
ASANTE KWA UPENDO WENU RUVUMA! 🙌 Shukrani za dhati kwa wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (@ccm_tanzania) mliojitoa kwa moyo wa pekee kushiriki na kushuhudia mikutano ya kampeni ya Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM, Mhe. Dkt. @SuluhuSamia, katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Ruvuma. Muitikio wenu wa kishindo umeandika ukurasa mpya wa mshikamano na imani ya kweli katika safari ya maendeleo ya taifa letu. Safari ya Ushindi inaendelea kwa nguvu mpya na matumaini makubwa kuelekea tarehe 29 Oktoba #DiraYaSamia #SamiaHadi2030 #HaijapataKutokea #KaziNaUtu2025












