Taarifa za nyinyi Tume kutumika na chama tawala kuiba na kuvuruga uchaguzi sio UVUMI, ni FACTS ambazo zilishapata kuthibitishwa mara kadhaa na Makada wa CCM akiwemo Nape na sasa Balozi Polepole kamaliza kabisa with DETAILS…
NB: Acheni huu udwanzi mnaua hili Taifa!
#NRNE
Mwanamitindo na Mtangazaji, Ney Paul ameshauri Vijana kufikiria kabla ya 'kuposti' kauli za Chuki Mtandaoni kwa kujiuliza kama wanajenga au wanabomoa wangejisikiaje iwapo Mtu mwingine angetumia kauli hiyo kwao.
Amesema “Epuka jazba, Usijibu kwa hasira Chukua muda kupumua na kufikiri kabla ya kujibu maoni au jumbe zinazokukasirisha”.
Aidha, amesema Mitandao imebeba fursa nyingi na fedha nyingi, hivyo ni vizuri kama Vijana wataamua kuitumia vizuri.
#JamiiForums#JamiiAfrica#HumanRights#KauliZaChuki#StopHateSpeech#DigitalPeace#NoToHateSpeech#ResponsiblePosting#JamiiYenyeUelewa
Hii Nchi inahitaji Uhuru na ukombozi wa haraka sana.
Inawezekanaje mtandao unavurugwa.
Maisha, biashara za watu zinaharibiwa kwasababu ya ujinga na hakuna mtu wa kujibu au kuwajibishwa?
TRA mtakusanya kodi kwenye biashara za mitandao ambayo haiko reliable mtu mmoja au wawili kwa mapenzi yao wanaweza kuvuruga mtandao wa watu millioni 65!!!!
Shame.
Alichokisema Polepole aliewahi kuwa mjumbe wa cc ya ccm.
Kiongozi wa juu kabisa katika ccm na serikali hakiwezi kupuuzwa.
Tume ya Taifa ya uchaguzi ni tawi la ccm haiwezi kusimamia uchaguzi huru katika Nchi hii.
Msimamo wa chama chetu ni sahihi na Watanzania tusikubali tena uhuni kwenye uchaguzi.
#NoReformsNoElection
"Kwenye makaa ya mawe kampuni moja kutoka Australia – Intra Energy Tanzania Limited (IETL) wakimiliki 70% ndiyo ilikuwa mbia wa Serikali kupitia National Development Corporation (NDC) wakimiliki 30%. IETL wamekuwepo tangu 2011 na hivi karibuni wakataka kujitoa. Aliyekuwa mtoa huduma pale mgodini, Rostam Aziz akasema ananunua hisa zilizobaki kwa Sh5 Bilioni. Serikali ikasema hapana kwa ndiyo walikuwa na right of first refusal (ROFR). Wakati pesa inatafutwa ili Serikali kununua hisa za mwekezaji na kumiliki mgodi wa makaa ya mawe (Ngaka Coal Mine) kwa 100%. Simu moja ilipigwa kutoka juu. Pesa zikarudishwa Serikalini. Hivi tunavyozungumza Rostam Aziz ndiye mmiliki wa mgodi huo wa makaa ya mawe. Mkaangalie pale Fair Competition Commission (FCC) kama mnunuzi wa zile hisa 70% za IETL (kampuni ya Rostam Aziz, Mirambo Mining) imelipa hata kodi. Nchi yetu inabagazwa sana" – Balozi Humphrey Polepole
@Sativa255 sasa kazi ya vyombo vya dora ni nini wao kutwa kuwinda chadema tuu ndo kazi yao lakin mambo kama hayo hawayaoni unashangaa sana hii inchi hii
DODOMA: Akizungumza Agosti 18, 2025 kwenye Baraza la Wafanyakazi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari ametoa onyo kwa Watumishi wanaovujisha siri za Serikali, akibainisha kuwa ofisi yake itawafuatilia kwa ukaribu na kuchukua hatua za kinidhamu kwani ni kinyume na miongozo, Kanuni na Sheria za nchi, pia kufanya hivyo ni sawa na kujipiga risasi mwenyewe.
Pia, alieleza kusikitishwa na uwepo wa Mawakili wa Serikali wenye tabia za uongo, akisema jambo hilo linaweza kuipunguzia heshima taaluma ya Sheria na kuichafua taswira ya Serikali mbele ya umma.
Soma zaidi jamii.app/MwanasheriaSer…#JamiiAfrica#JamiiForums#Accountability#Uwajibikaji
DAR: Imam wa Msikiti wa Manyema, Sheikh Hameed Jongo akizungumza wakati wa kutoa hotuba ya Ijumaa Agosti 15, 2025 amesema kuwa Rais Samia anatenda haki na kufanya vizuri katika uongozi wake ndiyo maana wafanyabiashara wamechangia kikubwa walichochangia.
Ameongeza kuwa kuna Wanawake wana uwezo wa kuongoza kuliko wanaume, uongozi uliopita tumeona jinsi wanaume walivyoongoza, awamu hii ya sita Rais Samia anaongoza 'Fantastic'.
Soma zaidi jamii.app/HarambeeCCMAma…#JamiiForums#JamiiAfrica#JFSiasa#UchaguziMkuu2025
DODOMA: Mahakama Kuu inatarajiwa kutoa uamuzi wa mapingamizi yaliyowekwa na Chama Cha Mapinduzi (#CCM) dhidi ya Mchungaji Dkt. Godfrey Malisa, ambaye anapinga uhalali wa mchakato uliompitisha Rais Samia Suluhu Hassan na mgombea mwenza Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwania urais kupitia Chama hicho.
Mawakili wa CCM, Fabian Donates na Alex Mgongolwa, leo Agosti 19,2025 wamewasilisha mapingamizi wakidai hatua za kufungua shauri hilo hazikufuatwa, huku wakisisitiza mlalamikaji alipaswa kuandika barua kwa Katibu Mkuu badala ya mwenyekiti wa Chama.
Aidha, wakili wa mlalamikaji, Denis Maringo, amesema taratibu zilizingatiwa kwani Februari, 2025, Dkt. Malisa alimwandikia barua Rais Samia akilalamikia uteuzi wake, ambapo baada ya hoja za pande zote kusikilizwa, Kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 22, 2025.
Soma jamii.app/MalisaNaCCM#JamiiAfrica#JamiiForums#Siasa#Demokrasia#UchaguziMkuu2025#Governance
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere unastahili kuwa kinara!
Tupigie kura ili ushinde tuzo ya “Uwanja Bora wa Ndege Afrika” katika World Travel Awards 2025.
Onyesha uzalendo na mchango wako kwa maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga Tanzania.
Piga kura leo kupitia kiungo hiki:
worldtravelawards.com/vote-for-juliu…#ChaguoLaWasafiri#PigaKuraJNIA#WorldTravelAwards
#MICHEZO: Klabu ya Al Merriekh kutoka nchini Sudan, imemfuta kazi kocha wao raia wa Italia, Giovanni Solinas kutokana na mwenendo mbovu wa matokeo.
Timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu nchini Mauritania wanashika nafasi ya 6 katika msimamo wakiwa na alama 18, wakishinda michezo 5, sare 3 na kupoteza michezo 3 baada ya michezo 11.
#Michezo#Hainakuchoka#EastAfricaTV