Levodopacarbidopa
1.3K posts

Levodopacarbidopa retweetledi


@MwanaHabariNews Huyu jamaa huwa haaminik kabisa mtu wa ndimi mbili
Indonesia

@IAMartin_ Nakumbuka, siku ambayo matokeo yanatangazwa, eneo la magereza, Bomani polisi walizuia njia na kupiga mabomu ya machozi. Waliharibu gari ya muziki.
Huyu jamaa sijui alipoteleaga wap alikuaga anasukuma toroli pale mitaa ya kuingia sokon
Indonesia

Leo naikumbuka; Jumatatu, Oktoba 13, 2008 (miaka 17 iliyopita)
Mwaka ambao alifariki mbunge wa Tarime (kabla ya kugawanywa kuwa majimbo mawili) pia alikuwa ni Diwani wa kata ya Tarime Mjini Chacha Zakayo Wangwe
Chacha Zakayo Wangwe alifariki kwa inayoelezwa ni ajali ya gari, Kibaigwa, Dodoma. Hivyo jimbo na kata kubaki wazi bila mbunge na Diwani kwa wakati mmoja.
Mchakato wa kumtafuta mgombea ubunge wa CHADEMA, ulifanyika ukumbi wa AMA-HOTEL, na kufanikiwa kumpata Charles Mwera Nyanguru
Kupeperusha bendera ya CDM. Alikuwa ni Diwani kata ya Nyanungu wakati huo na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Tarime. Alishinda tukiamini ni mzoefu.
Kampeni zile, nilishiriki mwanzo mwisho. Kuanzia siku ya kwanza hadi siku ya mwisho. JUA na MVUA, nikiondoka asubuhi na kurejea usiku nyumbani, kila siku.
Nilifika kata zote, nikiwa na rafiki yangu KOTIDE (apumzike kwa amani) na NABII (amehamia CCM sasa) wakitoa hamasa ya muziki na kutumbuiza.
Ndugu zangu hawa, walitumbuiza katika mikutano ya kampeni ya mgombea ubunge CDM. Tulizunguka jimbo zima. Kwangu, pasi na kulipwa na mtu yoyote.
Kutokana na ukaribu wangu wakati huo wa kupenda CHADEMA, NABII (msanii wa kughani aliyeletwa na KOTIDE) alijitokeza kuwa rafiki yangu mkubwa.
NABII alitoka makao makuu ya kutumbuiza pamoja na KOTIDE. Jioni baada ya kampeni, tunashinda wote, na nyakati zote alikuwa akilala nyumbani kwetu sisi.
Mama yangu alimpenda sana. Alikuwa akitupikia chakula cha jioni na asubuhi, tunakula sote. Mchana hatupo kwa sababu tumekwenda kwenye kampeni, huko vijijini.
(Baadae nilisikia NABII alihamia CCM. KOTIDE alifariki. NABII alikuwa na kigongo chake, nitakitafuta, halafu nitakipandisha msikilize. Ameyachana MaCCM)
Naam. Vuguvugu la mabadiliko lilikuwa kubwa nyakati hizi, huu ndio wakati ambao siasa ya Tanzania ilianza upya kupata moto. TARIME ilikuwa imeiva sana.
Uchaguzi ule ulileta kauli mbiu ya kisiasa na baadae ilikwenda kuibua hisia kali na haya kutumika katika uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru Mashariki
Huko ilizaliwa kauli ya “MAMBO KAMA TARIME” na hata kushinda uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki kwa Josh Nassari kwa kutumia kauli ile.
Nyakati hizi ndio nilipata kuwafahamu kwa karibu viongozi wengi wa CHADEMA. Nilihudhuria vikao vyao vya ndani na mikutano yao hadhara katika kampeni.
Tulifanya kampeni kubwa. Kampeni nzito. Dhidi ya mgombea ubunge wa CCM ambaye alikuwa maarufu. Mwenye fedha. Christopher Mwita Kangoye.
Pia mgombea udiwani, Tajiri sana (mabasi ya Mwanza-Tarime), Peter Zakaria. Kampeni zile ziligubikwa na fujo nyingi. Watu walikatwa mapanga na kujeruhiwa.
Nguvu ya matumizi ya dola ilikuwa kubwa. Uchaguzi ulikuwa na ‘hype’ kutokana na mazingira yenyewe. CCM walileta nguvu kazi ikiongozwa na Nape Nnauye.
