kamwene retweetledi
kamwene
57.8K posts

kamwene retweetledi

‼️Free Tundu Lissu!✊🏽‼️
Tundu Antiphas Mughwai Lissu alikamatwa Mbinga, Songea tarehe 9
Aprili 2025 na akashitakiwa kwa uhaini kwa sababu ya msimamo wake
kwamba kama hakutakuwa na mabadiliko ya sheria na mifumo ya
uchaguzi, hakutakuwa na uchaguzi.
Baada ya ukimya wa muda mrefu, kesi ya Lissu imeitwa mahakamani tarehe 11 Juni 2025. Tunasisitiza kwamba lazima Tundu Lissu aachiwe huru bila masharti yoyote. Tunadai pia watuhumiwa wengine wote wa tuhuma za kisiasa waachiwe huru na bila masharti.
Msimamo wa Lissu uko wazi, hakukuwa na uchaguzi Oktoba 2025. Lissu anadai kuundwa kwa Tume Huru ya Ukweli, Usuluhishi na Upatanishi yenye watu waadilifu, huru, na wasio na maslahi binafsi, ili kuchunguza matukio yote ya ukiukaji wa Katiba, utekaji, upotezaji, mateso na mauaji ya raia wa Tanganyika, Zanzibar kuanzia mwaka 2016 hadi 2026. Tume hii iwe na mamlaka kamili ya kufichua ukweli, kubaini wahusika, na kupendekeza hatua za kisheria na kiutawala zitakazorejesha imani ya wananchi kwa vyombo vya dola.
Harakati za kuhakikisha Lissu anaachiwa huru n jukumu la kila mmoja wetu. Kwa kipekee tunaelekeza wapiganaji wetu wa mstari wa mbele GenZ kwa kuendeleza mapambano katika ngazi zote na wakati wote ya kuhakikisha Lissu na wafungwa wengine wa kisiasa wanaachiwa huru bila
masharti. #FreeLissu ni sauti ya Watanganyika na tunawaonya wale wote
wanaojaribu kutweza damu za raia wa Tanganyika wasio na hatia
waliouawa kikatili wakiipambania Tanganyika tarehe 29 Oktoba 2025
kuacha mara moja kwani Lissu alisema No Reforms, No Election #NRNE
na huo ndio msimamo wa Watanganyika.
#FreeTunduLissu
#SamiaMustGo

Indonesia
kamwene retweetledi

Nani mwenye hekima amnyang'anye Kalamu Naibu msajili wa vyama vya Siasa?
Mimi siyo Muumini wa dhihaka na Matusi. Lakini hata kwa akili za kuvukia barabara tuu huwezi kunishawishi kwamba Kauli hii ni dhihaka.
Na wala siyo ya kashfa ,Tusi na haijavunja Sheria wala Maadili yeyote mbele ya watu wenye akili timamu.
Nimeshauri na ninarejea kushauri ile ofisi imeacha kazi zake za Msimgi na wamejitwika jukumu la udhibiti maoni.Nashauri tena kwa maslahi mapana ya Taifa ifutwe haraka.
BAK Mwabukusi.

Indonesia
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi

MAHAKAMA YA RUFAA KUSIKIKIZA KESI DHIDI YA MHE. LISSU, June 11,2026:
Mahakama ya Rufaa itasikiliza maombi ya Mkurugenzi wa mashitaka nchini dhidi ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mhe Tundu Antipas Lissu Alhamisi ya tarehe 11 June, 2026.
Haya ni yale maombi ya Jamhuri ambayo waliyapeleka baada ya Mahakama kuu kukubali pingamizi la Mhe Lissu dhidi ya maombi ya Serikali kuraka kuongeza maelezo ya nyongeza ya shahidi.
Jopo la Majaji 3 wa Mahakama ya Rufaa wamepangwa ambao ni, Mhe Mwalija, Mhe Jaji Muruke na Mhe Jaji Khamisi.
Hakikisha ujumbe huu umewafikia kwa wingi marafiki wa Demokrasia na Haki.
@ShundoGaston,
Mkurungenzi wa Sheria wa CHADEMA HQ

