Muha
12.3K posts



@swahilitimes wakati wazee ndio mnafuja Mali za hii nchi humuangali future ya. vijawana mnawaza nyie na matumbo tenu
Indonesia

Ninawatakia Watanzania wote heri ya Maadhimisho ya Miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Muungano wetu ni lulu na urithi wa kipekee tulioupokea kutoka kwa waasisi wetu. Hivyo, nasi tuna wajibu wa kuutunza, kuulinda, na kuuimarisha ili tuurithishe kwa vizazi vijavyo ukiwa salama na imara kama tulivyoupokea.
Ninatoa wito kwa Watanzania kuendelea kushirikiana, kufanya kazi kwa bidii, na kuimarisha uzalendo wetu, ili tujenge Tanzania moja, imara zaidi, yenye umoja na maendeleo jumuishi kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Ubariki Muungano wetu.

Indonesia

Mtaalamu wa maridhiano na utatuzi wa migogoro, Dkt. Dennis Mchunguzi, ameipongeza Tume ya Uchunguzi iliyoongozwa na Othman Chande kwa kazi kubwa iliyofanywa kwa muda wa siku 153, akieleza kuwa haikuwa kazi rahisi bali ilihitaji umakini, weledi na uzalendo wa hali ya juu.
Aidha, amempongeza Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wa kuunda tume hiyo, akisema hatua hiyo imeonyesha dhamira ya kweli ya kutafuta ukweli na kuimarisha misingi ya haki na amani nchini.
Akizungumza baada ya kuisikiliza ripoti hiyo kwa kina, Dkt. Mchunguzi amesema,
“Nikiwa mtaalam na msomi mbobezi wa maridhiano na ujenzi wa amani, naweza kusema wazi kuwa ripoti hii imeandikwa kwa utaalam mkubwa, ikifuata viwango vya juu vya kitaaluma na kutekeleza ipasavyo hadidu za rejea.”
Hata hivyo, ameeleza masikitiko yake juu ya madhara yaliyotokea kufuatia matukio ya vurugu ya Oktoba 29, ikiwemo kupotea kwa maisha ya Watanzania, majeruhi pamoja na uharibifu wa mali. Ameungana na Rais Samia kutoa pole kwa familia zilizoathirika na taifa kwa ujumla.
Kwa mujibu wa Dkt. Mchunguzi, ripoti hiyo ni nyenzo muhimu itakayosaidia taifa kusonga mbele kwa kujenga msingi wa haki, uwajibikaji na maridhiano ya kweli.
Akizungumzia hotuba ya Rais Samia wakati wa kupokea ripoti hiyo, alisisitiza kuwa msisitizo wake juu ya umoja wa kitaifa na mshikamano ni sahihi na wa wakati muafaka.
“Tunapaswa kuwa makini na maadui wasiolitakia mema taifa letu. Yaliyotokea yamelitia doa taifa, na hatupaswi kurudi huko tena,” amesisitiza.
Dkt. Mchunguzi pia alikaribisha msimamo wa Rais kuhusu kuanzishwa kwa mchakato wa maridhiano ya kitaifa, akibainisha kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuliponya taifa na kuweka msingi wa mabadiliko makubwa, ikiwemo kufikia Katiba Mpya.
Amefafanua kuwa kuchelewa kuanza kwa mchakato huo kulichangiwa na kusubiri ripoti ya tume, na sasa mapendekezo yaliyotolewa yatawezesha kuboresha na kuelekeza vyema hatua zinazofuata.
Aidha ametoa wito kwa Watanzania wote kuunga mkono juhudi za maridhiano.
“Tusipinge maridhiano, bali tuyakumbatie. Haya ndiyo yatakayotujenga upya kama taifa na kutupeleka katika hatua nyingine ya maendeleo. Kila mmoja anapaswa kuwa tayari kushiriki pale muda utakapofika.”
Ka
Indonesia

@MsigwaGerson Jeuri ya madaraka inakupa kiburi Cha kuwaita binadamu wenzako walioumbwa Kwa mfano wa Mungu unawaita nguchiro? Jitafakari uongozi unakuja na changamoto hizo positive msg zikutie moyo, matusi yapuuzie, mengine kama yana ukweli yafanyie kazi Mzee this is wrong
Indonesia

