Sabitlenmiş Tweet

Mbinu 10 Za Haraka Za Usalama Kila Mtu Anapaswa Kujua:
1. Ukihisi harufu ya kitu chenye utamu ndani ya gari lako, simamisha kuendesha mara moja kwa sababu huenda kuna uvujaji wa betri au kimiminika cha kupozea injini (coolant).
2. Ukihisi kuna mtu anakufuata kwa kukufatilia fanya mizunguko minne ya kushoto, akiwa bado yuko nyuma yako, kuna uwezekano anakufuatilia.
3. Ukidondosha funguo zako ukiwa unafukuzwa, endelea kukimbia usisimame, utapoteza sekunde muhimu.
4. Daima weka viatu vyako karibu na kitanda majanga mengi hutokea usiku.
5. Mgeni akikuomba umsaidie kutafuta mnyama wake aliyepotea, usiende hii ni mbinu inayotumiwa mara nyingi kuvutia waathiriwa.
6. Ukikwama kwenye moshi, tembea kwa kujikokota chini hewa safi zaidi hubaki karibu na sakafu.
7. Usiache kinywaji chako bar bila uangalizi hata kwa sekunde moja.
8. Hisia aka Intuition zako zikikuambia usiende, ziamini.
9. Ukishikwa mkono kwenye kifundo, zungusha mkono wako kuelekea upande wa kidole gumba cha mshambuliaji hapo ndipo sehemu dhaifu zaidi.
10. Hakikisha simu yako ina chaji angalau 50% kabla ya kutoka nyumbani simu iliyozimika hukata mawasiliano ya msaada.
Chukua na hii...⤵️
Indonesia














