Sabitlenmiş Tweet
Rahim Muro
19.3K posts

Rahim Muro
@muro_rahim
Allah is my guydens🙏🙏🙏 Kila hatua dua💪💯💯 Mbezi beach Africana📌📌 0710828084 na 0767 974074🇹🇿🇰🇪🇺🇬
Dar Esalaam(Africana kwa Zena) Katılım Kasım 2021
4.8K Takip Edilen5.7K Takipçiler

TANZIA: Mwanasiasa mkongwe William Vangimembe Lukuvi amefariki Dunia, asubuhi ya Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mshtuko wa moyo.
Taarifa ya msiba wa Lukuvi aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani imetangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka.
Lukuvi ambaye alizaliwa Agosti 15, 1955, alikuwa Bungeni kwa kipindi cha Saba ikiwa ni tangu Mwaka 1995 ulipofanyika Uchaguzi wa Mfumo wa Vyama Vingi nchini.
Zaidi jamii.app/RIPLukuvi
#JamiiForums #JFMatukio #RIPLukuvi

Indonesia

Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi (Mb.), aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, kilichotokea leo jijini Dodoma.
Tumepoteza kiongozi shupavu, mahiri, mwenye uzoefu mkubwa, mzalendo na mtumishi wa umma aliyelitumikia Taifa letu kwa uadilifu, weledi na kujitolea. Mchango wake mkubwa katika ujenzi na maendeleo ya Taifa letu utaendelea kuenziwa na kukumbukwa siku zote.
Ninatoa pole kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu, familia, wananchi wa Jimbo la Isimani, ndugu, jamaa na marafiki pamoja na Watanzania wote kwa msiba huu.
Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.
Amina.

Indonesia

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza kifo cha Mbunge wa Jimbo la Isimani na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), William Vangimembe Lukuvi, kilichotokea leo tarehe 25 Machi, 2026, majira ya saa moja asubuhi katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mshtuko wa Moyo.
Taarifa hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na kusainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt. Moses Kusiluka.
Marehemu Lukuvi alikuwa akihudumu kama Mbunge wa Isimani Mkoani Iringa na Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu wa shughuli za Serikali, pamoja na masuala ya watu wenye Ulemavu.
Rais Samia ametuma salamu za rambirambi kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Familia ya marehemu, Ndugu, Jamaa, Wananchi wa Jimbo la Isimani na Watanzania wote kwa ujumla.
#MillardAyoUPDATES

Indonesia

@BesteNicolas Ukiwa na hela utaitwa Mohammed ukiwa huna hela watakuita Mudi...😂😂😂😂
Indonesia

Africa has over 122,500 dollar millionaires, yet it still takes Mr Beast to step in and help in this situation.
The Mayor@themayor_ke
The saddest thing I have seen on the Internet today
English
