Kuna nguchiro wamechapisha namba yangu binafsi ya simu mitandaoni na kuanza kuhamasisha watu wanishambulie. Nataka kuwaambia huo ni upuuzi na ni uvunjaji wa Sheria.
Ukiondoa watu wachache sana wanatuma meseji za hovyo, asilimia 99 wananitumia meseji za kunitia moyo na kueleza utayari wao wa kuilinda nchi yao dhidi wenye nia ovu. Wale wanaoeleza changamoto za ajira na mitaji ninawapa majibu na nafikisha kwa wahusika zifanyiwe kazi.
Nguchiro na chawa wa nguchiro acheni kupoteza muda na rasilimali mkiporomosha matusi, tulieni na tuungane kujenga na kulinda nchi yetu.
Indonesia

Rais Samia Suluhu Hassan ameeleza namna alivyogoma awali kwenda kuzindua meli ya uvuvi baada ya kuambiwa na wasaidizi wake kuwa meli hiyo ni ndogo na haina hadhi ya kuzinduliwa na Rais.
Rais Samia ameyasema hayo leo Jumamosi, Aprili 25, 2026, katika hafla ya uzinduzi wa meli ya kwanza ya Serikali ya uvuvi wa bahari kuu ya Shirika la Uvuvi Tanzania (Tafico), iliyofanyika Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Indonesia

@MangiwaKwanza1 @msaliti_yu76041 Amina sana kaka hata Mimi naomba Mungu asinichukue nishuhudie anguko la wauaji
Indonesia

@millardayo Siku kanisa langu likisema Ile ripoti ya tume imeponya ndio ntakubali
Indonesia

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Sheikh Walid Alhad Omari, amesema Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Vurugu za Oktoba 29 imeleta matumaini kwa Watanzania kwa kuibua mambo muhimu ambayo wengi walikuwa wakiyatarajia, akieleza kuwa ripoti hiyo imefungua ukurasa wa kujenga taifa lenye mshikamano, haki na amani ya kudumu.
Akizungumza leo April 24, 2026 Jijini Dar es salaam, Shekh Walid amesema baada ya kutolewa kwa Ripoti hiyo, sasa ni wakati wa Viongozi wa Dini kubeba jukumu la kuyahubiri maudhui ya Ripoti hiyo kwa Waumini wao ili kusaidia kujenga uelewa, maridhiano na kuimarisha umoja wa kitaifa, akisisitiza kuwa Nyumba za Ibada zina nafasi muhimu katika kuhimiza maadili na kulinda amani ya Nchi.
Aidha, Sheikh Walid ameongeza kuwa utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na Tume hiyo unaweza kuwa msingi wa kujenga upya Tanzania imara zaidi, akitoa wito kwa Watanzania kuendelea kushirikiana kulinda amani na kutumia fursa hiyo kama mwanzo wa safari mpya ya maridhiano ya Kitaifa.
#MillardAyoUPDATES
Indonesia


@ze_mandevu @kilepi_tweve naogopa sana kutukana watumishi wa Mungu mnoo naogopa sana
Indonesia

Mtu anayesagwa maharage atatwambia nini sisi?🚮🚮
joseph_selasini@joeselasini
Uhuru na weledi ikatoka na uongo wa karne sio? Busara ni kudhibiti mdomo pale ambapo nafsi inapotaka kusemea jambo gumu.
Indonesia

Katibu Mkuu wa chana cha CHAUMMA na mgombea urais kupitia chama hicho kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2025, Ndugu Salum Mwalimu, amesema kuna watu kadiri tunavyo kuwa na misukosuko ndio maisha yao.
Aidha Mwalimu ameipongeza Tume kwa namna ya uwasilishaji wao na kuwapongeza kwa njia za uchunguzi walizo zitumia.
Indonesia

YALIPANGWA
YALIRATIBIWA
YALIFADHILIWA na
YALITEKELEZWA.
Eee Mwenyezi Mungu tusadie, tufumbue macho na tuongoze kutambua na kuwakataa wenye nia ovu dhidi ya Tanzania.
#NeverAgain
Indonesia














