Engr.Vini🦅 retweetledi

Mpwa wa #MheshimiwaTemba ametekwa kwa zaidi ya siku tatu, huku msanii huyo akikaa kimya bila kutoa tamko lolote. Huu ndio udhaifu mkubwa wa wasanii wazembe wa mbogamboga. Ndugu yake ametekwa, haonekani nyumbani siku zote hizo, hajawahi kupaza sauti kwa kuandika katika kurasa zake huko Instagram au kusema kwa maneno. Baada ya kijana huyo kupatikana ameuawa kinyama, akiwa amekatwa kichwa na mwili wake kutupwa mtoni, ndipo Temba anaibuka na kuandika: “Mungu yupo, atatenda miujiza.” Mungu hamsaidii asiyejisaidia: Huwezi kusubiri majanga yafike mwisho ndipo upaze sauti. Hakuna aliye salama. Ni lazima sote tusimame kidete na kukataa katakata vitendo hivi vya UTEKAJI na mauaji ya kinyama.
Indonesia


















