I’M ALMAS retweetledi

Naitwa Vumilia Mariki, mkazi wa Uru, Moshi, mkoani K'njaro. Naomba msaada wa matibabu kwa mwanangu Levina John (06) mwenye tatizo la miguu kupinda kiasi cha kushindwa kutembea.
Levina alizaliwa mzima kabisa na alipofikisha umri wa kutambaa alitambaa, baadaye akasimama na kisha kutembea. Lakini alipofikisha umri wa miaka minne miguu yake ilianza kupinda na ilizidi kupinda hadi akashindwa kutembea kabisa.
Kutokana na changamoto za kiuchumi nilishindwa kumpeleka hospitali hivyo nikawa nampeleka kwenye maombezi. Baadhi ya ndugu na marafiki walinishauri nimpeleke kwa waganga lakini nilikataa.
Nilimtumainia Mungu na kuamini kwamba ataniinulia watu wa kumsaidia mwanangu kusimama tena. Mimi ni single mother na kutokana na changamoto za kimaisha nilirudi kwa wazazi wangu Uru, japo hawana uwezo wa kunisaidia lakini walinitia moyo na kuniombea.
Nilihangaika maeneo mbalimbali kuomba msaada bila mafanikio. Nilikaribia kukata tamaa kuona mwanangu anakua mlemavu nami sina jinsi ya kumsaidia. Lakini nikapata msaada wa TZS 600,000/= kupitia kikundi cha “Sadaka Yetu” nikampeleka mtoto hospitali ya Mawenzi.
Baada ya vipimo aligundulika kuwa na tatizo liitwalo Tibia vara (Blount’s disease) yaani ukuaji usio wa kawaida wa sahani ya tibia inayosababisha mfupa kupinda kwa ndani.
Walinipa rufaa kwenda CCBRT kwa matibabu zaidi. Akajitokeza msamaria mwema mmoja ambaye alinichukua mimi na mtoto kwenda CCBRT Dar.
Madaktari walishauri ili mwanangu aweze kusimama tena anahitaji operesheni 4 yaani mbili kila mguu. Kila operesheni itagharimu kiasi cha TZS 1.2M hivyo jumla ni 4.8M.
Namshukuru msamaria aliyenitoa Moshi alilipia gharama za operesheni moja. Sasa imesalia operesheni moja kwenye mguu aliofanyiwa, na operesheni mbili kwa mguu mwingine.
Jumla ya gharama zinazohitajika ni 3.6M. Naomba Watanzania wanisaidie ili kumuokoa mwanangu na ulemavu. Nimeambiwa akikamilisha operesheni hizi atakuwa na uwezo wa kutembea tena. Mungu awabariki.
#MyTake:
Mimi na wewe tuna nafasi ya kumsaidia mtoto Levina kusimama tena. Tuma sadaka yako kupitia M-PESA #0752581983, Tigopesa #0719744954, CRDB #0150633516500, NMB #24110012109 Gifted Hearts Foundation. RudishaTabasamu, LetLoveLead.

Indonesia