Aliyechochea uchaguzi kuwa na shamra-shamra za kutisha ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Reuben Mtikila,
Mtikila ambaye alisimama viwanja vya shule ya msingi Sabasaba na kutuhumu CHADEMA kumuua Chacha Zakayo Wangwe, alipigwa mawe, na wananchi,
Baada ya kutandikwa kwa mawe ya kombeo na akapasuliwa, akapelekwa hospitali, kwa-mzalifu. Baada ya hapo ‘ALILALA MBELE’ hakugeuka nyuma.
Ni katika kampeni hizo za uchaguzi mdogo wa Tarime 2008, niliendesha baiskeli kutoka Tarime Mjini hadi kata ya Komaswa. Huo ni umbali wa 21 min (23.7 km).
Niliendesha baiskeli yangu kwa nguvu ikiwa na bendera kubwa ya CHADEMA, kwenda kumpokea aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa.
Nilitumia zaidi ya kilometa 50 kwenda na kurudi, nafika nakuta Dkt. Wilbroad Slaa ameshaanza kutoa hotuba yake eneo la Msikiti Mkuu wa ijumaa, Tarime.
Nimefika kila kiungo cha mwili kinauma balaa. Lakini sikuona shida. Nilikuwa na morali ya kuona mabadiliko ya kisiasa katika jimbo letu la uchaguzi, Tarime.
Siku ya uchaguzi, watu wakapiga kura, usiku ule wa 13.10.2008 Charles Mwera Nyanguru akatangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi ule uliokuwa mgumu sana.
Nyanguru alitangazwa mshindi kwa kupata kura 34,545 dhidi ya Christopher Kangoye (CCM) aliyepata kura 28,996 shangwe nyingi na nzito zikaanzia hapo.
Kambi ya CHADEMA na masuala ya tallying ilikuwa mtaani kwangu kabisa, nyuma ya nyumbani kwetu, katika hotel ya MAKOMA, wakati huo ya moto!
Usiku ule, Mwenyekiti Freeman Mbowe akahitaji muziki uanze kupigwa, shangwe na nderemo zianze, gari ya matangazo ilikuwa full equipped, iwashweeee.
Gari ilikuwa na sound system imara sana. Ilikuwa built-in. Gari ilikuwa na jukwaa la kufanya mikutano ya hadhara na ilikuwa na generator kubwa sana.
Gari ilikuwa hapo nje ya NGOME ya CHADEMA ya uchaguzi. Lakini dereva hayupo, lazima afuatwe anapolala. Wapi? Riverside. Magamaga pale.
Mwenyekiti Freeman Mbowe akaomba tumfuate huko anapolala, aamshwe na kufika ngome. Simu yake ilikuwa haipatikani. Saa 10 kuelekea 11 alfajiri hivi.
MMM, Mdogo wangu, marehemu sasa (Frank Maranja Masese) na Mwita MATUTU (marehemu sasa) tukaenda kumfuata Dereva na bwana KOTIDE (marehemu).
Tuliwafuata huko hotelini ili wafike ngome ili kuwasha muziki. Maana ngome hadi wakati huo watu wamejaa. Wanataka kuanza kucheza muziki. Washangilie.
Watu wa wakati ule walikuwa na morali kubwa sana kuliko sasa katika siasa. Tumefika sasa pale RIVERSIDE. Tumevaa ‘skafu’ zetu na bendera za CHADEMA.
Tumegonga. Mlinzi akafungua geti pale Roverside. Kuulizia watu tunaowahitaji, mlinzi katuweka chini ya ulinzi, walikuwa walinzi wawili. Wote wenye silaha.
Akaitwa Meneja, akasema tumekwenda kuvamia hotel. Sisi ni majambazi. Akaitwa mkurugenzi (mmiliki) wa hotel, kumbe ni kada wa CCM anaitwa KISUNTE.
Aliposikia ni watu wa CHADEMA, acha alifura kama maiti, alikasirika, akawaka, akasema tufungwe kamba na tusubiri afike hapo akitokea nyumbani kwake.
Bahati mbaya sana. Bwana KOTIDE na wenzake walipotoka ndani ya vyumba wakasema hawatufahamu. Sijui waliogopa nini wale watu. Wakatukana.
