BOB
18.1K posts









VIDEO: Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA @ChaummaT) kimeanza rasmi mchakato wa kuandika upya Katiba ya chama hicho, hatua inayotajwa kuchochea chama hicho kwenda sambamba na ukuaji wake huku dhamira ikiwa ni kuwa chama kikubwa zaidi kwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati Katibu Mkuu wa CHAUMMA Salum Mwalimu leo, Jumanne Machi 24.2026, amezindua rasmi Kamati mahsusi iliyopewa jukumu la kuandika Katiba Mpya ya chama hicho, kamati yenye Wajumbe 11 ikiongozwa na Mwenyekiti wake Benson Kigaila ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Tanzania Bara, Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa kamati hiyo, iliyofanyika kwenye ukumbi wa makao makuu wa CHAUMMA, Kinondoni, Jijini Dar es Salaam, Mwalimu amesema mchakato huo unapaswa kukamilika katika kipindi cha miezi sita (6) ikiwa ni utekelezaji wa vikao halali vya chama hicho kuanzia Mkutano Mkuu, Halmashauri Kuu na Kamati Kuu.




















