Vlux
3.5K posts



#TANZANIA: WALIOHUSIKA WAFIKISHWE KWENYE VYOMBO VYA HAKI, WATU WEMA TUNAOBAKI TUINGIE KWENYE MARIDHIANO - WASIRA Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira amesema kabla ya kuanza kwa mchakato wa maridhiano ya kisiasa, ni vyema kuwabaini kuwachukulia hatua za kisheria kupitia vyombo vya haki watu waliohusika na vurugu zilizosababisha madhara vikiwamo vifo. Amempongeza Rais Samia Suluhu kwa kuunda Tume ya Kuchunguza Vurugu za Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 kwa lengo la kujua kiini cha tatizo hilo. Wasira aliyaeleza hayo Mei 16, 2026 alipohutubia mkutano wa hadhara Mjini Kigoma akiwa katika ziara ya kichama mkoani humo. "Mimi sijasema jina la mtu, lakini wenye kujua hayo mambo wanajijua, waache jinai ichunguzwe kama walihusika waende kwenye vyombo vya haki na sio wengi, wanaobaki watu wema tukae tufanye nao maridhiano," alisema. Alimpongeza Rais Samia kwa kuunda tume ya kusaidia kujua chanzo cha vurugu hizo, pia alipongeza kazi nzuri iliyofanywa na tume hiyo kufanya uchunguzi huo. "Rais tunamshukuru na kumpongeza sana, kwa kuunda tume ya kutusaidia kujua chanzo. Tunampongeza na tunaipongeza tume ambayo imesema katika uchunguzi wake imegundua kuna watu si wengi lakini ndio walioanza mpango ule walifadhili" - Wasira "Sasa wanasema (tume) wao hawakuwa polisi wa kuwakamata, lakini wanasema tuchunguze wale walioonekana ili tusiwe tunafuga nyoka ndani ya nyumba" - Wasira. Aidha, Wasira alisema hakuna anayeshabikia matukio yenye kuumiza yaliyosababisha vifo na kwamba anayefanya hivyo hayuko sawa kiakili. "Wanasema watu wamekufa, ni nani anafurahia kufa watu labda uwe na wewe akili yako imeharibika kama unasherehekea kufa watu. Wote tunapinga mauaji, lakini nani amesababisha, halafu wale walioko wengine kama tunawahisihisi ndio tena wanataka kutufundisha namna ya kufanya vurugu muanzishe nyie na namna ya kumaliza mgogoro mtupe nyie, hapana" - Wasira










Kwa Mujibu wa @HecheJohn Makamu Mwenyekiti @ChademaTZ2 ni kwamba hali ya kiafya ya @TunduALissu ni mbaya, Ana maumivu makali sana ya Tumbo. Magereza awajatoa taarifa yoyote kuhusu changamoto ya Afya anayokabiliwa nayo Mhe. Lissu, na kueleza kama amepata matibabu yoyote kutokana na changamoto hiyo.





Eti huyu jamaa na chama chake ndio wawaongoze Tanzania kwenye maridhiano. Eti chama hiki kilichotudharau na kutebeza Watanzania kipindi tunajipanga na maandamano ya kukomboa taifa eti leo ndio kisimamie maridhianozzzz CCM wanajitekenya na kucheka wenyewe. Maridhiano Kati ya CCM na ACT Wazalendo yasituhusishe Watanzania. Wafanye wenyewe kujifurahisha nafsi zao ila wasituhusishe wanachi. Watanzania imani yetu ipo kwenye chama kilichosimama na sisi kipindi cha mauaji ya Oktoba 29. Na Chama hiko ni Chadema pekee!!!! Vyama vingine vyote hatuvitambui……








