alinamdaj
5.1K posts











VIDEO: Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mwenyekiti wa Kamati ya Kusukuma Maridhiano Tanzania, Charles Odero, amesema ni muhimu kwa vyama vya siasa pamoja na Serikali kukaa meza moja ya mazungumzo kwa lengo la kulisogeza taifa mbele kimaendeleo na kuimarisha mshikamano wa kisiasa nchini. Akizungumza na Jambo TV, Odero amesema Chama cha CHADEMA hakitakiwi kuona ugumu wa kukutana na Serikali pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa ajili ya kufanya maridhiano licha ya changamoto mbalimbali zinazokikabili chama hicho. Amesema changamoto hizo ni pamoja na kukamatwa kwa viongozi wa chama, kushikiliwa kwa wanachama na wafuasi wake, pamoja na kushikiliwa gerezani kwa Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Tundu Lissu kwa tuhuma za uhaini, akisisitiza kuwa hali hiyo haiwezi kuwa kikwazo cha mazungumzo ya kisiasa. “Hata sasa pamoja na CHADEMA kuwa na kesi mahakamani, wafuasi wake mamia kuwa gerezani na Mwenyekiti Tundu Lissu kushikiliwa kwa kosa la uhaini, mambo yote hayo na maumivu makali hayawezi kumzuia John Heche kukutana, kupeana mkono na Rais Samia Suluhu Hassan, kwani katika mazungumzo suluhu haikosekani,” amesema Odero. Akisisitiza hoja yake, Odero ametolea mfano wa kipindi cha aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe ambaye alishikiliwa gerezani kwa tuhuma za ugaidi, ambapo aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, aliweza kukutana na Rais Samia Suluhu Hassan, mazungumzo ambayo yalifungua ukurasa mpya wa kisiasa nchini.





Kama Mama alishinda kwa 98% maana yake anaungwa mkono na Watanzania 98%. Kama ni hivyo mbona milio mingi kuhusu Wananchi kuwanyanyapaa Wasanii walioiunga mkono CCM ambao waliokaa kimya wakati jamii inashughulikiwa? Wanahangaika na 2%.?? Familia tuendelee kukaza hapo hapo, wanakaribia kusema Mama alipata ngapi.

















