The Survivor.™️

1.6K posts

The Survivor.™️

The Survivor.™️

@think_huge

The revolution will not be televised..!! TaL to tell the tale!

Tanzania Katılım Haziran 2017
662 Takip Edilen67 Takipçiler
Sabitlenmiş Tweet
The Survivor.™️
The Survivor.™️@think_huge·
@Tigo_TZZ Tigopesa Super App is super duper! Kwanini Tigopesa Bustisha imekua kama ya kitapeli siku izi?? Unalipia huduma kwa Bustisha na pesa hamfikii Mfanyabiashara baadae unakatwa kwamba eti unadaiwa Bustisha! Hii haijakaa sawa inatupa mashaka na huduma yenu.
Indonesia
1
0
0
162
The Survivor.™️ retweetledi
Godbless E.J. Lema
Godbless E.J. Lema@godbless_lema·
GEITA ASANTE SANA. Barabara ya lami si maendeleo ya kweli. Maendeleo ya msingi na yenye maana huanza kwa kuheshimu utu wa watu, haki zao, uhuru wao na usawa wao. Mambo mengine kama lami, majengo na miundombinu yanapaswa kuwa huduma za kawaida za dola, si mbadala wa haki za wananchi
Godbless E.J. Lema tweet mediaGodbless E.J. Lema tweet mediaGodbless E.J. Lema tweet mediaGodbless E.J. Lema tweet media
Indonesia
13
175
802
11K
The Survivor.™️ retweetledi
Brenda Rupia Jonas
Brenda Rupia Jonas@BrendaRupia·
Asanteni Katoro, Taarifa ya mchango wenu kwa ajili ya kueneza injili ya Katiba Mpya na Free Tundu Lissu ni kama inavyoonekana, Asanteni tena na tena. Tuendelee kukichangia chama chetu,kupitia namba 0744 446969 Jina Chadema HQ
Brenda Rupia Jonas tweet media
Indonesia
9
110
545
5.7K
The Survivor.™️ retweetledi
Mtikila Jr
Mtikila Jr@Legend_Mtikila·
FAM alituuza sana, Ahsante mwenyezi Mungu kwa kutuletea Lissu na Heche. Pipoooooz✌️
HT
27
84
859
25.6K
Brenda Rupia Jonas
Brenda Rupia Jonas@BrendaRupia·
Jana tarehe 15 Mei 2026 nimeshiriki katika kikao Maalum cha kanda ya Victoria kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar, Mhe. Said Mzee Said, kilichowakutanisha viongozi wa ngazi ya Kanda na mikoa katika maandalizi ya uzinduzi wa Operesheni ya #KatibaMpya #FreeLissu,itakayofanyika leo Katoro Mkoa wa Geita. Peeeeoooooopllessssss💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾
Brenda Rupia Jonas tweet mediaBrenda Rupia Jonas tweet mediaBrenda Rupia Jonas tweet mediaBrenda Rupia Jonas tweet media
Indonesia
5
57
275
4K
ACTWazalendo
ACTWazalendo@ACTwazalendo·
Ameandika Katibu Mkuu ACT Wazalendo @AdoShaibu MAKOSA 5 YA KIMKAKATI YA VYAMA VYA UPINZANI. Vyama vya Upinzani Tanzania, katika miongo mitatu ya uwepo wake, vimefanya mengi, mazuri kwa mabaya. Kwa maoni yangu, yafuatayo ni makosa ya dhana ya vyama vya upinzani (strategic misconceptions) katika kuing’oa CCM madarakani; 1. Kudhani kuwa, katika mazingira yetu, kuna Chama kinaweza kufanikiwa chenyewe kuing’oa CCM bila mshikamano wa vyama vya siasa. 2. ⁠Kudhani kwamba CCM inaweza kuvihurumia vyama vya upinzani na kukubali kuweka mazingira itayoking’oa. 3. ⁠Kudhani CCM inaweza kuleta mabadiliko (reforms) bila shinikizo 4. ⁠Kudhani kwamba vinapambana na CCM badala ya dola. 5. ⁠Kudhani kwamba CCM inaweza kudondoka bila kukata mizizi yake ambayo ni hali ya Chama hicho kujigeuza kuwa Chama dola (State Party) Unakubaliana na mimi? Kuna makosa gani mengine vyama vya upinzani tunayafanya? Yataje. Tupo tayari kujifunza. #TaifaLaWote #MaslahiYaWote
ACTWazalendo tweet media
Indonesia
37
10
49
10.2K
The Survivor.™️ retweetledi
Tito Magoti
Tito Magoti@TitoMagoti·
Walimuweka jela SC Tundu Lissu ili tusiwe na kiongozi. Mungu ni mwema, kwa zaidi ya mwaka, tumeumizwa kwa viwango vyote, ila sisi ni IMARA zaidi yao. Stay safe & vigilant, Tata John Heche.
