Thom Mnkondya@Thommunkondya
Kuna mshikaji wangu, baada ya kumaliza chuo alipata kazi ya jiji. Wakati huo mimi naendelea na udalali wa kupangisha vyumba kwa wanafunzi.
Siku moja, nimetoka mishe zangu Kigamboni, nikakutana naye mitaa ya Lumumba. Alikuwa amemkaba jamaa mmoja aliyekuwa na bodaboda. Nikamuuliza, “Oya, shida nini?” Akasema amepita sehemu ambayo hakutakiwa kupita. Nikamwambia, “Ni shilingi ngapi, nimlipie?” Wakagoma, wakaamua kuchukua pikipiki ya yule jamaa. Roho iliniuma sana.
Nikamuuita rafiki yangu pembeni, nikamwambia:
“Mwanangu, umechagua kazi ya kimaskini sana, na ya roho mbaya mno. Huwezi kufanikiwa kwa kazi hii. Umechagua kunyanyasa maskini wenzetu. Nchi yetu vijana wengi hawana ajira, elimu, wala exposure, na wengi ni maskini. Ili kuwacontrol hawa watu, ni lazima kuwe na mazingira wezeshi ya kupata riziki au uwape ajira. Lakini hivi hivi, hata uweke sheria kali vipi, kama hawapati kipato hawataweza kutii. Tafuta kazi nyingine. Hii si kazi ya kijana msomi wa chuo, tena UDSM.”
Nikamuacha pale nikaendelea na mambo yangu.
Kumbe yale maneno yalimgusa sana. Akaondoka, akaanza kujitafuta Kkoo, Mungu akambariki, akaanza biashara za kwenda China. Leo hii amefanikiwa sana.
Juzi nilikuwa na kikao Palm Village na wachina wanaotaka eneo la kujenga kiwanda. Nikawapeleka kwenye site zetu, wakapenda. Tukakutana kwa ajili ya discussion kumbe jamaa ndiye aliyewaleta.😀
Nilipofika pale, akanishukuru sana. Akasema yale maneno yangu ndiyo yaliyombadilisha na leo ana maisha mazuri. Nikamwambia kwa utani, “Kama ni kunishukuru, hakikisha hawa wachina wananunua eneo letu nawasubiri!” 😂😂
Kwa kweli nilifurahi sana.
Kwa Bongo, kufanya kazi za enforcement bila kutumia akili au huruma ni lawama tupu. Inahitaji busara kubwa, vinginevyo unajikuta unawaumiza watu maskini ambao tayari wanapambana na maisha.