@godbless_lema Mimi ninaomba mnaomzungumzia @zittokabwe mwachane naye,
Hapaswi kujadiliwa bali apuuzwe na kunyimwa ushirikiano wowote,
Ilisjajulikana njia na tabia yake,
Mkalieni kimya apotee
Siasa ya ukombozi ni harakati takatifu ya kupigania haki, utu na uhuru wa watu. Haipaswi kabisa kubadilishwa kuwa biashara ya udalali au njia ya kujinufaisha binafsi. Ndani yake kuna maumivu, vifo, na mateso ya kweli ya wapigania haki. Ni jambo la kusikitisha kuona watu wanaojitokeza leo wakitafuta uhalali wa kisiasa tena, ilhali jana walishirikiana na watesi na wakatili. Ushirikiano huo hauwezi kufutwa kwa maneno matamu , kwani ni doa katika historia ya ukombozi.
Mtu yeyote ambaye hakusimama upande wa haki wakati ulipohitajika, bali akajitahidi kuzima sauti za waonewa, ni mtesaji na muuaji kama wale tunaowalaumu leo. Sasa wanarudi kwa mbinu mpya kama “drones” zinazojaribu kutua kwa ujanja lakini ukweli unabaki pale pale, hawa ni wanafiki wanaojificha nyuma ya kivuli cha siasa.
Ukombozi wa kweli hauwezi kuletwa na walafi wa mamlaka, bali na watu waaminifu kwa misingi ya haki, uadilifu, utu wa mwanadamu. Tunapaswa kukemea tabia hizi, kwani hii haipaswi kuwa tabia ya Nchi yetu na watu wake.
Kaka @zittokabwe habari za siku mbili tatu?
Tangu baada ya ‘uchafuzi wenu’ umepoa sana arifee. Unachungulia TL kama unaaga maiti vile. Hata kutoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu, jamaa na marafiki umeshindwa? Njoo tujadiliane mlivyolinda kura.
Pole pia kwako kwa kukamatwa na kutunzwa mahabusu kwa vurugu za baada ya kushindwa huko Kigoma Mjini. Pole kwa wafuasi wako wote waliopewa kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kuchoma moto.
Vipi, umefanikiwa kumuona BABA LEVO akiapishwa kuwa mbunge wa Kigoma Mjini? Umeona anatamba kwamba ameangusha mbuyu? CHAWA grade one amekushinda? Amekustaafisha kiroho mbaya.
Tulikueleza ukasema muhuni hasusiwi. Tukakuuliza kivipiii? Ukakaza shingo na kusema piga kura, linda kura. Tulijua, huo ni udalali. Kiko wapi sasa? Hadi kesi mmepewa. Umetumika kuhalalisha uchafuzi haramu.
Anyways, hujachelewa sana braza. Kuna dili la maridhiano feki linazunguka. Bado halijapata expert. Unaweza kuchumpa na kuishi nalo. Biashara ya ubunge imekufa kifo cha mende. Pole sana BLO’ angu.
YESU aliingia Yerusalemu kwa Maandamano huku wananchi wakimshangilia na kuimba Hosana ajaye kwa jina la Bwana. Mafarisayo walikwazwa sana na ile Nyomi🤣( Kwasababu ya wivu na uovu wao) lakini Mungu wala hakukwazwa.
Ila Biblia yangu inanionesha Mungu alikwazwa na Kaini kumwaga Damu ya nduguye Abeli .Uuwaji ndiyo unaoondoa utukufu wa Mungu wa Mbinguni siyo maandamano.
Hata Yeriko Iliangushwa kwa Maandamano watu walizunguka mara saba.
Baba Askofu Kalikawe Lwakalinda Bagonza SIYO PIGO KWA Tundu A. M. Lissu ! Tumepigwa Wote.
Nimesikia baadhi ya watu wanasema Tundu Lisu amepata pigo mahakamani baada ya mahakama kuamua kwamba mashahidi watakaotoa ushahidi katika kesi ya uhaini, watakuwa wa siri. Yeye hatawajua na umma hautawajua, hautawaona, na hata familia zao hazitajulikana. Hili Si pigo kwa Lisu. Ni pigo kwa mahakama na pigo kwa haki. Zingatia.
1. Tunazo mahakama tatu: Mhimili wa dola, mahakama ya umma na ya Mwenyezi Mungu. Hii ya mwisho haina rufaa na ndiyo pekee yenye mashahidi wa siri. Jaji ni Mwenyezi Mungu. Uamuzi wa leo unaigeuza mahakama ya dola kuwa ya Mungu. Haikubaliki.
