Sasa wanasubiri nini mpaka saa hizi si wamtimue tu dadeki zake
Ndani ya miezi miwili kocha kashinda mechi mbili tu za ligi tena kwa uwezo binafsi wa wachezaji
🚨𝐔𝐏𝐃𝐀𝐓𝐄
“Kama Viongozi wanataka kuwapeleka wachambuzi mahakamani nadhani na sisi wachambuzi tujiandae kuwafungulia mashtaka ya Upangaji wa matokeo,Betting nk.
Hakuna aliyesalama sana kwenye mpira Wetu Kama vipi funikeni kombe mwanaharamu apite.
Tena sasa hivi Ndio balaa,tunajuana guys.”
- Juma Ayo, Mtangazaji na Mchambuzi wa CrownFM.
#MeaMswahiliUPDATES
@g_ki02@meamswahili@Mzeewajambia Bado tu huelewi sijui akili mnapelekaga wapi wana yanga hapo nimesema kwenye club nani anakujua au unamchango gan mpaka umpeleke popote wewe una uwezo hta wa kumshaur kiongozi wa yanga wewe. Au kupiga kelele tu waachie viongoz ndo wanajua sio kuleta kihereher 😂😂
@vitalisvedasto@mshambuliaji Wangepeleka lalalamiko tff ndo ningewaona wa maana sasa wanapeleka sehem ya kazi kuumbe hawana kesi nae wana kesi na redio au kibarua chake😂😂😂
Klabu ya Yanga SC, kupitia kampuni ya Uwakili ya ‘M/S Nassoro & Co. Advocates’ imewasilisha barua ya malalamiko mazito ya kisheria dhidi ya kampuni ya EFM/TVE ikilalamikia kashfa zinazotolewa na mfanyakazi wa Kampuni hiyo, Wilson John Oruma katika uchambuzi wake wa michezo ambao unachafua taswira ya klabu hiyo.
Katika barua hiyo Yanga SC imesema mchambuzi huyo amekuwa akitumia studio za EFM/TVE kutoa taarifa zinazodai klabu hiyo inashinda kwa njia za rushwa na kupanga matokeo hatua ambayo imedai inapunguza heshima, inavuruga mikataba ya udhamini, na kuchochea chuki.
Ikiainisha mambo kadhaa kama msingi wa malalamiko yake yakiwemo madai ya kampeni endelevu kwenye vipindi vya EFM/TVE ambao imedai watangazaji wake wamekuwa na utaratibu wa muda mrefu kuichafua klabu hiyo ikitolea mfano uchambuzi uliofanywa na watangazaji baada ya ushindi wa 6-0 dhidi ya Mbeya City, ambapo kauli zilizotolewa ziliashiria mchezo huo haukuwa wa haki.
Young Africans SC imedai uchambuzi huo umeonesha kutokuwa na imani na uhalali wa ushindi huo huku ikitaka mamlaka husika kuingilia kati ikitafsiri hatua hiyo kama kuivunjia heshima kwani kitendo hicho kinaharibu jina, hadhi, na heshima ya klabu kwa wanachama, mashabiki, na wadhamini.
#KitengeSports