Tito Magoti tweet media
Indonesia
8
173
930
8.5K
Mtikila Jr
Mtikila Jr@Legend_Mtikila·
Ni miongoni mwa watu wachache sana waliomkataa Mbowe kwa usaliti wake. Namna Martin alivyokuwa karibu na Mbowe ilikuwa ni ngumu sana kumtema, jamaa akachagua democrasia na ukweli. Hapa ndipo nilianza kumkubali Martini Salute kwake✌️
Mwinshehe 🕊️@Mwinshehe07

Martin maranja masese @IAMartin_ ni mtetezi wa haki za binadamu na mchambuzi wa siasa mwenye ushawishi mkubwa katika mijadala ya kijamii hasa kupitia mitandao ya kijamii Alianza maisha yake ya kazi kama mwalimu kisha akaamua kuacha ajira ya serikali na kujikita katika shughuli huru za kijamii na kitaaluma akilenga zaidi kuelimisha jamii kuhusu haki za binadamu, uwajibikaji na utawala bora Umaarufu wake umejengwa juu ya uwezo wake wa kipekee wa: 1:kuchambua masuala ya kisiasa kwa kina na kwa mantiki 2:kuunganisha sheria, historia na uhalisia wa kijamii katika hoja zake 3:kuelimisha vijana kuhusu haki zao na wajibu wao katika jamii 4:kuhimiza uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi Kupitia mitandao ya kijamii hasa X/Twitter amekuwa chanzo cha mijadala yenye manufaa kwa jamii akisaidia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu demokrasia, haki za binadamu na masuala ya utawala Katika safari yake amekutana na changamoto mbalimbali ikiwemo shinikizo la kijamii na kuitwa na vyombo vya dola kutokana na msimamo wake wa wazi lakini hali hiyo haijamzuia kuendelea kusimamia anachoamini Mpaka sasa anaendelea kutambulika kama mmoja wa sauti muhimu zinazochangia uelewa wa haki za binadamu, uwajibikaji wa viongozi na maendeleo ya fikra za kisiasa miongoni mwa vijana Tanzania

Indonesia
8
17
159
10.4K
The Survivor.™️ retweetledi
Baba Mwita
Baba Mwita@BabaMwita·
TAL ni Kiongozi wa Taifa zima si tu wa CHADEMA. Hivyo, ni WAJIBU kila mmoja wetu, pasipo kujali ITIKADI zetu za kisiasa KUHAKIKISHA tunapaza sauti Lissu atoke gerezani. Mahakama IMESHINDWA kufanya kazi kwa UHURU. Lissu atatoka kwa nguvu ya Umma tu. #FreeTunduLissu #FreeTunduLissu
Indonesia
16
218
674
8.4K
𝐉𝐚𝐬𝐮𝐬𝐢
MARIDHIANO TENA???? 🙄 Huu ni msimamo wa Chadema au wa Joseph Mbilinyi?
