
Mdau: We jamaa, Mungu aliumba ulimwengu na kila unachokiona, haikustaajabishi? Mimi: Hapana, ili nikimjua aliyemuumba huyo Mungu aliyeweza kuumba vyote hivi aisee nitastaajabu sana. Swali 1: Kwa nini hoja inaishia tu kwenye chanzo cha ulimwengu na kuhitimisha kuwa ni Mungu na sio chanzo cha huyo Mungu?? Tumesahau yale maswali ya Lawino kwenye Song of Lawino and Ocol? Lawino aliuliza, yeye Mungu alitoka wapi? Alikuwa wapi wakati anaumba ulimwengu? Akili au mawazo ya kuumba ulimwengu alitoa wapi? Swali 2: Tukishasema na kuamini CHANZO NI MUNGU au chochote, then what?🤔 Faida yake ni nini haswa kwenye maisha ya mwanadamu??








