DAR: Abiria wamelazimika kuzuia basi la Mwendokasi kupita katika Kituo cha Kimara Mwisho baada ya kusubiri usafiri huo kwa saa kadhaa bila mafanikio, asubuhi ya leo Aprili 22, 2025
Ikumbukwe mara kadhaa Wadau wa JamiiForums.com wamekuwa wakilalamikia changamoto ya usafiri wa Mwendokasi ikiwemo kukaa muda mrefu kituoni
Soma jamii.app/MwendokasiMgomo#JamiiForums#JFHuduma#ServiceDelivery
Video: Kagaba_GR
"Tulishauri kuwa chama (CHADEMA) kiende kikasaini kanuni za maadili na tume ya taifa ya uchaguzi ambayo yalikuwa yanasainiwa tarehe 12 Aprili 2025. Ushauri wetu tuliotoa chama hakikuzingatia hata kidogo, na ilipofika tarehe 12 hawakwenda kusaini. Lakini vilevile tunapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza viongozi wa dini ambao wameona umuhimu wa kufanyika kwa reforms, na wote wameunga mkono msimamo wetu wa G55 na ushauri wetu kwa chama, hakuna kiongozi wa dini aliyesema kwamba tukazuie uchaguzi. Wote wamehimiza waumini wao kwamba waende wakashiriki uchaguzi lakini uchaguzi uwe huru, wa haki na wa amani, kwahiyo mahubiri yote ya Pasaka yameendana na tahadhari tuliyoitoa kwa chama kwamba tunaona hatari ya kupoteza kundi muhimu kama tukiendelea na msimamo kwamba tunakwenda kuzuia uchaguzi, na viongozi wa dini wameungana na G55 kwamba wanaunga mkono mageuzi lakini wanataka watu wakashiriki uchaguzi"- Mrema.
John Mrema kwa niaba ya wafuasi wenzake wa Kundi la G55 ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akizungumza na waandishi wa habari siku ya Jumanne Aprili 22, 2025 mkoani Dar es Salaam juu ya yanayoendelea kufanywa na chama hicho hasa suala zima la kutoshiriki uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt Balozi Emmanuel Nchimbi kuanza ziara ya Siku tano katika Mkoa wa Mara
Karibu kufuatilia ziara hiyo kupitia vyombo vya Habari na Mitandao yetu ya Kijamii
Kazi na Utu , Tunasonga Mbele
Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ambapo hadi kufikia Februari, 2025 kilomita 13,820 kati ya 16,280 zimejengwa na kuunganisha wilaya 109 kati ya 139 pamoja na vituo 111 vya kutolea huduma za Mawasiliano.
🛑 TAARIFA KWA UMMA KUHUSU TAARIFA ILIYOSAMBAA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII IKIWAHUSISHA ABIRIA WA MABASI YAENDAYO HARAKA KUZUIA MOJA YA BASI KATIKA KITUO CHA KIMARA MWISHO.
Katika kipindi cha mwaka 2020 hadi mwaka 2025 serikali imeajili walimu 44,527 wakiwemo walimu 447 wa elimu maalumu.
Huu ni utekelezaji wa vitendo wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2020-2025).
#MamaAnafanikisha#KaziNaUtuTunasongaMbele
Urefu wa barabara za vijijini na mijini zilizojengwa kwa kiwango cha lami umeongezeka.
✅Mwaka 2020 - kilomita 2.025
✅Mwaka 2025 - Kilomita 3,467.30
Hii ni hatua kubwa kuelekea kuimarisha usafiri, kukuza uchumi wa ndani na kuunganisha maeneo.
#MamaAnafanikisha#KaziNaUtuTunasongaMbele
Serikali imetoa mikopo ya shilingi bilioni 158.50 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambapo shilingi bilioni 63.40 ni wanawake (vikundi 8,576), shilingi bilioni 63.40 ni vijana (vikundi 4,981) na shilingi bilioni 31.70 watu wenye ulemavu (vikundi 2,319)
Katika kipindi cha Novemba, 2020 hadi Machi, 2025
Makusanyo halisi ya mapato ya ndani ya halmashauri yameongezeka kutoka shilingi bilioni 757.05 mwaka 2020/21 hadi shilingi trilioni 1.15 mwaka 2023/24 sawa na asilimia 77.
Fedha za mapato ya ndani zilizopelekwa katika miradi ya maendeleo zimeongezeka kutoka shilingi bilioni 276.69 hadi shilingi bilioni 313.26 sawa na asilimia 13.21.
Katika kipindi cha mwaka 2020 hadi Machi 2025, serikali imeajiri wataalamu wa afya 34,720.
#MamaAnafanikisha upatikanaji wa huduma bora za afya karibu na wananchi.
#KaziNaUtuTunasongaMbele
Kwa taarifa nilizopata asubuhi ya leo ni kwamba kuna Bus 🚌 41 kutoka mikoa 19 wanaosafiri kwenda Dae es Salaam kwa ajili ya kesi ya Tundu Lissu hiyo kesho kutwa. Mabasi mengi hasa ya mikoa ya pembezoni yameanza safari leo. Kitu nilichokipenda ni kwamba hawajavaa sare za CHADEMA wala kuweka bendera ya chama kwenye magari yao.
Hawa mabumunda wa akili kisoda nguvu nyingi watakuwa na wakati mgumu sana labda wazuie mabasi yote ya kukodisha kuingia Dar. Hata hivyo watu wengi zaidi wamekata tiketi kwenye mabasi ya mikoani. Wengi wataanza kuingia kesho asubuhi na kesho kutwa asubuhi. Hotel za Dar zimeanza kujaa leo.
Serikali imeendelea kutekeleza mkakati wa kuwatambua, kuwasajili na kuwaendeleza wafanyabiashara ndogondogo. Hadi Februari 2025, tayari wafanyabiashara 63,222 wamesajiliwa. Aidha, shilingi bilioni 8 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya mikopo yenye mashartinafuu kwa wafanyabiashara ndogondogo. Hadi kufikia Februari, 2025 wafanyabiashara ndogondogo 1,008 wamepata mikopo hiyo.
Tayari imekamilisha ujenzi wa vyuo vipya 29 vya ufundi stadi ambavyo vimechangia kuongezeka kwa udahili wa wanafunzi wa ufundi stadi kutoka 415,131 mwaka 2023/2024 hadi 425,509 mwaka 2024/2025.