TRT Afrika Swahili

17.9K posts

TRT Afrika Swahili banner
TRT Afrika Swahili

TRT Afrika Swahili

@trtafrikaSW

Afrika kama ilivyo

Katılım Ağustos 2022
24 Takip Edilen43K Takipçiler
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Thailand imeweka masharti ya lazima ya karantini ya siku 21 kwa wasafiri wanaotoka au waliopitia Jamhuri Kidemokrasia ya Congo au Uganda ili kudhibiti uwezekano wa maambukizi ya Ebola. Wasafiri walio na dalili au wasio "na dalili za Ebola lazima wakae karantini kwa siku zisizopungua 21", wizara ya afya ya Thailand imesema katika taarifa siku ya Jumanne.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
62
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Wabunge wa Tanzania wameeleza msimamo wao bungeni wakisisitiza kuwa nchi hiyo ni huru na inatakiwa kuheshimiwa katika masuala ya uhusiano wa kimataifa, kufuatia kauli za baadhi ya wabunge wa Marekani zilizoibua wasiwasi kuhusu hali ya uhuru wa kisiasa na haki za kiraia nchini. Akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje, mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, amesema Tanzania haiwezi kupimwa au kudhalilishwa kwa kutumia changamoto zake za ndani, bali inatakiwa kuendeleza ushirikiano wa kimataifa kwa misingi ya kuheshimiana.
Indonesia
0
0
1
29
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Siku ya Arafah ni miongoni mwa siku tukufu zaidi kwa Waislamu na pia ni nguzo kuu ya ibada ya Hajj. Mahujaji hukusanyika katika eneo la Arafah wakifanya dua, toba na kuomba rehema za Mwenyezi Mungu. Kwa Waislamu wasiokuwa katika ibada ya Hajj, huitumia siku hiyo kwa kuongeza kufanya ibada, kufunga na kuzidisha dua nyingi.
Indonesia
0
0
0
22
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na mwenzake wa Iran Masoud Pezeshkian: - Tunafikia kusherehekea sikukuu ya Eid tukiwa na huzuni kwa sababu ya mgogoro katika kanda yetu; watu wa Iran watafanikiwa kuzikabili hizi changamoto na kupata amani - Uturuki inajitahidi…
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
51
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limekataa kusimamishwa kazi kwa Rais wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) Hussein Mohamed, pamoja na wajumbe wengine wa Kamati Kuu ya Kitaifa (NEC). Mnamo Aprili 24, wajumbe tisa kati ya 14 wa Kamati Kuu ya Kitaifa walipiga kura ya kumuondoa Mohamed madarakani, kwa madai ya ubadhirifu wa zabuni ya bima yenye thamani ya zaidi ya Dola 320,000 sawa na Shilingi milioni 42.4 za Kenya iliyohusishwa na michuano ya ligi za ndani barani Afrika (CHAN) ambayo iliandaliwa na nchi jirani za Uganda na Tanzania mwaka wa 2025. Kulingana na FIFA, mchakato wa kumsimamisha kazi haukufuata Kifungu cha 41 cha Katiba ya Shirikisho la Soka la Kenya (FKF), ambayo imeweka wazi jinsi maafisa wanaweza kusimamishwa kazi kwa muda au kufutwa kazi.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
120
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Mamilioni ya mahujaji wanakusanyika leo katika Mlima wa Arafa nje ya jiji la Makkah ili kuadhimisha siku hiyo muhimu zaidi ya Hajj. Wengi wakiwasili mapema kabla ya kupambazuka, Waislamu kutoka matabaka mbalimbali wanaitumia siku nzima kuzidisha ibada.  Siku ya Arafa inachukuliwa kuwa na umuhimu zaidi katika kalenda ya Kiislamu.
Indonesia
0
0
0
63
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Wabunge wa Tanzania wameeleza msimamo wao bungeni wakisisitiza kuwa nchi hiyo ni huru na inatakiwa kuheshimiwa katika masuala ya uhusiano wa kimataifa, kufuatia kauli za baadhi ya wabunge wa Marekani zilizoibua wasiwasi kuhusu hali ya uhuru wa kisiasa na haki za kiraia nchini humo. Mjadala huo umeibuka baada ya kauli za wabunge wa Marekani kupendekeza kutafakari upya uhusiano wao na Tanzania.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
61
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Hajj ni ibada ya kila mwaka ambayo inawaleta pamoja mamilioni ya waumini wa Kiislamu katika mji mtukufu wa Makka nchini Saudi Arabia, lengo likiwa ni kushiriki ibada hiyo kama ilivyofundishwa na Mtume Mohammad kwa wafuasi wake karne 14 zilizopita. Ikiwa ni nguzo ya tano katika Uislamu, kila Muislamu anatakiwa kufanya ibadi hiyo angalau mara moja katika maisha yake iwapo atakuwa na uwezo wa kiafya na kifedha. Inaashiria kiwango kikubwa cha imani, kujitolea na umoja.
TRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
34
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewaapisha majaji wapya tisa wa Mahakama Rufani ya nchi hiyo.  Sherehe hizo zimefanyika katika Ikulu ya Dar es Salaam. Rais Samia ailwateuwa majaji hao hivi karibuni.
TRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
45
