Sabitlenmiş Tweet
Polycarp The Bibliophile
45.8K posts

Polycarp The Bibliophile
@PolycarpMDM
- (Historical, Scriptures &Traditional Analyst) - (Highway Engineering) - (CAD Tech 3D Modeling) - (Machinery, Equipments & Industrial Enthusiast)
Iringa, Tanzania Katılım Mart 2018
1.3K Takip Edilen21.8K Takipçiler

Ndege ya kijeshi ya siri ya Marekani aina ya RQ-180, inayojulikana kwa uwezo wake wa hali ya juu wa kujificha dhidi ya rada (stealth), inaripotiwa kuonekana ikitua katika kambi ya anga nchini Ugiriki hapo jana, tukio ambalo limezua mjadala mkubwa kutokana na unadra kwa ndege hiyo kuonekana hadharani.
RQ-180 ni moja ya miradi ya juu kabisa ya ujasusi ya Marekani, inayoaminika kuendeshwa na United States Air Force kwa kushirikiana na kampuni ya Northrop Grumman.
Ndege hii imeundwa kwa ajili ya kuruka katika kimo ee22 sana kwa muda mrefu, ikikusanya taarifa za kijasusi (surveillance) katika maeneo yenye ulinzi mkali wa anga bila kugunduliwa kirahisi.
Kwa kawaida, uwepo wa RQ-180 hufichwa sana, na serikali ya Marekani haijawahi kuthibitisha rasmi kwa kina kuhusu uwezo wake au matumizi yake.
Hata hivyo, inaaminika kuwa hutumika kufuatilia shughuli za kijeshi katika maeneo yenye mvutano mkubwa duniani, hasa katika maeneo yenye mifumo ya kisasa ya ulinzi wa anga.
Ripoti za kuonekana kwake Ugiriki zinaeleza kuwa ndege hiyo huenda ililazimika kutua kutokana na hitilafu ya kiufundi au sababu za kiusalama.
Tukio hili limeifanya ionekane wazi mchana, jambo ambalo ni la nadra sana kwa teknolojia ya aina hii ambayo kwa kawaida hufanya operesheni zake kwa siri kubwa.
Wachambuzi wa masuala ya kijeshi wanaamini kuwa kuonekana kwa RQ-180 katika eneo la Ulaya ya Kusini kunaweza kuhusishwa na ongezeko la ufuatiliaji wa hali ya usalama katika ukanda huo, hasa kutokana na mvutano unaoendelea kati ya mataifa makubwa na shughuli za kijeshi katika maeneo ya karibu kama Mashariki ya Kati na Bahari ya Mediterania.
Kwa ujumla, tukio hili limeibua maswali mengi kuhusu operesheni za siri za Marekani, uwezo halisi wa ndege hiyo, na jukumu lake katika ujasusi wa kisasa wa kimataifa.

Indonesia


@PolycarpMDM Tunarukwa kwa sababu ya upumbavu wetu wa 29 October
Filipino

Bandari ya Lamu imepokea meli yake ya pili ya kubeba magari, iliyokuwa ikisafirisha magari 3,800 kutoka Yokohama, Japan, ambayo awali yalikuwa yakielekea Bandari ya Jebel Ali, Dubai, kutokana na mzozo unaoendelea.
Meli hiyo iitwayo Grande Florida, inamilikiwa na kampuni ya usafirishaji ya Grimaldi Shipping Line, na ina uwezo wa kubeba magari 9,000.
Mpaka sasa jumla ya magari yaliyopokelewa bandarini hapo yamefikia zaidi ya 4,200.
Magari hayo yatahifadhiwa katika maghala ya bandari.
Bandari ya Lamu inatarajia kupokea meli zaidi zitakazobadili mwelekeo wao, kwani mawakala kadhaa wa usafirishaji tayari wameanza kuulizia nafasi za kutia nanga. Kwa ujumla, shughuli za bandari zinatarajiwa kuongezeka kadri mwaka unavyoendelea.


