"Kuna makubaliano ambapo shirika letu la umeme TANESCO na Shirika la Umeme la Rwanda, wataanza kuuziana umeme kwa ajili ya kuchochea zaidi maendeleo ya kiuchumi." - Rais Samia Suluhu Hassan na Rais Paul Kagame wakizungumza na waandishi wa habari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa Ziara ya Kikazi, tarehe 03 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe. Paul Kagame akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa Ziara ya Kikazi, tarehe 03 Mei, 2026.
Kwani sisi wanawake ni viumbe vilivyolaaniwa?
Kwanini kila kiumbe dhaifu hufananishwa na Mwanamke?
Siku nyingine wekeni hata mnyama mbaya please...
Mbali na ukweli kwamba Samia katuchafua lakini yuko Netumbo Ndaitwah kule Namibia anatuheshimisha sana.
Siku ya Jana ilikuwa njema sana, kongamano la wanafunzi wa vyuo vikuu lilifana sana. Vijana walipata madini ya kutosha na kuelewa vema itikadi na falsafa ya @ChademaTZ2 , ni jukumu la Vijana wasomi kupigania nchi yao. Viongozi wetu wamejenga sprit mpya ya mapambano kizazi hiki.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo na Ujumbe wa Rwanda uliongozwa na Rais wa Nchi hiyo Mhe. Paul Kagame, tarehe 03 Mei, 2026.
#KitengeUpdates
Mjomba wake msanii TEMBA alitekwa, jana maiti yake imeonekana imesombwa na maji huko Tabata haina KICHWA.
Hutasikia uwajibikaji kwa vitendo vyote hivi vya utekaji kwasababu watekaji ni wao.
Tanzania kuna VIBAKA wachache wao ndio wanatoa VIBALI vya watu kuishi sio kazi ya MUNGU tena.
James Temba ni ndugu wa Mwanamziki wa kundi la TMK Wanaume Family wakuitwa Mhe. Temba James
Temba alitekwa na watu wasiojulikana Jijini Dar es salaam siku kadhaa zilizopita jana mwili wake umeonekana ukielea mto msimbazi Tabata huku ukiwa hauna kichwa.
RAIS SAMIA NA KAGAME WAKUBALIANA KUONDOA VIKWAZO VYA BIASHARA KUCHOCHEA UCHUMI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Rwanda zimefikia makubaliano ya kuondoa vikwazo visivyo vya kikodi pamoja na changamoto nyingine za kibiashara ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi kati ya mataifa hayo mawili.
Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya Rais wa Rwanda, Paul Kagame, Rais Samia amesema hatua hiyo inalenga kutumia kikamilifu fursa zilizopo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na soko huria la Afrika.
Amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana, bado kuna haja ya kuendelea kuboresha mazingira ya biashara ili wafanyabiashara na wawekezaji wanufaike zaidi na ushirikiano uliopo.
Rais Samia ameeleza kuwa kuondolewa kwa vikwazo hivyo kutasaidia kuongeza kiwango cha biashara ambacho tayari kimefikia shilingi bilioni 644, huku pia kikichochea uwekezaji zaidi kutoka Rwanda nchini Tanzania.
Amesisitiza kuwa serikali zote mbili zimejipanga kuhakikisha kuwa majadiliano yanaendelea ili kutatua changamoto zilizopo na kuweka mazingira rafiki zaidi kwa biashara na uwekezaji.
Ziara hiyo imeelezwa kuwa ni hatua muhimu katika kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi na kuimarisha mahusiano ya kihistoria kati ya Tanzania na Rwanda.
"Hakuna kitu kinachonikera kama mtu kuniambia kwamba UVCCM wanaruhusiwa kufanya kongamano chuoni, sisi tunazuiwa, hakuna aliyewazuia mmejizuia nyie wenyewe kwa uoga wenu na nyie mmekubali kama ngombe, nini maana ya elimu?, kama elimu yako haikuwezeshi kufikiri na kukataa ujinga." Mhe. @HecheJohn