Mwenye ile video ya Zitto Kabwe akiwahakikishia CCm kuwa wasijali hakuna maandamano yatatokea kwenye uchaguzi sababu kuna kimoja tu Tanzania kinachoweza kuitishisha maandamano na chama hiko ni ACt na wao wanashiriki uchaguzi. Naomba nitumie hiyo video WhatsApp +1 424 537 3057
@zittokabwe Mnataka umoja gani, mliombwa msishirki uchaguzi wa kihuni ili kuupunguzia nguvu, mkagoma. Sasa mnataka umoja na nani? Mko vyama 17 mliokubali kushiriki uchaguzi, unganeni na muwaiganishe wananchi kuuamgusha huo utawala. Cdm msikubali hizi ghiliba za Zito maana amekosa atakacho.
Historia inaonesha kwamba hakuna mfumo kandamizi unaoanguka kwa sababu ya malalamiko yaliyotawanyika ya wale wanaokandamizwa. thechanzo.com/2026/05/17/mkw…
@HecheJohn Huko mnakopita kama inawezekana pandisheni wananchi kadhaa kutoa ushuhuda wa mauaji ya 29 October. Na msikubali chochote kuhusu maridhiano ya hadaa, na wahausika wote ikiwemo rais watajwe bila hofu.
Siku ya pili oparesheni #freetundulissukatibampya tutafika kila kona ya Nchi..
Endelea kuchangia mabadiliko kupitia 0744446969 Chadema HQ
Asante sana Geita.
Viwanja vya Nyankumbu, Geita Mjini vimeongea! Zaidi ya TZS 2,559,000 zimepatikana kupitia #ToneTone. MaCCM hayataki kuamini kwamba chama cha siasa ambacho ni mali ya umma Tanzania ni CHADEMA. Angusha TONE lako hapo kupitia 0744446969; Jina - CHADEMA HQ. #PeoplesPower. 👊🏾
@BrendaRupia@HecheJohn@YerickoNyerereT anaweza kuzirai kwa hiki anachokiona. Kama anaamani Chauma inakubalika hivyo, waitishi mikutano wapime nguvu yao kwa umma.
Geita mmetisha sana! Asanteni sana kwa mapokezi yenu makubwa na ya kihistoria. CHADEMA tunawashukuru kwa kujitokeza na mioyo yenu ya kujitolea na michango yenu ya ton tone ,hakika mchango yenu ina nguvu kubwa katika mapambano haya. Mwenyezi Mungu aendelee kuwabariki sana.
Kesho tunaelekea Kahama kuendeleza mapambano ya kudai haki, demokrasia ya kweli, uhuru wa kweli kwa Watanzania wote na mwisho lakini sio kwa umuhimu uwajibikaji wa waliotoa order ya shoot to kill Oktoba 29.
CHADEMA NI 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
#KatibaMpyaNiSasa#FreeTunduLissu#TunawatuTutashinda
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tanzania Bara, John Heche, ametangaza mikakati mazito ya kukiamsha chama hicho nchi nzima ikiwa ni pamoja na kujiandaa kuitisha maandamano makubwa ya kihistoria ili kushinikiza kuachiwa kwa Mwenyekiti wao, Tundu Lissu, na kupatikana kwa Katiba Mpya.
Heche ametoa msimamo huo leo Mei 17, 2026, mjini Geita wakati akihutubia mamia ya wananchi kwenye mkutano wa operesheni ya chama hicho, ambapo amewataka viongozi kuanzia ngazi ya Kanda hadi Kata kuwafuata wananchi majumbani mwao kwa ajili ya kusajili wanachama wapya.
Mwanasiasa huyo amewataka Watanzania kuweka agano thabiti na CHADEMA kama wanavyoweka agano kwenye klabu za Simba na Yanga, huku akisisitiza kuwa nguvu ya mabadiliko ipo kwenye idadi ya watu (namba) watakaokuwa tayari kukipigania chama hicho.