Indonesia

@cooler1134180 @Collins071188 Wajinga hawa, Badala watafute kujihakikishia, ananiforce 😁
Indonesia

Kwa Mujibu wa Bloomberg,
India imepeleka meli za kivita za jeshi la wanamaji karibu na Mlango wa Hormuz ili kusindikiza meli zake za mafuta.
India inatuma zaidi ya nusu dazani ya meli za kivita kuelekea Ghuba ya Oman ili kuhakikisha usalama wa meli zake, ikitarajia kwamba Iran inaweza kuruhusu meli zake zaidi za mafuta kupita katika Mlango wa Hormuz.
Hivi karibuni, India ilifanikiwa kuhakikisha usafiri salama wa meli mbili za serikali zilizokuwa zikibeba gesi ya petroli iliyoyeyushwa (LPG), na kwa sasa inaendelea na mazungumzo na Iran ili kuruhusu meli nyingine zaidi za mafuta kupita.

Indonesia

@PolycarpMDM @ayubu_madenge Ni heri angekuwa padri awabatize Kwa moto
Indonesia

Kituo cha mafuta nchini Japani kimeweka bango wiki hii ambalo limeenea sana mtandaoni, Bango hilo linasema: "Samahani… hakuna petroli kwa sababu ya Trump."
Japan huagiza mafuta yake mengi kutoka Mashariki ya Kati kupitia mlango Bahari wa Hormuz.
Sasa Japani iko kwenye mgogoro wa mafuta. Bei ya mafuta imefika 190.9 yen kwa lita, kiwango cha juu zaidi kulinganisha miaka mingi ya nyuma. Serikali imetoa akiba ya kimkakati ili kuzuia vituo vya mafuta kuisha, lakini baadhi tayari vimeisha.

Filipino

🚨 Shambulio la anga la Israel limepiga jengo lililopo ndani ya eneo la mtambo wa nyuklia wa Bushehr nchini Iran, takriban mita 350 kutoka kwenye kinu cha nyuklia.
Kinu chenyewe hakikuharibika, na hakukuwa na uvujaji wa mionzi wala vifo vilivyoripotiwa.
International Atomic Energy Agency (IAEA) imethibitisha tukio hilo na kuonya kuwa linaweza kuvuka “mstari hatari zaidi” wa usalama wa nyuklia, huku Russia ikiilaani hatua hiyo kuwa “isiyo ya kuwajibika” kutokana na ukaribu wa kinu kinachofanya kazi na eneo lililopigwa na kombora pamoja na uwepo wa wafanyakazi eneo hilo.


Filipino

Utawala nchini Iran umewanyonga waandamanaji watatu walioandamana kupinga Utawala wa Kiislamu, Walikamatwa mwezi Januari kwa tuhuma hizo.
Majina yao ni;
• Saleh Mohammadi
• Saeed Davoodi
• Mehdi Ghasemi
Vyanzo vingi vinadai Walihukumiwa kifo na kunyongwa baada ya kulazimishwa kukiri kosa kupitia mateso, kunyimwa fursa ya kupata mawakili huru, na bila kuzingatia hata kanuni za msingi za haki na utaratibu wa kisheria.

Indonesia

Jasusi na Kamanda mwandamizi wa Hamas aliuawa katika shambulio la Israel Defense Forces katika Ukanda wa Gaza Strip hapo jana.
Jeshi la Israel (IDF) linasema kuwa shambulio hilo lilimuua Muhammed Abu Shaleh, afisa wa ujasusi wa kikosi cha Hamas cha Khan Younis.
Inadaiwa kuwa Shaleh alihusika katika kupanga shambulio la tarehe 7 Oktoba ndani ya Israel.
Indonesia

Picha mpya imetolewa, Ni yule aliyefanya shambulio katika sinagogi la Michigan, Anaitwa Ayman Mohamad Ghazali.
Alimtumia dada yake nchini Lebanon picha hiyo kabla ya shambulio, akiandika caption “kufa kishujaa” ili kulipiza kisasi baada ya shambulio la anga la Israel kumuua kaka yake (kamanda wa Hezbollah).
Ghazali alihamia Marekani kisheria mwaka 2011.

Filipino


















