Macocha Tembele

758 posts

Macocha Tembele banner
Macocha Tembele

Macocha Tembele

@mactembele

Ambassador of the United Republic of Tanzania to Indonesia and High Commissioner to Singapore

Jakarta, Indonesia Katılım Ocak 2011
713 Takip Edilen4.5K Takipçiler
Macocha Tembele
Macocha Tembele@mactembele·
Ijumaa iliyopita, pamoja na mabalozi wenzangu wa nchi za Afrika waliopo Jakarta tulisherehekea Siku ya Afrika (Africa Day 2026) ambayo huadhimishwa Mei 25 ya kila mwaka. Katika hotuba yangu kama Amidi wa Mabalozi wa Afrika pamoja na kukumbushia kauli mbiu ya Umoja wa Afrika kwa mwaka huu kuhusu upatikanaji endelevu wa maji ili kufanikisha malengo ya Ajenda ya 2063. Nilisisitiza pia umuhimu wa kuchagiza zaidi ushirikiano wa kiuchumi baina ya Afrika na Asia katika kutafuta uhuru wa kiuchumi kama ambavyo tulishirikiana baada ya Mkutano wa Bandung wa 1955 kuamsha fikra na hamasa za kupambania uhuru wa kisiasa kwa nchi zetu. #africaday2026
Macocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet media
Indonesia
0
2
7
992
Macocha Tembele
Macocha Tembele@mactembele·
I have deepest admiration and pride in all you have accomplished as you conclude your distinguished service at the UN. You discharged your duties with extraordinary grace, wisdom, and integrity, leaving a remarkable legacy. Your leadership at the UN has brought honor not only to yourself, but to all of us privileged to call you a compatriot. May your next chapter be just as impactful and fulfilling.
English
0
0
2
86
Joyce Msuya
Joyce Msuya@JoyceMsuya·
After 4 years in this role, I leave with one enduring truth: humanitarian action begins with humanity. Behind every meeting, mission, statement and statistic is a whole village of people making the work possible. To everyone who stood behind these stats: thank you.✨
Joyce Msuya tweet media
English
6
15
86
3.7K
Macocha Tembele
Macocha Tembele@mactembele·
Leo nilitembelea mashamba ya kampuni ya PT.Socfindo nje kidogo ya mji wa Medan kushuhudia usambazaji wa mbegu mpya za chikichi zenye vinasaba vya kijenetiki kutoka Tanzania. Mbegu hizi ambazo ni bora zaidi kwa uzalishaji wa mafuta na himilivu zaidi kwa magonjwa, ni zao la utafiti wa pamoja wa Wizara ya Kilimo ya hapa, Shirikisho la wafanyabiashara wa Chikichi Indonesia (@GAPKI_ID) na Taasisi yetu ya Utafiti wa Kilimo (TARI). Indonesia ina mshamba ya chikichi yenye ukubwa wa hekta milioni 16, na ndio nchi mzalishaji mkubwa zaidi wa mafuta ya chikichi duniani hivyo tunajivunia ushirikiano huu kwani utasaidia sana juhudi za serikali yetu kuinua zao la chikichi nchini ili sekta hii iweze kusaidia kupunguza nakisi ya uzalishaji wa mafuta ya kula ambayo yanatugharimu fedha nyingi za kigeni kuagiza nje.
Macocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet media
Indonesia
0
4
8
1K
Macocha Tembele retweetledi
The Chanzo
The Chanzo@TheChanzo·
Aprili 25, 1964: Mwalimu Nyerere akihutubia Bunge la Tanganyika juu ya mkataba wa muungano. Leo Aprili 26, 2026, Tanganyika na Zanzibar zinaadhimisha miaka 62 ya muungano uliounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni nini maoni yako kuhusu muungano?
Filipino
4
36
92
4.3K
Macocha Tembele retweetledi
Tanzania Embassy | Jakarta
Tanzania Embassy | Jakarta@UbaloziJakarta·
Balozi Macocha Tembele amekutana na ujumbe wa DART baada ya kuhitimisha ziara ya mafunzo nchini Indonesia na kusisitiza matumizi ya maarifa na uzoefu walioupata katika kuboresha usafiri wa umma na miundombinu nchini Tanzania. Ujumbe umeushukuru Ubalozi kwa uratibu wa ziara hiyo.
Tanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet media
Indonesia
0
1
2
102
Macocha Tembele
Macocha Tembele@mactembele·
Nilikuwa na wakati mzuri sana leo wa kunururisha fikra nilipomtembelea ofisini kwake Prof. Kishore Mahbubani, Mwanadiplomasia Mstaafu na nguli wa Singapore ambae pia ni mwanataaluma. Tumebadilishana mawazo juu ya dhana mbalimbali za maendeleo na kugusia pia nafasi ya Afrika katika kujitafutia maendeleo yake hususan kwa kufuata nyayo za baadhi ya nchi za Asia zilizofanikiwa kama Singapore ukizingatia kuwa tulikuwa ngazi sawa kimaendeleo kwenye miaka ya 70. Tumekubaliana kuanza mchakato wa kuwawezesha wanataaluma wa maeneo yetu kufanya tafiti za pamoja na kubadilishana ujuzi. Imekuwa bahati pia amenisainia tawasifu yake (Memoir) aliyokamilisha kuiandika hivi karibuni na akaiita “Living the Asian Century”.
Macocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet media
Indonesia
0
2
4
522
Macocha Tembele retweetledi
Abertus Paschal 🇹🇿𝕏
🇹🇿🇦🇴🇮🇩 Early today in Jakarta, #Tanzania’s Ambassador to Indonesia, Hon. Macocha Moshe Tembele, received Hon. Amb. Florêncio De Almeida, #Angolan Ambassador to Indonesia when he paid a courtesy visit to the Tanzania House.
Abertus Paschal 🇹🇿𝕏 tweet mediaAbertus Paschal 🇹🇿𝕏 tweet mediaAbertus Paschal 🇹🇿𝕏 tweet media
English
3
5
5
423
Macocha Tembele retweetledi
Tanzania Embassy | Jakarta
Tanzania Embassy | Jakarta@UbaloziJakarta·
MABALOZI WA NCHI ZA AFRIKA ZENYE UWAKILISHI NCHINI INDONESIA WAKIONGOZWA NA BALOZI MACOCHA TEMBELE WAKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA INDONESIA Mabalozi wa nchi za Afrika zenye uwakilishi nchini Indonesia wakiongozwa na Mheshimiwa Macocha Moshe Tembele, Amidi wa Mabalozi wa Afrika, ambaye pia ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Indonesia, tarehe 15 Januari,2026 walikutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Sugiono, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Indonesia. Lengo la mazungumzo hayo ilikuwa ni kupata uelewa wa pamoja kuhusu mtazamo wa Serikali, maeneo yake ya vipaumbele kuhusu Afrika pamoja na mwelekeo wa Sera ya Mambo ya Nje ya Serikali mpya ya Indonesia kuhusu Afrika. Kupitia Mkutano huo, Mheshimiwa Waziri Sugiono aliwahakikishia Mabalozi hao kuwa, Indonesia itaendelea kuthamini Uhusiano wa Kirafiki na Wakihistoria uliopo kati yake na nchi za Afrika ulioasisiwa katika Mkutano wa Bandung wa mwaka 1955 uliolenga kuimarisha umoja na mshikamano, ushirikiano, kupinga ukoloni, na kukuza maendeleo ya pamoja baina ya nchi za Asia na Afrika. Aidha, Mheshimiwa Waziri Sugiono alibainisha kuwa, Serikali ya Indonesia imejipanga kikamilifu kuimarisha zaidi ushirikiano wa kiuchumi kati yake na nchi za Afrika kupitia biashara na uwekezaji. Vilevile, alieleza kuwa, Indonesia itaendelea kutoa fursa nyingi zaidi za ufadhili wa mafunzo (scholarship) ya muda mrefu na muda mfupi kwa nchi za Afrika. Mwisho, Mheshimiwa Waziri Sugiono alibainisha kuwa, anakusudia kufanya ziara katika nchi mbalimbali za Afrika katika siku za usoni kwa lengo la kuimarisha zaidi Uhusiano wa Kidiplomasia na ushirikiano kati ya Indonesia na nchi za Afrika.
Tanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet media
Indonesia
0
2
1
140
Macocha Tembele retweetledi
Tanzania Embassy | Jakarta
Tanzania Embassy | Jakarta@UbaloziJakarta·
BALOZI TEMBELE AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MKUU WA KURUGENZI YA ASIA-PACIFIC NA AFRIKA WA WIZARA YA MAMBO YA NJE YA INDONESIA Mheshimiwa Macocha Moshe Tembele, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Indonesia na Amidi Mkuu wa Mabalozi wa nchi za Afrika zenye uwakilishi nchini Indonesia amekutana na kufanya mazungumzo na Dr. Santo Darmosumarto, Mkurugenzi Mkuu wa Kurugenzi ya Asia-Pacific na Afrika wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Indonesia. Mazungumzo hayo yamefanyika mapema leo tarehe 13 Januari,2026 katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje ya Indonesia (KEMLU) na kuhudhuriwa na Bi. Dewi Justicia Meidiwaty, Mkurugenzi wa Masuala ya Afrika, na Bi. Febrian Irawati Mamesah, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda wa Asia-Pacific na Afrika wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Indonesia. Aidha, mazungumzo hayo yalijikita zaidi kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Indonesia pamoja na maandalizi ya Mkutano baina ya Mheshimiwa Sugiono, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Indonesia na Mabalozi wa nchi za Afrika zenye uwakilishi nchini Indonesia unaotarajiwa kufanyika tarehe 15 Januari, 2026.
Tanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet media
Indonesia
0
1
0
145
Macocha Tembele retweetledi
Tanzania Embassy | Jakarta
Tanzania Embassy | Jakarta@UbaloziJakarta·