𝐉𝐚𝐬𝐮𝐬𝐢 tweet media
Indonesia
12
4
43
10.3K
Martin Maranja Masese
Martin Maranja Masese@IAMartin_·
Kwa wale ambao mmepata mgagasiko na kutoelewa ni kitu gani ambacho Nabii @godbless_lema ameandika kuhusu kaka @zittokabwe. Ni kwamba nabii anajaribu kuzungumzia BUSU LA YUDA kwa lugha ya picha. Busu ambalo linapatikana katika Mathayo 26:47-49. Katika simulizi za Injili, busu la Yuda halikuwa kielelezo cha mapenzi ya dhati, bali lilikuwa ishara ya kiufundi (signal) iliyolenga kuondoa utata wa nani aliyepaswa kukamatwa katika giza la bustani ya Gethsemane usiku huo. Huo ulikuwa ni uthibitisho wa kimya kimya. Bustani ya Gethsemane ilikuwa na miti ya mizeituni iliyotengeneza vivuli vizito. Askari wa Kirumi na walinzi wa hekalu ambao hawakumjua Yesu kwa sura, wangeliweza: (i) Kumkamata mtu asiyehusika wapo waliofanana naye. (ii) Kutoa mwanya wa kutoroka. Yuda alichagua busu kwa sababu ya ukaribu na uhakika. Maandiko ya asili ya Kiyunani, neno linalotumika ni “kataphileo”, maana yake ni kubusu kwa kurudia. Yuda alifanya hivyo ili kuhakikisha askari hawaachi shaka hata kidogo kuhusu nani anayepaswa kutiwa mbaroni. Ni kitendo kinachotumia lugha ya upendo (busu) kutekeleza dhamira ya mauti (usaliti). Hii inafundisha kuwa si kila anayekukaribia kwa tabasamu au ishara ya mshikamano ana nia njema; mara nyingi “busu” hutumika kuficha kisu kilicho nyuma ya mgongo. Yuda hakuwa na upendo wa dhati. Kwake, Yesu alikuwa “bidhaa” yenye thamani ya vipande 30 vya fedha. Hii inatofautisha kati ya: (i) Wafuasi wenye Itikadi: Ambao wako tayari kufa na mwalimu wao. (ii) Wafuasi wenye Maslahi (Opportunists): Watamuuza mwalimu. Wanajitokeza “kutubusu” wakati huu wa shinikizo dhidi ya Msajili wa Vyama vya siasa. Mshikamano wao si wa dhati, bali ni mbinu ya kujitengenezea mazingira ya kurithi wanachama na wafuasi wetu iwapo chama kikuu cha upinzani kitakumbwa na dhoruba za kisheria. Utawala uliopo madarakani hauna uhalali kwa umma. CCM wamepachikwa madarakani kwa nguvu za DOLA na kutafutiwa uhalali na vyama mpango wa kando kama ZAMBARAU na vyama vingine ambavyo vimetumika kuhalalisha ushindi wa 98% wa MaCCM. Wakati tunasema tuwakatae MaCCM, wao walisema watalinda kura. Wamemaliza kazi ya shetani, na shetani ameanza kushughulika na WATEULE. Vibaraka wa shetani wanajitokeza kutubusu, wakifikiri kwamba hata kama CHADEMA itafutwa, tutahamia chama chao. Huwezi kuwa na dhamira njema na CHADEMA wakati katika siku 400 hujawahi kwenda gereza la Ukonga kumuona Tundu Lissu au kuhudhuria kesi ya uhaini Mahakamani. Unaogopa kuwakwaza ‘mabosi’ wako kuonekana unasimama na Tundu A.M Lissu. Katika mazingira ya mapambano yoyote, busu la Yuda linabaki kuwa fundisho la tahadhari. Ni ukumbusho kwamba adui hatari zaidi si yule aliyesimama mbali na silaha, bali ni yule anayekusogelea kwa ishara ya urafiki ili kukutia alama kwa ajili ya wapinzani wako. Tunataka mshikamano (solidarity) kutoka kwa kila mtu ambaye anapinga mifumo kandamizi ya dola la CCM hadharani. Lakini tunataka ambaye ana mwendelezo (consistency) wa kupambania haki za kijamii bila kutumika na Serikali katili ya CCM kuhalalisha ukatili.
Martin Maranja Masese tweet mediaMartin Maranja Masese tweet media
Filipino
32
175
770
29.9K
The Survivor.™️
The Survivor.™️@think_huge·
@MsigwaPeter Baba Mchungaji Mungu akupe maisha marefu! Umeandika ukweli na bila ukweli ndo silaha pekee ya kuliponya hili Taifa.
