
Leo nimeshiriki katika harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo cha watoto wenye mahitaji maalum cha Bagamoyo Diaconic Lutheran Centre kinachojengwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT).
Katika harambee hiyo iliyoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Benki ya CRDB na kampuni zake tanzu pamoja na mimi na familia yangu tumetoa ahadi ya jumla ya Shilingi Milioni 220 kusaidia ujenzi wa kituo hiko.
Kipekee sana nimshukuru Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Askofu Dkt. Alex Gehaz Malasusa kwa kutupa heshima ya kushiriki baraka hii kwa watoto hawa ambao wanahitaji kutazamwa kwa jicho la kipekee.




Indonesia



















