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Bunge la Senegal limemchagua aliyekuwa Waziri Mkuu Ousmane Sonko kuwa spika siku ya Jumanne, hatua ambayo itampa nafasi ya kuwa mpinzani wa Rais Bassirou Diomaye Faye. Spika wa bunge El Malick Ndiaye alijiuzulu siku ya Jumapili hatua ambayo wachambuzi wanasema ilikuwa ya wazi ya kumpa Ousmane Sonko nafasi kuwania uongozi wa bunge, ambapo chama chake cha Pastef kina wabunge wengi. Rais Faye alimfuta kazi Sonko siku ya Ijumaa na kuvunja baraza la mawaziri.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
1
1
84
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Rais wa Jamhuri ya Congo Denis Sassou Nguesso ametangaza nchi yake kuondoa viza kwa raia wa Afrika kuanzia Januari 1, 2027. Rais Nguesso pia aliunga mkono pendekezo la matumizi ya hati moja ya kusafiria ya Afrika. Alitoa tangazo hilo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afrika yaliyofanyika pamoja na Mikutano Benki ya Maendeleo ya Afrika, mwaka 2026 huko Brazzaville. Nguesso alisema uamuzi huo unalenga kuimarisha umoja wa Afrika, ushirikiano wa kikanda na utekelezaji wa Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA), ambao unalenga kukuza biashara ya ndani ya Afrika na uchumi jumuishi.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
28
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Leo XIV ametoa wito kwa watu duniani kuwa waangalifu katika kukabiliana na akili mnemba (AI) na kuhimiza uwazi katika mchakato wa maendeleo. Alitoa barua yake ya kwanza siku ya Jumatatu, iliyoongelea jinsi ya kumlinda binadamu katika wakati wa Akili Mnemba. Barua hiyo inasisitiza umuhimu wa kukabiliana na Akili Mnemba kwa tahadhari na kutoiruhusu kuchukua nafasi ya ubinadamu.
TRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
25
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Kila mwaka, mamilioni wa mahujaji wanakunywa maji ya Zamzam, kisima ambacho kinaaminiwa kutoka maji kwa zaidi ya miaka 4,000. Katika dini ya Kiislamu, maji ya Zamzam yanaonekana kama moja ya miujiza inayoendelea kuwepo, na ishara ya utukufu. Hivi ndivyo maji hayo yalivyo tofauti na maji mengine.
TRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
16
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Takriban Waislamu milioni 2 wanashiriki ibada ya Hajj mwaka huu, ambayo ni moja ya nguzo tano katika Uislamu inayotekelezwa kila mwaka. Ibada ya Hajj huleta pamoja kila mwaka mahujaji kutoka pande mbalimbali za dunia, na kuifanya Hajj kuwa moja ya mikusanyiko mikubwa zaidi ya kidini duniani. Lakini wakati wa janga la Covid-19, idadi ilipungua sana. Saudia iliwaruhusu mahujaji 10,000 pekee mwaka wa 2020 kabla ya idadi kuanza kuongezeka tena pole pole katika miaka iliyofuata. Hivi ndivyo idadi ya mahujaji inavyoongezeka kila mwaka.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
35
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amewatahadharisha wananchi wake kuchukua hatua za kujilinda na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola ili kuhakikisha kuwa wanazuia kuenea kwa ugonjwa huo. Rais Museveni, wakati anahutubia kwa mara ya kwanza bunge la 12, baada ya kuapishwa kuongoza kwa muhula mwengine, alitoa mfano wa wabunge hao walikuwa wamekaa karibu bila kuchukua tahadhari yoyote. Uganda tayari imesajili wagonjwa 7 waliothibitishwa kuwa na maambukizi ya Ebola na kifo cha mtu mmoja.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
1
77
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Chama kikuu cha upinzani Uturuki, CHP, kinakabiliwa na moja ya mgogoro mkubwa katika historia yake ya hivi karibuni. Haya ni baadhi ya matukio kuelekea mgogoro huo
Filipino
0
0
0
30
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Watu wawili wanashukiwa kupata maambukizi ya Ebola huko Milan, kaskazini mwa Italy, kulingana na gazeti la kila siku la Italia Corriere della Sera. Watu hao, ambao ni wa jinsia mbili tofauti, wenye asili ya Como, inasemekana walirudi hivi karibuni kutoka Uganda, ambako walikuwa wakifanya kazi ya kutoa misaada kwa miezi mitatu. Waliripotiwa kupata dalili, ikiwa ni pamoja na homa kali, kutapika, kuharisha, na kichefuchefu.
TRT Afrika Swahili tweet media
Indonesia
0
0
0
100
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Mgogoro katika chama kikuu cha upinzani cha Uturuki
TRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet media
0
0
0
29
TRT Afrika Swahili
TRT Afrika Swahili@trtafrikaSW·
Uamuzi uliotolewa na mahakama ulichochea mgogoro na mpasuko mkubwa katika chama kikuu cha upinzani cha Uturuki.
TRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet mediaTRT Afrika Swahili tweet media
Polski
1
0
0
36