Filipino
0
0
2
508
Peter Msigwa
Peter Msigwa@MsigwaPeter·
Tanzania haihitaji hofu zaidi. Inahitaji uponyaji. Kwa sababu taifa lililojeruhiwa, mwishowe huanza kujijeruhi lenyewe. Leo tunapaswa kusema ukweli si kwa chuki,si kwa kisasi,bali kwa hofu ya kweli kuhusu mustakabali wa nchi yetu. Kama Michael Jackson alivyowahi kusema: “Tunapaswa kuponya dunia yetu iliyojeruhiwa. Machafuko, kukata tamaa, na uharibifu usio na maana tunaouona leo ni matokeo ya watu kujisikia wametengwa kutoka kwa wenzao na mazingira yao.” Kauli hii kwa sasa Inakuwa onyo hata kwetu sisi Watanzania, kama sehemu ya dunia Wananchi wanapoanza kujisikia: hawasikilizwi, wametengwa, wananyamazishwa, wanadhalilishwa, au wanachukuliwa kama maadui kwa sababu tu wana mawazo tofauti. umbali wa hatari huanza kujengwa kati ya wananchi na dola. Na historia inatufundisha jambo moja la kuogopesha: Mataifa mengi hayaanguki kwanza kwa sababu ya adui wa nje. Huanzia kudhoofika ndani wakati imani ya wananchi inapokufa. Nchi haiwezi kujenga amani ya kudumu: kama hofu inakuwa kubwa kuliko uhuru, kama utii unakuwa muhimu kuliko ukweli, kama taasisi zinaonekana kuwa za upande mmoja, au kama ukosoaji unatafsiriwa kama usaliti. Kwa sababu jamii iliyojeruhiwa huzalisha wananchi walioumia. Na wananchi walioumia mwishowe huzalisha: hasira, mgawanyiko, msimamo mkali, kukata tamaa,au chuki ya kimya kimya. Viongozi wanapaswa kuelewa: si kila ukimya ni amani. Wakati mwingine watu wananyamaza kwa sababu: wamechoka,wanaogopa,au wamekata tamaa. Na kukata tamaa ni hatari kwa taifa lolote. Tanzania ilijengwa juu ya msingi imara ya : utu,umoja,mazungumzo, uvumilivu,na hisia ya kuwa taifa ni la wote. Julius Nyerere alielewa jambo kubwa sana,taifa haliishi kwa nguvu pekee (power) linaishi pia kwa uhalali wa kimaadili. Wananchi wakianza kuhisi kwamba: haki inategemea upande wa kisiasa, ambao mtu yupo, taasisi si huru tena, au demokrasia ipo kwenye maneno lakini si kwenye vitendo, ule mkataba wa kihisia kati ya taifa na wananchi huanza kupasuka. Kwa hiyo haya si mashambulizi. Hili ni onyo. Onyo kwamba: siasa zinapokuwa za uhasama kupita kiasi, mamlaka zinapoanza kuogopa ukosoaji, wapinzani wanapoonekana maadui, na wananchi wanapopoteza imani kwa mifumo ya taifa taifa lenyewe huanza kujeruhiwa kihisia. Na taifa lililojeruhiwa huwa taifa lisilo tulivu. Hatuhitaji kulewa kisiasa zaidi. Tunahitaji hekima. Hatuhitaji viongozi wanaotaka kusifiwa tu. Tunahitaji viongozi wenye uwezo wa kusikiliza ukweli usiofurahisha. Kwa sababu uzalendo si ukimya. Wakati mwingine uzalendo ni ujasiri wa kusema: “Kuna jambo linaenda vibaya kabla hatujachelewa.” Kama Tanzania inataka kubaki imara, basi uponyaji lazima uwe sera ya taifa. Uponyaji: kati ya viongozi na wananchi,kati ya dola na upinzani,kati ya mamlaka na uwajibikaji,kati ya sheria na haki. Kwa sababu hakuna taifa linaloweza kuishi milele kwa: hofu, propaganda,au mgawanyiko wa kihisia. Mwisho wa yote, taifa huwa imara zaidi pale wananchi wake wanapoamini kwamba: wao ni sehemu ya taifa,wanalindwa, wanasikilizwa,na utu wao una thamani. Mungu ailinde Tanzania isije kuwa nchi ambayo wananchi wanaogopana kuliko kuaminiana. Na viongozi wetu wakumbuke: historia haitawahukumu viongozi kwa barabara, madarasa , vituo vya afya walivyojenga pekee, bali pia watahukumiwa kwa hali ya kihisia walizoliachia taifa. Usisahau: “Jamii iliyojeruhiwa huzaa watu waliojeruhiwa… na watu waliojeruhiwa huongeza machafuko zaidi.” Rev Petet simon Msigwa! Iringa
Indonesia
171
234
1.1K
55K
Peter Madeleka
Peter Madeleka@PMadeleka·
Mheshimiwa NAPE NNAUYE 👇 ni mmoja wa WANASHERIA NGULI ambao Tanzania IMEBAHATIKA kuwa nao, hata kama FORM 4 hakupata DIVISHENI WANI.