Sasa hapo ndio tukaonekana majambazi Kweli. Ndugu yetu KOTIDE na yule dereva wakaondoka kuelekea ngome maana walipigiwa simu na wakubwa.
Nikajisemea moyoni kweli tumeyavagaa. Sisi tukabaki kuchezea kichapo ‘heavyweight’ tukiwa chini ya ulinzi. Hizi kumbukumbu huwa hazinitoki kirahisi.
Tukafungwa kamba, mikono nyuma, tukaunganishwa. Wote. Martin, Frank na Mwita Matutu. Tukachezea ‘mabapa ya panga’. Tulivimba kama vitumbua
Tulichezeshewa kichapo tukiwa tumefungwa kamba. KISUNTE akatoa bastola, akasema anatu-shuti na atajibu kuwa sisi ni MAJAMBAZI tulivamia hotel kwake.
Baada ya kipigo cha kama nusu saa hivi, akatupakia kwenye TOYOTA HILUX, Pick-up (rangi ya dark blue) na kuondoka na sisi hadi keep-left ya Tarime Mjini.
Akaturudisha tena RIVERSIDE, akatufungua kamba. Tukachezea ‘mabapa’ tena ya mgongoni. Hawa MaCCM sio watu wazuri kamwe. Sio marafiki kamwe.
Hata baada ya kufahamu sisi ni watoto wa MARANJA na MATUTU (wazee maarufu Tarime mjini) bado aliendelea kushikilia msimamo wake wa kutumaliza kabisa.
Ingelikuwa zama hizi, TUNGELIPOTEZWA. Tulichezeshewa kipigo cha MBWA KOKO alfajiri ile, tukiwa tumefungwa kamba. Baridi kali sana.
Kabla ya saa moja kasoro-robo, asubuhi, akatuachia. Tukatembea kutoka pale RIVEESIDE hadi MAKOMA. Huko ndipo ilipokuwa ngome ya uchaguzi ya CHADEMA.
Tumefika ngome, tunakuta watu wengi sana wanaruka ngoma ya “CHADEMA MWENDO MDUNDO, FICHUA MAFISADI” bila wenge, watu wengi kweli-kweli.
Tukaungana nao, tukaruka debe, kuendelea kushangilia ushindi. Raha ya ushindi, hatukukumbuka hata kueleza ambayo tulikutana nayo usiku huo. Furaha tupu.
Uchaguzi wa 2008 ndio ambao ulimleta John Heche katika medani za siasa. Uchaguzi huu, katika kura za maoni alishindwa, akachukua fomu ya udiwani,
Binafsi, nikiwa kijana mdogo kabisa, nikamuunga mkono, tukapitishwa na chama. Tukapambana na moja ya tajiri mkubwa sana Tarime, anaitwa PETER ZAKARIA.
Wakati John Heche akiwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha amtakatifu Augustin (SAUT), Mwanza. Tulishinda udiwani kata ya Tarime mjini. Tulimshinda mtu tajiri sana.
Uchaguzi huu ndio uliacha watu walemavu wa mwili na viungo kadhaa, watu walipasuliwa macho kwa mabomu ya machozi, watu walivunjwa miguu na mikono yao.
Watu walishuhudia nguvu kubwa ya matumizi ya polisi isivyo kawaida. Kumbuka ni nyakati hizi ndio 'kanda maalum ya polisi Tarime na Rorya' ilikuwa imeanza.
Nakumbuka mabomu ya machozi kurushwa ndani ya hospitali ya Dr. MZALIFU katika mtaa wa Mawasiliano kata ya Bomani. Kulikuwa na mengi sana ya ajabu.
Sitaki kusimulia yaliyoendelea baada ya hapo.. Kuhusu hilo. Nyuma ya pazia. Kisasi kilienda vipi.. Lakini leo nimekumbuka sana hizi nyakati na hii siku mbaya.
Nimetoka mbali sana na hiki CHAMA. Ni sehemu ya maisha yangu. Apumzike kwa amani rafiki yangu MWITA MATUTU (cheusi), aliipenda sana CHADEMA.
Apumzike pia kwa amani huko alipo mdogo wangu, Frank Maranja Masese (Ze Don). Hawa tulizunguka jimbo lote la Tarime mwaka 2008 kutafuta kura za mgombea wetu.
Uniambie nihame CHADEMA, uelekeo uwe CHAUMA? Huko nakwenda kutimiza ndoto za nani ambaye atabeba historia yangu nikiwa CHADEMA? Haiwezekani.
MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.
Indonesia

