TRT Afrika Swahili

16.7K posts

TRT Afrika Swahili banner
TRT Afrika Swahili

TRT Afrika Swahili

@trtafrikaSW

Afrika kama ilivyo

Katılım Ağustos 2022
24 Takip Edilen43.1K Takipçiler
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Baada ya wiki kadhaa za sintofahamu, hatimaye serikali ya Kenya imelipa ada ya kiasi cha Dola milioni 30 (Shilingi bilioni 3.9 za Kenya), kama ada ya kuandaa michuano ya AFCON 2027, hapo mwakani. Katika taarifa yake iliyotolewa Machi 31, 2026, waziri wa michezo wa nchi hiyo, Salim Mvurya amesema kuwa Kenya imefanikiwa kulipa ada hiyo, kama ilivyokuwa imeelekezwa na Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF).
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
11
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Michel Kuka Mboladinga, yule shabiki, aliyepata umaarufu mkubwa wakati wa fainali za AFCON 2025 nchini Morocco, atakosa kushiriki mechi ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia, baada ya kukosa viza ya kusafiri hadi Mexico.  DRC itakutana na Jamaica, Aprili 1, 2026 katika mechi ya kufuzu michuano hiyo mikubwa, inayoandaliwa kwa pamoja na Marekani, Canada na Mexico. Hata hivyo, ‘Lumumba Vea’, bado ana nafasi ya kupata viza nyingine kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia, iwapo DRC itafuzu, zikiwa zimebaki siku 72, kabla ya kuanza kwake.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
24
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Viongozi wa Kikatoliki walipata wakati mgumu kuadhimisha ibada ya Jumapili ya Matawi siku ya Machi 29, baada ya kuzuiwa kuingia ndani ya kanisa kuadhimisha ibada hiyo.
Indonesia
0
0
0
33
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Ulaya iko katika njia panda—ndani ya Bunge la Ulaya, kura kali kuhusu uhamiaji inaweza kuunda upya mipaka, sera, na mamilioni ya maisha. Lakini nyuma ya siasa ni watu halisi - wafanyakazi, familia, na wakimbizi - ambao wanasaidia kuimarisha uchumi wa Umoja wa Ulaya.
Indonesia
0
0
0
35
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Kundi lenye silaha limewaua watu wasiopungua 20 katika eneo la chuo kikuu kaskazini kati mwa Nigeria, kusababisha mamlaka kutangaza amri ya kutotoka nje kwa saa 48 trtafrika.com/swahili/articl…
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
43
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi na wa Pakistan Ishaq Dar – vyanzo vya kidiplomasia
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
82
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wamejadili hali ilivyo Mashariki ya Kati na juhudi za kumaliza vita vinavyoendelea vya Iran wakati wa mazungumzo kwa njia ya simu, Vyanzo vya Kidiplomasia vya Uturuki vinasema
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
54
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Mlipuko wa kipindupindu katika gereza moja magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umesababisha vifo vya wafungwa 11 na kuwaambukiza wengine kadhaa, wizara ya sheria ilisema siku ya Jumatatu trtafrika.com/swahili/articl…
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
26
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais wa serikali ya Jimbo la Kurdi ya Iraq, Nechirvan Barzani: - Wamejadili mapigano katika kanda na yanayoendelea kwa sasa - Alitoa salamu zake za rambirambi kwa Barzani kufuatia mashambulizi katika nyumba yake - Alisisitiza kuwa Uturuki inapinga vikali mashambulizi kama hayo na kwamba migogoro katika kanda yetu yanatakiwa kufikia kikomo mara moja
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
2
46
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Vurugu zimezuka katika mji wa KuGompo, Afrika Kusini, baada ya waandamanaji wenye hasira kuchoma moto magari na majengo, wakilenga mali za raia wa kigeni. Maandamano hayo yanafuatia kutawazwa kwa kiongozi wa Waigbo wa Nigeria Solomon Ogbonna Eziko kama “Igwe Ndigbo,” hatua ambayo imesababisha hasira miongoni mwa baadhi ya wenyeji kuona kama kudharau utamaduni wao.
Indonesia
0
0
0
110