Peter Madeleka tweet media
Filipino
23
44
654
30.7K
Zitto MwamiRuyagwa Kabwe
Zama za Ofisi ya Msajili wa Vyama kuwa mchezaji namba 12 wa CCM FC zimekwisha. Dola isome alama za nyakati. The writing is on the walls! Msajili STOP THIS NONSENSE ya kutaka kufuta CHADEMA. Utafutwa wewe, No doubt about this! Tume ya Chande iliyoundwa na Rais imetoa Taarifa inayosema wananchi wanailalamikia Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa kutokutenda haki kwenye kusimamia shughuli za vyama vya Siasa. Badala ya Msajili kuchutama, kuwajibika na kubadilika anarudia makosa yaleyale yaliyopelekea mauaji yaliyoanza Oktoba 29. Msajili anajua, Watanzania wanajua na Dunia inajua kuwa Kuna ushahidi wa kutosha wa CCM kufanya makosa makubwa kuliko hata ambayo msajili ameituhumu Chadema, hatukuwahi kuona hatua zozote zimechukuliwa na Ofisi hii ya Msajili. Ofisi ya Msajili ijue WATANZANIA SIO MABWEGE. Tunachukulia tishio lolote dhidi ya CHADEMA ni tishio dhidi ya Demokrasia. An attack to one, is an attack to all. Iacheni CCM ifanye Siasa za Ushindani dhidi yetu. Nasi tufanye siasa za ushindani dhidi yao. Acheni kuwa mbeleko ya CCM. Mtaanguka nayo. Ujumbe huu sio wa Msajili tu bali pia ni kwa VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA pia. Kaeni pembeni acheni vyama vya Siasa vifanye Siasa. Mnataka watu wangapi wafe ili mpate somo?
Indonesia
135
420
1.5K
49.8K
Boniface Mwabukusi
Boniface Mwabukusi@Mwabuk2Boniface·
OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA IDHIBITIWE KABLA HAIJASABABISHA MAAFA KWA MARA YA PILI. Tumeshauri sana na tunaendelea kushauri.Ofisi ya Msajili wa Vyama ndiyo chemichemi ya vurugu za kidemokrasia ndani ya Vyama vya Upinzani na inamchango mkubwa katika vurugu za Oktoba 29. Kimsingi Tume ya Uchaguzi na Ofisi hii ya Msajili wa vyama kwa matendo au kutowajibika kwao zimesababisha asilimia zaidi ya 60 kupelekea Mauwaji ya Oktoba 29/2025. Baadhi ya Maofisa wake kwa makusudi,kujipendekeza au kutumika wana mchango mkubwa sana katika kuharibu Haki, Amani ,umoja,utulivu wa kidemokrasia ndani ya vyama vya siasa na ustahimilivu wa Kidemokrasia Ofisi hii Inafanya na Kutenda kwa kuzingita Uonevu,ubaguzi,hila na Inaongoza kwa matumizi mabaya ya Mamlaka. Tunaweza tukalaumu vyombo vingine vya kusimamia sheria kama Polisi,Jeshi,Mahakama na vyombo vingine vya Ulinzi ila tusisahu kuwa kinu kinachofua na kuandaa hila, fitina na machafuko ni Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa ambayo imeacha kazi ya kusajili vyama na imejigeuza Ofisi ya kuvutuga utulivu ndani ya vyama na kuminya uhuru wa kidemokrasia na ushiriki mpana wa vyama vya siasa. Tusipo ziba Ufa tutajenga Ukuta,Mwanzo wa ngoma ni lele , na Asiye sikia la Mkuu huvunjika guu.Hala hala kidole na Jicho. BAK Mwabukusi.
Boniface Mwabukusi tweet media
Indonesia
87
511
1.6K
29K