TECHNICIAN 🇹🇿
2.4K posts

TECHNICIAN 🇹🇿
@Avitusherman
Pharmaceutical personel 💊||Entrepreneur 🤵🏾♂️ || @Chelsea || @simbascTanzania ||Graphic designer 🎨


#TajiriLaKihaya Nimeangalia karibu kila mechi ya World Cup hadi sasa. Na kuna kitu nimekigundua… France ndio timu tishio zaidi kwenye mashindano haya. Watu wengi wanaangalia vipaji vyao, lakini kinachowafanya wawe hatari pamoja na majina makubwa walionayo … mfumo pia unachangia… France hawalazimishi kumiliki mpira. Wanakuruhusu uufurahie, halafu wanakusubiri ufanye kosa moja tu. Ukipoteza mpira sehemu mbaya, ndani ya sekunde chache unakuwa umefungwa. Hiyo ndiyo silaha yao kubwa: transitions na counter attacks. Kwa maoni yangu, kuna timu mbili tu ambazo zinaweza kuwadhibiti wakikutana nazo. 1. Spain 🇪🇸 Ingawa siwapendi (wanapenda kuwaweka wachezaji wetu wa Arsenal benchi 😂), lakini kisoka ni lazima niwape heshima. Spain wanacheza positional football. Short passes, movement ya hali ya juu na control ya tempo ya mchezo. Wanapoteza mpira mara chache sana, hivyo wanaipokonya France nafasi ya kutumia silaha yao kubwa ya counter attack. Kwa kifupi… France ni kama Real Madrid. Hawahitaji kutawala mchezo ili washinde. Spain ni kama Barcelona. Wanakunyima mpira, wanakuchosha na wanakuzuia kabisa usicheze mchezo wako. Ila barcelona inawapiga madrid mkono kila wakikutana na Mbappe wao🤣 MFUMO 2. England 🏴 Watu wengi wanawabeza, lakini England wana kila kitu cha kwenda sawa na France. Nguvu, kasi, depth ya kikosi, aerial threat na uwezo wa kushambulia kwa pande zote. Pia wanaweza kupress juu au kushuka chini kutegemeana na mchezo unavyotaka. Na kwa utani kidogo… France wanafanana na PSG. Lakini PSG wakikutana na Arsenal huwa hawaonekani wale wale. 😅 AKINA dembele walipigwa hadi Sub… bila Gabriel kupaisha penalty kombe lilikua letu lile😂 England wana wachezaji wengi wanaocheza pamoja Premier League, chemistry yao ni kubwa kuliko watu wanavyodhani. Kwa hiyo, kwangu mimi… 🥇 France bado ndio favorites. 🥈 Spain ndiye matchup mbaya zaidi kwao. 🥉 England ndiye timu inayoweza kuwapa vita ya kweli. Mpira hauna hesabu za moja kwa moja, lakini styles make fights. Si kila timu bora ndiyo inayoweza kuifunga timu bora zaidi. Wakati mwingine mfumo mmoja ndiyo unaua mfumo mwingine. Haya ni maoni yangu baada ya kuangalia karibu mechi zote za World Cup hadi sasa… Je, wewe unaona ni timu gani inaweza kuisimamisha France? Au unaamini hakuna wa kuwazuia mwaka huu?




