Indonesia
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi

VIDEO:
Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA)@bavicha_taifa , limeipiga chini kaulimbiu inayotumiwa na serikali na baadhi ya taasisi ya "Never Again" likitaja kauli hiyo kama propaganda na upotoshaji unaolenga kuficha uwajibikaji wa waliohusika na mauaji ya raia mnamo Oktoba 29 mwaka jana.
Msimamo huo umetolewa jijini Dodoma jana na Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa, Wakili Deogratius Mahinyila, wakati akisoma maazimio ya kikao cha Kamati Tendaji ya baraza hilo kilichodumu kwa siku tatu mkoani humo.
Wakili Mahinyila amebainisha kuwa vijana wa CHADEMA @ChademaTZ2 hawatakuwa tayari kuimba wimbo huo wa amani ya maneno, hadi pale uchunguzi huru wa kimataifa utakapofanyika ili kujua nani aliyefanya mauaji na nani aliyemtuma.
Indonesia
kamwene retweetledi

VIDEO:
Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) Taifa, limewaonya wanachama waliokihama chama hicho kwa matusi na kashfa hadharani, kuwa kama wanataka kurejea, lazima watumie kurasa na majukwaa yaleyale waliyoyatumia kukidhalilisha chama hicho kuomba radhi kwa Watanzania.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa, Wakili Deogratius Mahinyila, amesema Kamati Tendaji imepokea ripoti ya kuwepo kwa wimbi kubwa la watu wanaotaka kurudi, lakini akasisitiza kuwa baraza lake halitakubali chama kigeuzwe kuwa "kichaka cha kusafisha watu waliofanya siasa kuwa biashara."
Wakili Mahinyila ameeleza kuwa CHADEMA ni chama cha demokrasia na kinakaribisha kila mtu, lakini hakiko tayari kulea mbegu ya migogoro inayoweza kuvuruga mshikamano wa sasa wa chama kuelekea harakati kubwa za kitaifa.
Filipino
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi

🙄 Hivi Nyahoza unatuonaje?
Mmeambiwa msichukue hatua YOYOTE kuanzia tarehe 25 Mei - hii ni pamoja na kuzua kesi nyingine na kutishia kuifuta TENA !
Usituone wajinga!
Na hizi barua mbona unaandika wewe na unatoa ufafanuzi wewe!?? Msajili yuko wapi?
CLEARLY unatumwa na Abdul kweli nje ya utaratibu rasmi! Ila elewa hamuwezi kuendesha parallel state! Fuateni sheria na utaratibu na kaa pembeni! Abdul atafute pa kuishi hii nchi si yake na mama yake!
#TutaelewanaTu #SamiaMustGo

Suomi
kamwene retweetledi

Moja kati ya mambo mengi mazuri yanayonivutia @ChademaTZ2 ni pamoja na fursa pana inayotoa kuwajengea uwezo wanawake kisiasa na kiongozi ili kutuwezesha kutoa mchango wetu katika kuleta mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli ndani ya Taifa letu.
#KatibaMpyaFreeLissu ✌️




Indonesia
kamwene retweetledi
kamwene retweetledi

"Hata askari haruhusiwi kutekeleza amri isiyo halali ambayo inapelekea kukinzana na katiba" Jaji Mstaafu Prof. John Ruhangisa.
Amesema hayo wakati wa mahojiano maalum ya kipindi cha #KatibaKitaa jijini Arusha.
Kutazama mahojiano kamili tembelea Youtube ya Wakili TV.
Indonesia
kamwene retweetledi

‼️🚨Msajili wa Vyama vya Siasa
Anapanga Mauaji Mengine ya
Watanganyika!‼️
Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi na Msaidizi wake Sisty Nyahoza wameibuka wakiratibu mauaji mengine. Pamoja na kushindwa kesi mahakamani, bado Msajili ameendelea kuratibu mikakati ya kufuta Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Kwa muda mrefu Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imekuwa kitovu
cha kuchochea vurugu na mauaji ya Watanganyika nchini Tanzania. Bila
kuheshimu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayowapa raia
haki ya uhuru wa kushiriki mikutano ya kisiasa, Jaji Mutungi na mwenzake Sisty Nyahoza wamekuwa wanaendesha mipango miovu dhidi ya raia wa Tanganyika kwa takribani miongo miwili sasa.
Hukumu ya Jaji Mugeta ya tarehe 25 Mei 2026 iliweka wazi na kumzuia Msajili kuigusa CHADEMA kwa jambo lolote lile. Hii ina maana kwamba Ofisi ya Msajili ni ofisi iliyojitwalia mamlaka ambayo yako juu ya maamuzi ya mahakama. Suala hili ni ushahidi wa kukosekana kwa utawala wa sheria nchini hasa Tanganyika.
Hivyo basi tunamtaka Msajili kuacha mara moja kuleta vurugu za kisiasa
na tunadai kwa sauti moja kufutwa kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na kuandikwa upya kwa sheria ya vyama vya siasa itakayolenga kuimarisha demokrasia.

Indonesia