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Tani bilioni 1.3 za chakula, karibu thuluthi moja ya vyakula vyote vinavyozalishwa duniani, hutupwa kila mwaka.  Ilhali kuna watu milioni 295 wanakabiliwa na njaa kali, na mamilioni ya watoto wakiwa hawana chakula.  Hizi ni baadhi ya nchi ambazo hutupa kiwango kikubwa cha chakula
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
37
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Wizara ya Ulinzi ya Uturuki: - Makombora ya balistiki, ambayo yanaaminika kurushwa kutoka Iran na kufika anga ya Uturuki, yamekatwa makali na mifumo ya ulinzi ya anga na makombora ya NATO iliopelekwa Mashariki ya Mediterania - Hatua zote muhimu bila kusita zimechukuliwa dhidi ya tishio lolote lililoelekezwa kwa mipaka ya nchi na anga yetu - Yote yanayoendelea katika kanda yanafuatiliwa kwa karibu huku kipaumbele kikiwa kwa usalama wa taifa letu
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
43
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Uchaguzi wa kumpata mrithi wa Umoja wa Mataifa Antonio Gutteres utafanyika Disemba 2026. Mataifa wanachama takriban 20 wamekataa pendekezo la Burundi la kumpitisha Rais wa zamani wa Senegal Macky Sall kuwa mgombea rasmi wa bara wakidai mchakato muafaka wa kumteua haukufuatwa. Kwa hivyo, ingawa nchi kadhaa zilimuunga mkono, lakini uungwaji mkono wake rasmi haujakamilika kutokana na nchi hizo kukataa uamuzi huo.
Indonesia
0
0
1
89
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Video ya Rais wa Rwanda Paul Kagame akiagiza baadhi ya maafisa wa serikali kusimama wakati wa hotuba yake Machi 23, 2026 imesambaa mitandaoni. Akionekana kukasirika, Kagame aliwaambia maafisa hao kusimama kwa sababu baadhi yao walikuwa "wanalala" wakati yeye akizungumzia kuhusu masuala muhimu ya utendakazi wao na maslahi ya wananchi. Katika hotuba yake, Kagame alieleza kuhusu makosa ya taasisi za umma, kutotafuta wafanyakazi hodari, kutozingatia vipaumbele mahsusi, matumizi mabaya ya raslimali za umma, na kushindwa kufuatilia utekelezaji wa miradi ya serikali. Hali hii ilijitokeza katika Chuo Cha Kijeshi cha Rwanda huko Gako, kilichoko Mkoa wa Mashariki nchini humo.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
2
46
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Je, unajua baadhi ya samaki wanaweza kuwa na thamani kubwa kuliko hata bei ya magari, mifugo, au nyumba? Rekodi zinaonesha baadhi yao wameuzwa kwa mamilioni ya dola hasa katika bara Asia. Samaki hawa wanathaminiwa kutokana na upekee wao, uzuri, na umuhimu wa kitamaduni, wakionesha utajiri wa hazina ya baharini na ndoto kuu ya kila mvuvi. Hawa ndio baadhi ya samaki ghali zaidi duniani.
TRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
1
0
0
118
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Milioni 6 Hiyo ndiyo idadi ya watu ambayo, kutokana na vita vya Israel wamelazimika kuondoka katika makazi yao katika kipindi cha miaka miwili na nusu tu. Milioni tatu nchini Iran. Milioni mbili Gaza ya Palestina. Milioni moja Lebanon. Wataalamu wanasema juhudi za Israel za kuwatimua watu kutoka katika ardhi za mababu zao ni mkakati wa makusudi.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
43
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cape Town nchini Afrika Kusini unaendelea kushika nafasi yake kama uwanja bora wa ndege Afrika, kwa mujibu wa ripoti ya  Skytrax World Airport Awards. Kiwango hicho, ambacho ni cha juu duniani kwa wasafiri wa anga, kinatathmini ubora wa huduma, na ubora wa miundombinu kulingana na maoni ya abiria. Hivi ni viwanja 10 bora vya ndege katika bara.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
64
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Malengo ya Marekani na Israel hapo awali yalilenga kuizuia Iran kutengeneza silaha za nyuklia na kubadilisha utawala wa nchi hiyo. Hata hivyo, wiki nne zimepita sasa, Marekani inaonekana kuweka malengo mapya ambayo yanalenga kudhibiti raslimali za mafuta za Iran na Mlango Bahari wa Hormuz. Je, haya yalikuwa ndio malengo halisi ya Marekani tangu awali ya kudhibiti mafuta ya Iran?
Indonesia
0
1
1
62