




Reema-MinjBen@MinjBenReema
37.3K posts

@RMinjben
BiTtER ThAn Leaf











TCRA Yasitisha Leseni ya Jambo TV Kwa Siku 90 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetangaza kusitisha kwa muda wa siku tisini leseni la chombo maarufu cha Habari Tanzania, Jambo Online TV kwa madai ya kuchapisha, "maudhui ambayo hawakuwa na uhakika nayo na yasiyo na uthibitisho". Katika taarifa yake TCRA inaeleza kuwa maudhui hayo yaliupotosha umma kuhusu hali ya matukio mbalimbali yanayoendelea nchini na matokeo yanayotarajiwa kutoka kwa Tume ya kuchunguza matukio wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. Maudhui yanayoelezwa ni makala ya maoni iliyochapishwa katika chombo hicho na mwandishi mkongwe, Manyerere Jackton yenye kichwa cha habari, Ripoti ya Jaji Chande ndiyo ya, ama kuliponya au kuliua Taifa. Katika Makala hiyo Manyerere amesisitiza juu ya uwajibikaji. Taarifa ya TCRA imeeleza kuwa leseni za Jambo Online TV zimesitishwa kuanzia Aprili 02, 2026. Taarifa hiyo imeeleza: "Aidha, katika kipindi kifupi cha takribani miezi sita sasa, yaani tangu mwezi Septemba 2025, Jambo Online TV imekuwa na mashauri manne mfululizo ya ukiukaji wa Sheria, Kanuni, Masharti ya Leseni, Maadili, Misingi na Taaluma ya Uandishi na Utangazaji wa Habari." Mnamo Septemba 06, 2025, TCRA pia ilisitisha leseni ya Jamii Forums kwa kipindi cha siku tisini.
















All buses, trains, and trams are free in this country. For everyone! Luxembourg is unreal. When will your country have this?