"Tunataka kuwa wengi, kila mtu ambaye hana kadi ya chama kachukue kadi na uweke agano... Watanzania wekeni agano na CHADEMA kwamba hiki ni chama chetu tutakipigania mpaka tone la mwisho la damu yetu,” amesema Heche.
Akizungumzia hofu ya maandamano nchini, Heche ameshangazwa na hatua ya baadhi ya watu kudhani kuwa maandamano ni uhaini, akibainisha kuwa CHADEMA imeshafanya maandamano mengi ya amani mikoa mbalimbali kama Mwanza, Arusha, na Geita bila kuleta madhara yoyote.
“Kila ukitaja maandamano tumbo linawakata, wanafikiri maandamano ni uhaini. CHADEMA imeshafanya maandamano kibao kwenye nchi hii hata nzi hakufa... Sisi maandamano tutakayoyafanya ni yatakayofuata sheria zote na taratibu, lakini yatakuwa makubwa hayajawahi kutokea nchi hii na yatakuwa na matokeo tunayoyahitaji,” amesisitiza.
Heche amehitimisha kwa kuweka wazi kuwa maandamano hayo yanalenga kushinikiza mamlaka kumuachia huru Mwenyekiti Tundu Lissu, kuleta Katiba Mpya, na kutekeleza mambo yote ya msingi ambayo wananchi wanayahitaji kwa ustawi wa nchi yao.
@zittokabwe Na hivi vyombo vya ulinzi vinaingizwa kwenye siasa kupitia madaraka ya rais. Ni lazima madaraka ya rais kwa vyombo vya ulinzi na usalama yadhibitiwe. Wakati wa Magufuli na sasa kwa Samia vyombo vya dola vimetumika wazi wazi kuharibu demokrasia yetu kwa maslahi ya ccm.
Hatua ya muhimu kabisa kuokoa Taifa letu ni kuviondoa vyombo vya Ulinzi na Usalama kutoka kwenye Siasa. Ushiriki wa TISS katika siasa na haswa siasa za vyama ndio kumepelekea nchi yetu kuingia kwenye mkwamo na kusababisha mauaji ya raia. Ni lazima kuendesha kampeni mahususi ya kuviondoa vyombo vya dola kutoka kwenye Siasa zetu
Mahakamani shaidi hudodoshwa ili kumcondradict na ushaidi wake na mwisho kumpotezea credibility.
Story ya Hilda sitaki kuisema kuwa yote ni ya ukweli au yote ni uongo. Nitakuwa nagusa maeneo maalumu tu.
1. HILDA: Buyobe alimdanganya Mshabaha kwamba Msuya alikuwa Diwani wa Chadema wa Ubungo huku akijua
fika kwamba Msuya hajawai kuwa Diwani.
FACT: Si kweli nilidai Msuya alikuwa diwani Ubungo. Ili limepindishwa makusudi kimkakati. Nilimtambulisha Msuya kama aliyewahi kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Ubungo Msewe.
2. HILDA: Mshabaha alimuliza ndani ya CHADEMA anamfahamu nani Buyobe akasema @ExMayorUbungo na Hilda Newton kama girlfriend wake japo kwasasa Msuya hana mahusiano mazuri na Bony.
FACT: Sikuwahi kutaka kwa njia yoyote kumtumia Bonny kutia ushawishi ili Msuya aaminike. Sijisikii vizuri kumjadili hapa Bony kwani nitakuwa namuingiza kwenye issue isiyomuhusu. But ni kweli tukiwa kwenye maongezi ni Msuya mwenyewe alieleza juu ya ukaribu wake na Bony very casually. Pia ni kweli Msuya alitueleza mimi na Mshabaha kuwa Hilda alikuwa girlfriend wake. Hapa ukakasi ninaoupata, Hilda kwa nini anataka kujitenga na Msuya kwa kukana kutomjua. Lets say inawezekana hawakuwa na mahusiano, vipi ashindwe kumtambua Msuya kama mwenyekiti wa mtaaa maarufu kama Msewe, ambao wakati ule ulikuwa ni kama kambi ya wasomi wengi wa UDSM
NB: Nitaomba nisaidiwe, Msuya alitueleza alikuwa mwenyekiti wa wenyeviti mkoa wa kichama Ubungo. Kama ni kweli, Hilda bado anashindwa kumtambua kiongozi wake huyu chamani?