@Ntobi_ @idualliance Au bando unakilinda chama kwa wivu mkubwa
Indonesia

Wakili Alicia Magabe, ni mke wa Mhe Tundu Lissu, walikutana wakiwa wanafunzi wa sheria UDSM mwaka 1991, na baadaye walifunga ndoa mwaka 1997. Na wamebarikiwa watoto wawili.
Hapa Mhe Adv Alicia anampigania mme wake—mbele ya mkutano wa IDU (@idualliance) 💔
#FreeTunduLissu
#FreeTunduLissuNow!
Filipino

"Mwanamke yeyote ndoto yake kubwa kuwa na Mume, katika maombi yangu yote hilo naliomba sana lakini siwezi kumpangia Mungu atayajibu lini".
"Mkisikia natangaza harusi mjue maombi yamejibu, nipate mwanaume yeyote ili mradi awe anapumua, ana hofu ya Mungu, mtu ambaye mchapakazi, asiwe Marioo, anipende mimi na kazi yangu ninayoifanya" - Muigizaji Johari
#Trending #BongoMovie #Viral #Johari

Indonesia

🎙️Samuel Eto'o : " I was sitting at home in Douala when suddenly! My phone rang.
The number? Unknown, but something in my heart said, "Answer, Samuel."
When i answered i heard "Samu? Do you still have the same number from 2009?" (He laughs quietly.)
So I said to him, "Lionel?! Even if I changed my number 100 times, I would have made you the first to know! But why are you calling in the middle of the night? Do you want to finally admit that I'm the best at pikey-pikey among us?
Then he started laughing and said, "No, this time it's bigger I've seen what you're doing in Africa, and I've seen the eyes of children in some remote villages when you visit them. I want to be part of this, but in my own way."
My heart stopped for a moment. Messi talking about Africa with such passion?!
Then I heard him say, "I want to build schools and hospitals, but not in my name. In the name of the football that brought us together." And you know the way, Samuel".
The following week, Messi secretly flew to Yaoundé. No press conferences, no cameras. Just him and me visiting a remote village.
There, we met a little girl named Ama. She was holding her worn-out ball and saying to Messi, "You're magical, but my ball doesn't fly like yours!" At that moment, I saw Messi's tears. He took out his phone and said to me, "Here. We're going to build a playground for every child in this village, and we're going to teach them that true magic is giving without expecting anything in return."
Messi didn't stop there! He launched a secret program called "10." The program collects donations from football legends to save forgotten villages in Africa.
The most beautiful thing? His only condition was: "No media, no noise, only action."
That day, I understood why Messi was "great." Not because he scores goals, but because he knows how to strike hope into the hearts of those who have no voice.
Now, whenever someone asks me, "What's the difference between Messi and all other players?" I say, "Some live to love football, and Messi lives to make football love people."
Africa doesn't need heroes seen on screens, but heroes who come down to earth and hold children's hands.
And Messi came down."
Source : [ UNICEF PODCAST]

English

@Gentamcin @prince_hoffman Kama prezidaa anapenda nyashi.. mimi nani nisipende?
Indonesia

@Gentamcin @Gaspinho15 Shida ni kwamba utajuaje kama ni wako? Unaweza jua ni wako kumbe sio wako ni wa mwingine.. mapenzi hayanaga mwalimu sahihi 😀😀😀
Filipino