2. Serikali iliyotaka kupinduliwa ni yetu wananchi. Si ya Rais wala chama. Umma una haki kuwajua na kuwahoji mashahidi waliotusaidia kuzuia serikali yetu isipinduliwe na huyu mhaini. Kuwaficha mashahidi ni kuwanyima haki ya kutambuliwa uzalendo wao.
3. Uhaini ni kosa kubwa (high crime). Mahakama huendesha kesi hizi kwa wazi na kuwaadhibu wakosaji kwa wazi ili kutoa fundisho kwa wengine. Leo tunaficha mashahidi, kuna siku tutaficha wahaini na kuwanyonga mafichoni. Haiwezekani kuipindua serikali sirini. Aliyeshauri mashahidi wa kesi hii wawe siri afutiwe matokeo ya elimu yake. Sina tatizo na Jaji aliyekubaliana na ushauri huu. Kuna kupigwa upofu feki unaoitwa “maelekezo toka kinyume cha chini”.
4. Mtuhumiwa wa uhaini ana haki zake. Moja ni kuwajua wanaomshtaki (ambao ni sisi Jamhuri), na kuwajua wanaoshuhudia uhaini wake. Kwa kuwa ni mtuhumiwa na kwa msingi wa uamuzi wa kulinda mashahidi, hata yeye angefichwa tusimjue ili ikitokea akashinda kesi, tusiendelee kumwona na kumnyanyapaa kuwa ni mhaini. Tungemwona tu baada ya kuhukukiwa. Kwa kuwa tunamjua mtuhumiwa, tuwajue mashahidi.
5. Kuingiza au kuonekana unaingiza mizengwe mahakamani ni kuifanyia uhaini mahakama yetu. Mtu mmoja aitwaye Tundu Lisu asifanywe kuwa ana nguvu na umuhimu wa kulazimisha mahakama yetu inajisiwe. Mahakama ina wajibu wa kuitetea heshima yake. Umma una haki ya kutetea uhuru wa mahakama.
6. Kutumia siasa kutatua masuala ya kisheria au kutumia sheria kutatua masuala ya kisiasa ni kufanya uchochezi na kuchonganisha siasa na sheria. Katika mwaka wa uchaguzi, ni kuwachagulia wananchi viongozi kinyume na matakwa yao. Tunaandaa uongozi wa kutawala miili badala ya mioyo. Kuna watu wengi saaana wako tayari kumchagua Rais Samia akiwa na mpinzani kuliko akiwa peke yake.
7. Yanayoonekana kupitia chaguzi ndani ya vyama ni kielelezo halisi cha hali ya nchi yetu. Huu si uchaguzi, si uchafuzi, ni urasmishaji wa rushwa katika taifa letu. Baada ya kupata viongozi kupitia mtindo huu, hatuwezi kupata kiongozi wa kupambana na rushwa. Wapi hapajafikiwa na rushwa katika taifa letu?!
8. Tuliwahi kuwa na gaidi feki. Ikiwa tumeruhusu mashahidi wawe siri
na ushahidi uwe siri, basi tutakuwa na mhaini feki. Pia tunaye kijiweni msaliti feki anayedaiwa ni mchanga katika chama chetu “kinachochukia” rushwa. Ufeki
huu utatufanya tuone kila kitu ni feki. Nimeishaitwa Askofu feki.
Hukumu hii inasisitiza TURUDI MEZANI. Mahakamani hakuna msaada.
@KumbushoDawson Huyo Dr. Mie simwelewagi kwa kweli, Sijui alipitaje hata hizo awamu 2.
Hii drama ya mke wake ni ya kuomba kura za huruma na wajumbe wameshakula chao
Mgombea Ubunge Jimbo la Siha ambaye pia ni naibu waziri wa Afya, Godwin Mollel anadai Mke wake ametekwa na kupigwa kisha kupatikana baadaye. Godwin ameviambia vyombo vya habari kwamba gari lake limechomwa kituo cha polisi.
Ajabu ni kwamba anawapongeza polisi kwa kazi nzuri😂.
Wameshajua hana kesi, ni kichomi kwao akiwa huru. Watamwacha huru baada ya uchaguzi. Bahati nzuri sana hatokei mikoa ya mpakani, wangeshasema sio raia.