3. HILDA: Nilimpigia simu Buyobe, nikamuuliza kwanin alimdanganya Mshabaha kwamba mimi ni Girlfriend wa Msuya wakati anajua mimi na Msuya hata hatufahamiani, alijiumauma sana mwisho akajitetea kwamba Msuya alimdanganya.
FACT: Sijawahi kuulizwa na HILDA juu ya taarifa za Msuya kudai wana mahusiano. Nazidi kutia mashaka kwa nini hapa kwenye Mahusiano anaparejea hadi kutoa ushuuda wa uongo. The fact ni kwamba Hilda anamjua Msuya inawezekana sio kama mpenzi wake. Kumkana kutomjua Msuya hadi kutotambua nafasi yake ya uongozi chamani inaweza kutoa strong suspicion ya inawezekana wanajuana zaidi tujuavyo. Ni issues ndogo but yenye trustworthy issues.
HILDA: Msuya baada ya kupiga tukio jioni ya siku hiyo hiyo, alionekana maeneo ya Namanga akivuka kuelekea Dar wakati huo Buyobe yeye alikimbilia maeneo ya Busia (Hii ni kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe) na hapo alifanya bila kuwasiliana na mtu yeyote hata wale waliompokea hakuwajulisha, licha ya kwamba awali wakati anafika alisema haijui kabisa Kenya ni mara yake ya kwanza kufika Kenya.
FACT: Sikujiondokia bila taarifa. Mtu nisiyetaka kumuingiza kwenye mjadala kwa kuwa hausiki, tuliwasiliana naye. Nilipigiwa simu ya Mshabaha, huyu mtu mwingine wakiwa na nia ya kutaka kunibrief kilichotokea. Nilikuwa nimelala hotelini sikusikia simu zao.
Majira ya kwenda saa 11 nikampata Mshabaha na akanijuza kilichotokea na yupo hospital. Mshabaha pamoja na madhira yaliyompata, hakusahau his duty of care kwangu. Ni yeye akashauri niondoke haraka pale hotelini hadi itakapothibitika kuna usalama.
HILDA: Azizi na Msuya walikuwa wakiishi na mimi
FACT: Huu ni uongo! Msuya alikuwa anakaa Himalaya Heights, mimi nilikuwa ninakaa Myra residence
HILDA: Msuya alipoona Mshabaha amekataa mambo yatraining akamuomba amkutanishe na Hilda, Maria, Sativa, na Mwaipaya. Mshabaha alikataa mind you huyu mtu ambae anamuomba Mshabaha
amkutanishe na mimi, kwenye utambulisho wake alisema kwamba mimi ni girlfriend wake.
FACT: Hapa Hilda anajichanganya kwenye Dodoso la Pili (2. HILDA) Anasema kuwa mimi nilimtambulisha Msuya kuwa wanahusiano naye wa kimapenzi. Lakini Msuya akamkataza Mshabaha asimpigie Hilda kwa kuwa Msuya anajua uongo wake utajulikana. Hapa anarudi kujicontradict kuwa Msuya baada ya kuwa desperate kwa kukataliwa kutoa training kwa wanaharakati akaomba akutanishwe na kina Hilda na wenzake. Yani Hilda aliyemkwepa asitafutwe kwa kuwa uongo wake utajulikana, sasa anamtafuta bila kuhofia uongo wake. Hilda na Msuya Kunani?