

SIO “SHEIKH UBWABWA” TU, HADI “PASTOR WALI” YUPO Tanzania ni nchi ya kipekee ambayo, ukiweka mbali Ukosefu wa HAKI, UTAWALA BORA na MAENDELEO YA WATU, tulifanikiwa kuepuka Maadui hawa wawili; UDINI na UKABILA. Hii imefanya tuwe na UTULIVU, ambao kwa mbali unaweza kudhani ni AMANI. Nimefurahia jinsi WENYE NCHI, wakiongozwa na GEN Z, wakivyofanikiwa KUZIMA upuuzi wa kutugawa KIDINI ulioletwa na “Low Brain Strategists” wa WATAWALA. Ingawa kweli kuna waliojificha nyuma ya Dini ya KIISLAMU nakutoa kauli CHAFU na CHOCHEZI, ni UKWELI usiopingika, wapo Viongozi wa KIKISTRO ambao walifanya hivyo pia. Tuwakatae wote kwa pamoja na tusisite kuwaita MANABII WA UONGO. BAKWATA inajulikana kujaa “Mashehe Ubwabwa” ndio maana wakadai “AMANI kwanza kabla ya HAKI”, ili wasaidie NARRATIVE ya WATAWALA. Uzuri WAISILAMU hawafuati Maneno ya Mashehe, bali Mafunzo ya MTUME MOHAMMAD (sallallahu 'alayhi wa sallam) na QUR’ANI TUKUFU ya MWENYEZI MUNGU( subhanah wa ta’ala). Baadhi ya majina ya ALLAH (SWT) ni “Al-Adl”, “Al-Hakam” na “Al-Muqsit” na yote yana dhima ya HAKI. Leo Shehe kapewa mlungula, anapotosha UMMA na kuongelea Vurugu badala ya kukemea Mauaji. Pia kuna WACHUNGAJI UBWAWA kama MWAPOSA na yule mwingine ZERUZERU. Mwamposa unatumika na ipo wazi; hadi Kanisani kwako walikuja. Eti “Maandamano yanaharibu Utukufu Wa Mungu”. YESU aliandamana kuingia Jerusalem, na pia alifanya Vurugu kwenye Hekalu pale watu walipozingua. Biblia takatifu inasema Mungu wetu ni Mungu wa HAKI. ZABURI 89:14 “Uadilifu na Haki ndio Msingi wa Ufalme wako”. Pastor gani unahubiri neno la bwana, na unajipa upofu wa kutetea wapigania Haki, ilihali Mungu ni wa Haki? Tanzania has been a safe haven of all religions & faiths, where people (even fake pastors) worship in harmony, unbothered. Ni UTAMADUNI wetu, na unalindwa na KATIBA. Na kiukweli, familia zetu nyingi ni za KRISLAMU! Pongezi kwa Mashehe na Makanisa yaliyosimama kwenye UKWELI na HAKI. Na Kwa GEN Z waliozima UPUUZI. UJUMBE kwa Mapasta na Mashehe Ubwabwa, kama tunavyosemaga ACT Wazalendo, “EPUKA USALITI, DHIBITI NJAA YAKO” The Leader

