Kuna Msemo wa English “All bark no bite” (kubwekwa kwingi kung’ata huwezi).
Kwa miezi 3 Mahakama inatoa AMRI kila wiki 2 Serikali ikamilishe upelelezi. AMRI haitekelezwi. Mahakama inamrejesha mtuhumiwa RUMANDE!
Katiba imeipa Mahakama meno.
Swali:
Nani kaitoa MENO Mahakama?
Nina hakika ukimnyanyua mmoja kati ya hawa, ikiwemo huyu anayeongea, na kumuuliza katika miaka minne ya Rais @SuluhuSamia madarakani, ni ajira ngapi zimetengenezwa kwenye kada unayoisomea? Hawezi kujibu.
Nawaonea huruma sana wadogo zetu, laiti wangejua!
Tangu saa sita usiku polisi wamezingira Nyumbani kwa mhe Lissu, wamejaribu kutaka kuingia ndani, lakini ndugu wamewambia kama wanataka kufanya ukaguzi lazima mwenye nyumba awepo.
TAARIFA KWA UMMA:
Mheshimiwa Rais (Mst.) @jmkikwete ndiye MTU PEKEE DUNIANI ambaye alifanikiwa “KUMDHIBITI” Mheshimiwa TUNDU LISSU kwa HAKI na HOJA. Alitumia FALSAFA ya “HOJA HAIPIGWI RUNGU”. Tumpe 💐🌹🌷 yake Mheshimiwa KIKWETE.
@Mwabuk2Boniface Asante na Hongereni sana kwa kazi kubwa hii,
Saidieni Mataifa yetu haya.
Bado tunaimba demokrasia mdomoni.
Mungu awatumze na kuwainua zaidi.
Ongezeni nguvu na facts mmwokoe mpinganaji @TunduALissu
Jumuiya za Kimataifa na Kikanda za vyama vya Wanasheria zatoa Tamko kuhusu suala la kukamatwa na kushikiliwa kwa Wakili Tundu Lissu .
Suala la Tundu Lisu kufanyiwa dhuluma katika haki zake za Kujumuika na kutendewa kinyume cha sheria halikubaliki na hakuvumiliki. Kukamatwa kwake, kushtakiwa kwake na kuendelewa kuzuiwa ni shambulio dhidi ya demokrasia.
#FreeTun
@Mwabuk2Boniface Likabaki wazi kumaanisha kwamba chama kiliweza kusimama tena na uwezekano wa kufa ulitoweka. Hii ya sasa inamaanisha mgogoro umerejea CDM na kaburi limeanza kufukuliwa upya kwasababu wa kuzikwa kapatikana (CDM inakufa). NB: Kuna shati la kijani pembeni kumaanisha mzikaji ni CCM.
The voice of 1970s
Wana wa nchi leo wanapigania Matumbo yao,
Urafi wa madaraka, Rushwa
Unafiki na Usaliti kwa wananchi wao,
Wamekosa mistari ya kusimamia bali wanasimamia Matumbo na familiya zao.
Pumzika kwa amani Mzee wetu,
Mzalendo na Simba wa Mageuzi🇹🇿
Team Mwamba Wanapambana Sana hawajakubali yaliyotokea. Now wapo Tayari chama kife kwa hii story ya mpasuko kwenye chama. But naamini @TunduALissu na viongozi wenzake Wapo strong na wanajua namna ya kulimaliza hili.
Ili Chama Kisonge mbele.
Hii project ina pesa nyingi, wachache wanaoingoza kwa nyuma ni wanufaika wazuri sana pamoja na watu wao walioko upande wa pili. Kuna watu wanaletwa mbele kama bidhaa hawajui kama wanageuzwa bidhaa.Bungeni inajulikana kama Pandisha Presha. Kuna watu wanatajirika kupitia mradi huu na wengine ni bidhaa tu. Wakijua watakuja kukiri na kuomba msamaha kwa machozi ya damu. Nitanyoosha rula, yaliofanyika darini yatawekwa hadharani.
Mheshimiwa TUNDU LISSU ndiye MBUNGE WA KWANZA DUNIANI kuingia BUNGENI na VITABU VINGI na KUVITUMIA VYOTE kujenga HOJA ZAKE. Kumshinda LISSU kwa HOJA, ni LAZIMA uwe UMESOMA SANA, au vinginevyo, TUMIA ile 7 Septemba 2017, lakini hata hivyo, MUNGU ATAMLINDA.