ทวีตที่ปักหมุด

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA , BAADA, NA WAKATI WA INTERVIEW YA KAZI. Namba tano zitakusaidia sana.
KABLA YA INTERVIEW, ZINGATIA:
1. Chunguza kampuni na msimamo yao.
2. Kagua wasifu(CV) wako na uandae hoja za kuzungumza.
3. Jizoeze maswali ya kawaida ya mahojianokwa ufupi na uwazi.
4. Vaa ipasavyo na kukusanya nyaraka muhimu.
5. Hakikishi kuwa unafika kwa wakati.
WAKATI WA INTERVIEW, HAKIKISHA:
1. Kuwa mwangalifu na mmsikivu.
2. Dumisha lugha nzuri ya mwili (Body Language) na mawasiliano ya macho (Eye Contact).
3. Sikiliza kwa makini na uulize maswali RELEVANT. kama
-Kwasasa changamoto gani mmezipa kipaumbele cha juu zaidi ktk position uliyoomba kazi
-Yapi matarajio ya kampuni kwa miaka mitano ijayo
-Department gani nitakua nafanya nayo kazi zaidi, na muingiliano wa majukumu upoje.
Kadri unavyouliza maswali relevant ndivyo unaonekana upo serious na hiyo kazi.
4. Highlight ujuzi wako na uzoefu unaohusiana na jukumu/role unayoomba.
5. Toa majibu ya wazi na mafupi.
Baada ya INTERVIEW, ni muhimu ku:
1. Tuma ujumbe wa asante au barua pepe ili kutoa shukrani. mfano,
Dear Sir/ Madam, Asante kwa nafasi ya kuhojiwa kwa nafasi hiyo leo na kampuni yako. Nilifurahia sana mchakato huo na kujifunza zaidi kuhusu kampuni yako. Ikiwa unahitaji maelezo zaidi ya kukusaidia kufanya uamuzi, tafadhali usisite kuwasiliana nami.
Mwisho nikutakie kila la kheri huko uendako, Kaa chanya na uendelee kujiamini katika uwezo wako, Endelea kutafuta kazi na uzingatie fursa zingine.
follow for more tips and turn on notification please retweet iwafikie wengi usisahau ku like.

Indonesia




























