DON👁️🎯
4.3K posts



















#UPDATES_KESI_YA_UHAINI Part 187 Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi ASP Geofrey Lutufye. Mhe. Lissu: Mnajifanya mapolisi mnawasingizia watu vitu vya bure haya itakushangaza hao mliowakamata baada ya kesi yao kuisha ni mashahidi wa kesi hii? ASP Geofrey Lutufye : Hainishangazi. Mhe. Lissu: haikushangazi kwasababu huo ndio utaratibu wenu mapolisi wa Tanzania. Mhe. Lissu: Au unabisha nikufungulie ripoti ya Jaji Mkuu Othman Chande amesema mnawafungulia watu makosa ya uongo. Sasa nikuulize swali lingine, umewahi kuona video mimi nikiwa nazungumza habari za huo uchaguzi mkuu? ASP Geofrey Lutufye : amekaa kimya Mhe. Lissu: Unajua kwanini nimeshitakiwa kwa Uhaini ASP geofrey lutufye? Unajua sababu. ASP Geofrey Lutufye : Sababu ya ile kauli uliyotoa. Mhe. Lissu: Ipi hiyo? ASP Geofrey Lutufye : Ulisema utazuia uchaguzi wa mwaka 2025. Mhe. Lissu: Ndio nakuuliza uliiona hiyo video? ASP Geofrey Lutufye : Sikumbuki. Mhe. Lissu: Hawa ndio kesho watakuwa ma RPC siku inayofuata utashangaa anakuwa IGP, Sina maswali mengine Waheshimiwa majaji. Watu wanasonya tu hapa. Anasimama Wakili wa Serikali Renatus Mkude kwa ajili ya Re-examination Maelezo yako uliandika kama nani? ASP Geofrey Lutufye : Kama shahidi. Wakili: Unalizungumziaje kuhusu kujiandika mwenyewe? ASP Geofrey Lutufye : naweza kujiandika mwenyewe au kuandikwa. Renatus Mkude: Sina swali lingine. Re Examination imeishia hapo. Jaji anamruhusu Shahidi. Shahidi anatoka akiwa ameshika kipaza sauti. Jaji Ndunguru: Unasahau maji yako hapo. Shahidi: Hapana siyataki tena. Jaji: Basi turudishie hiyo MIC tafadhali. Anairudisha na kutoka nje akiwa anatikisa kichwa. Watu wanacheka.😂😂😂 Kesi inaahirishwa watu wakale. Tutaendelea baada ya lisaa limoja. Naomba repost yako.
















