Kamcheer retweetledi

Breaking News:
Wanaharakati wa mitandaoni Innocent Paul Chuwa (Kiduku) na Farida Mikoroti muda mfupi uliopita leo, Jumatano Oktoba 01.2025 wameachiwa kwa dhamana kutoka Kituo Kikuu cha Polisi cha Kati (Central Police) Dar es Salaam walipokuwa wanashikiliwa takribani juma moja tangu walipokamatwa, wakituhumiwa kutenda makosa ya mtandao
Licha ya kwamba wamepatiwa dhamana, lakini sasa watalazimika kuripoti kituoni hapo kila siku asubuhi, ikielezwa kuwa muda wowote wanaweza kufikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili,
Mawakili Kulwa William Maduhu kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC @humanrightstz), Paul Kisabo kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC @THRDCOALITION) na Fredrick Msaki kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS @TanganyikaLaw) ndio waliokuwa mstari wa mbele kufuatilia dhamana hiyo kwa muda wote huo.
Jambo TV itakuletea taarifa zaidi kuhusiana na hilo.

Filipino




























