraka iwezekanavyo ndani ya siku 14 tangu alipopokea barua hiyo, mteja wao atachukua hatua nyingine zaidi za kisheria pasipo kutoa taarifa nyingine ambapo atalazimika kudai fidia na gharama nyingine zaidi ya alizopendekeza awali.
ROYAL TELEVISION PLUS tweet media
Indonesia
5
8
46
8.9K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
VIDEO: Sheikh Abbas Ramadhan Abbas, ambaye kwa sasa ni Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema amepokea kwa HUZUNI uteuzi wa Baraza la Ulamaa la BAKWATA, lililomteua kushika nafasi hiyo iliyokuwa inashikiliwa kabla yake na Sheikh Walid Alhad Kawambwa Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi iliyofanyika kwenye Ofisi za BAKWATA Mkoa wa Dar es Salaam zilizopo Kariakoo, DSM leo, Jumamosi Julai 18.2026, Sheikh Abbas Ramadhan Abbas amesema HUZUNI huo unatokana na ukweli kwamba viongozi wa Dini wana jukumu la 'ulezi' wa roho za watu na kumtumikia Allah S.W ambaye jicho lake linaangalia katika uadilifu wa kuitumikia Dini Kuhusu mtangulizi wake Sheikh Walid Alhad Kawambwa, Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Sheikh Abbas Ramadhan Abbas amesema huyo ni Kaka yake, lakini pia ni 'Mwalimu' wake hivyo anaamini bado katika kutimikia nafasi hiyo anahitaji zaidi ushirikiano wake kwa kumkosoa, kumpa ushauri nk.
Indonesia
3
0
81
18.2K
ROYAL TELEVISION PLUS
ROYAL TELEVISION PLUS@Royaltv_plus·
VIDEO: Kutoka Mwananyamala, Jijini Dar es Salaam tunakusogezea taarifa alizochapisha kwenye mtandao wake wa Instagram Dada wa Hekaheka kutoka Clouds Media Geah Habib, ambaye kupitia video hii anasikika akieleza kisa kinachodaiwa kuwa Mtoto amewaua Baba yake Mzazi na Baba yake mdogo kisha kuwafukia Inadaiwa kuwa tayari Polisi wamefika kwenye eneo hilo, na taratibu nyingine zinaendelea, msikilize.
Filipino
1
1
10
2.8K