TANZANIA NA SINGAPORE KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Singapore zimekubaliana kuimarisha zaidi ushirikiano wa kiuchumi utakaowanufaisha wananchi wa mataifa hayo mawili. Hayo yamebainishwa wakati wa mazungumzo rasmi baina ya Mheshimiwa Macocha Moshe Tembele, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Singapore na Mheshimiwa Dkt. Vivian Balakrishnan, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Singapore yaliyofanyika mapema leo katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje ya Singapore. Viongozi hao wamekubaliana kuhusu umuhimu wa kukamilisha majadiliano ya Mkataba wa Uwili wa Kukuza na Kulinda Uwekezaji(BIT) na majadiliano ya Mkataba wa Kutotoza Kodi mara Mbili (DTA) kama hatua muhimu ya kuchochea fursa zaidi za ushirikiano wa kiuchumi katika sekta za biashara na uwekezaji kwa maslahi mapana ya wananchi wa pande zote mbili. Aidha, Mheshimiwa Balozi ametoa wito kwa mashirika ya Serikali na sekta binafsi ya Singapore kuchangamkia fursa za uwekezaji katika Miradi mbalimbali ya Kimkakati iliyopo nchini Tanzania hususani katika sekta za mafuta na gesi, nishati, madini,TEHAMA na miundombinu. Kwa upande wake, Mheshimiwa Waziri Dkt. Balakrishnan alimhakikishia Mheshimiwa Balozi kuwa, Singapore inathamini uhusiano wa kirafiki uliopo baina yake na Tanzania na inakusudia kuongeza zaidi mwingiliano wake wa kiuchumi na Tanzania kupitia biashara na uwekezaji katika miradi mbalimbali ya kimkakati iliyopo nchini, mara baada ya kukamilika kwa majadiliano ya Mikataba ya BIT na DTA. Vilevile, Mheshimiwa Waziri Dkt. Balakrishnan alimhakikishia Mheshimiwa Balozi kuwa,Tanzania itaendelea kunufaika zaidi na fursa za ufadhili wa masomo ya muda mrefu na muda mfupi yanayotolewa na Serikali ya Singapore kupitia Mpango wa Ushirikiano wa Singapore (SCP) na kutoa wito kwa Watanzania kuchangamkia zaidi fursa hizo. Tarehe 12 Disemba, 2025 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Singapore zitakuwa zinaadhimisha miaka 45 tangu kuanzishwa kwa Uhusiano wa Kidiplomasia.
Tanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet mediaTanzania Embassy | Jakarta tweet media
Indonesia
0
2
1
351
Macocha Tembele
Macocha Tembele@mactembele·
Kufuatia mwaliko wa Mkuu wa Chuo cha @cbeofficial1965 nimekubali heshima ya kushiriki kama mmoja wa Wachokoza Mada (Keynote Speakers) kwenye Kongamano la Sita la Maendeleo ya Biashara na Uchumi (BEDC2025) lililoandaliwa na Chuo hicho ikiwa ni sehemu ya sherehe za miaka 65 ya kuanzishwa kwake. Nimepewa jukumu la kuangazia mtazamo wangu juu ya taathira za siasa-kanda(Geopolitics) kwenye juhudi zetu za kujitafutia maendeleo stahamilivu na shirikishi. Nina shauku kubwa ya kushiriki na kubadilishana mawazo na kuchavusha fikra zetu juu ya mada hii muhimu hususan kwenye dunia ya sasa yenye mtanziko mkubwa
Macocha Tembele tweet media
Filipino
1
3
9
639
Macocha Tembele
Macocha Tembele@mactembele·
Nimesaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Kenya hapa Jakarta kufuatia kifo cha Mhe. Raila Odinga (Baba), Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya. Alikuwa Mwanasiasa mahiri na mwanamajumui wa Afrika asiyetiliwa shaka ambae umuhimu wake umedumu kwa miongo kadhaa kwenye sio tu siasa za #Kenya bali za kanda yetu ya kusini mwa Afrika na hata katika bara zima. Mwendo ameumaliza Baba, tunakuombea mapumziko mema
Macocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet mediaMacocha Tembele tweet media
Indonesia
0
2
4
303
Macocha Tembele
Macocha Tembele@mactembele·
Nimealikwa na nimekubali kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa Asia na Afrika kuhusu njia mbadala la usuluhishi wa migogoro ya kibiashara ulioandaliwa na Bodi ya Usuluhishi Migogoro ya Indonesia (DSI). Jinsi biashara ya kimataifa inavyokua ndio jinsi njia mbadala za usuluhishi wa migogoro zinavyozidi kuwa muhimu, ukizingatia kuwa njia nyingine sio tu zina gharama lakini pia zinakwaza mahusiano ya kibiashara yaliyojengwa kwa muda mrefu. Mkutano huu utaangazia namna ya kukumbatia njia hii muhimu sio tu kwenye kutatua migogoro ya biashara, bali pia kuhifadhi mahusiano. Nimealikwa kuchokoza mjadala kwenye mada hii
Macocha Tembele tweet media
Indonesia
0
0
2
106