Polycarp The Bibliophile
47.9K posts

Polycarp The Bibliophile
@PolycarpMDM
- (Historical, Scriptures &Traditional Analyst) - (Highway Engineering) - (CAD Tech 3D Modeling) - (Machinery, Equipments & Industrial Enthusiast)






BARUA YA WAZI KWA CHADEMA Chama cha siasa ni ideology; uanachama wa chama cha siasa ni values. Chama cha siasa kinajipambanua kwa vile kinavyoamini kuhusu sera ya umma na namna jamii inavyopaswa kuenenda. Uanachama na ufuasi wa chama cha siasa unatokea pale ambapo values za mtu binafsi zinalandana na ideology ya chama cha siasa. Ideology ya chama cha siasa ni kama sumaku, inavuta values zinazolandana nacho. Katika tafsiri hii, haiwezekani mtu leo akawa CHADEMA kesho akawa CCM halafu keshokutwa akawa CHADEMA. Haiwezekani leo ukawa progressive kesho ukawa conservative halafu keshokutwa ukawa tena progressive. Haiwezekani leo ukawa mjamaa kesho ukawa mbepari halafu keshokutwa ukawa tena mjamaa. Hata ikitokea kwamba mwanachama wa chama cha siasa hakubaliani na mambo fulani ndani ya chama chake kiasi cha kutaka kujiondoa, ni vigumu kwa mwanachama huyu kujiunga na chama cha siasa chenye ideology tofauti kabisa na ile ya chama chake. Ni vigumu kwa sababu values zake zilizomvuta na kujikuta amekuwa mwanachama wa chama chenye ideology A hazilandani na chama chenye ideology B. Ikifika hatua mtu akawa na uwezo wa kuhama vyama vya siasa atakavyo, tena vyama ambavyo ni two extremes sawa na mashariki na magharibi, kuna vitu vikubwa viwili: 1. Huyu mtu sio mwanachama wala mwanasiasa, ni opportunist. Ni ile aina ya wanasiasa ambao Mwalimu Nyerere aliwaita “wanasiasa malaya malaya.” Ni malaya malaya kwa sababu hawana values; hawavutwi na ideology. Kama hauna values maana yake ni kwamba unafit popote, ni mercenary kwa lugha ya Mwalimu. All you care about is money, fame, and material rewards. That’s all. 2. Chama kinachomruhusu yeyote kutoka na kuingia atakavyo sio chama cha siasa, ni version ya chama dola. CCM ni mfano mzuri wa chama dola kwa sababu hakina ideology wala wanachama wake hawana values. Kinachowaleta pamoja ni kitu kimoja tu, MADARAKA; ni MASLAHI BINAFSI. Yeyote anaweza kusajiliwa CCM, muhimu awe tu na uwezo wa kupata madaraka. Pesa na fame ndio values za CCM, yeyote mwenye haya anaweza kusajiliwa. Hii inamaanisha pia chama cha siasa kama CHADEMA kikianza kuwa na tabia hizi za chama dola nacho kinageuka kuwa version ya chama dola. Yani kinakuwa chama dola kisichokuwa na dola. Which means kama kikipata dola nacho kitabehave vile vile kama chama dola. Kwa mantiki hiyo kitafit kabisa ile tafsiri ya “CCM B.” Na ukitaka kuupima ukweli wa hili, sikiliza ile kauli ya “CHADEMA NI CHAMA CHA SIASA, MALENGO YAKE MAKUU NI KUSHIKA DOLA.” Hii ni kauli inayoweza kutolewa na watu wasiokuwa na values ndani ya chama dola. Yes, malengo makuu ya CHADEMA KUSHIKA DOLA kama wasemavyo watu hawa hayatofautiani kivyovyote vile na malengo makuu ya CCM KUENDELEA KUBAKI KWENYE DOLA kwa njia yoyote ile. Wote wana through line moja, DOLA KWANZA UMMA BAADAE. Hii inamaanisha pia watu hawa hawajali matatizo halisi ya umma, isipokuwa wanayatumia instrumentally kufikia malengo yao (I TRULLY HOPE THIS IS NOT THE CASE). Hata hivyo changamoto kubwa hapa ni kwamba CHADEMA ikiamua kuwa na tabia za chama dola, kamwe haiwezi kuwa mbadala wa chama dola kwa sababu kitabia na yenyewe inakuwa chama dola. Ikifikia hatua hiyo, CHADEMA inabadilika na kuwa mtaji mzuri sana wa kuhalalisha matendo ya chama dola na malengo yake ya kuendelea kubaki kwenye dola. Kazi ya chama dola itakuwa kusema tu, “si mnawaona hata wao? Kuna chochote cha tofauti mnachokiona kwao?” Matokeo yake ni kuukatisha umma tamaa kwa kuufanya ufikie hitimisho kuwa “wote ni walewale.” Natamani CHADEMA ingejipambanua kama CHAMA CHA SIASA CHENYE IDEOLOGY NA WANACHAMA WENYE VALUES badala ya version ya chama dola inayorudufisha umalaya wa kisiasa. Ideology inatengeneza integrity, na matokeo ya integrity ni imani ya umma. Natumaini CHADEMA haitawafikisha watanzania kwenye ile Orwellian state ambapo wanyama waliwaangalia wanadamu kisha wakajiangalia wenyewe kisha wakawaangalia tena wanadamu na kushindwa kuelewa wapi ni wanyama na wapi ni wanadamu. Ahsante!



























