固定されたツイート
Ally. Kombo
51.4K posts

Ally. Kombo
@Chikobe2000
Fearless on his thought, Sales and Distribution Guru
Arusha, Tanzania 参加日 Ocak 2012
224 フォロー中389 フォロワー

Kijana wa miaka 21, Sasan Azadvar Jongani kutoka mji wa Isfahan nchini Iran, ameuawa kwa kunyongwa baada ya kukamatwa akishiriki Maandamano ya kupinga Serikali.
Mahakama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema kuwa Sasan alihusika katika maandamano yaliyolenga kuipindua Serikali.
Inadaiwa kuwa alirusha mawe kwenye gari lililokuwa limewabeba maafisa wa Serikali, akavunja vioo vyake na pia kuwarushia mawe maafisa hao.
Mahakama hiyo pia inadai kuwa kabla ya kushiriki maandamano hayo, Sasan aliwaambia watu wa karibu naye kuwa angeingia barabarani kwa lengo la kuipindua Serikali, na aliwahamasisha marafiki zake kushiriki.
Hata hivyo, mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema haijulikani wazi jinsi alivyokamatwa, kama alipata wakili wa kumtetea na mazingira yaliyomfanya kukiri makosa hayo.
Siku ya Jumatano, Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, alisema kuwa tangu kuanza kwa maandamano nchini Iran, watu 21 wamehukumiwa kifo huku zaidi ya watu 4,000 wakikamatwa.
Aidha, Mashirika mawili ya haki za binadamu yalisema kuwa mwaka uliopita nchini Iran, watu 1,639 walinyongwa, ikiwa ni idadi kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa katika mwaka mmoja tangu 1989.
#KitengeUpdates

Indonesia

@mshambuliaji Mifumo hiyo ndiyo mnapenda,watu wakidai haki mnasema uasi ✌️✌️
Indonesia

@flahisha Ndo shetani alivyoamua kuishi nao.hata makahaba ,fuatilia
Indonesia

@Danny45405967 Mnafiki huyo !
Walipotoka kuvunja mali za watu na kuchoma Vituo vya Mafuta walitegemea nini kutoka kwa Serikali !?

@pastajoshuatz @ayubu_madenge Hujashangaa anaye wambwa msalabani !?
Indonesia

@ayubu_madenge Af kuna sisi mungu wetu tunampigania kwa igaidi wengine mungu wao alipigwa inch 6 msalaban yaan hii dunia bora uwe na nenge mda wote la sivo
Filipino

















