MR BEBERU JR retweetledi
MR BEBERU JR
106.7K posts

MR BEBERU JR retweetledi

Nilitarajia Mary Chatanda awe mtetezi wa wanawake waliopoteza watoto na waume zao katika mauaji ya Oktoba 2025."
Mwenyekiti wa @NgomeyaWanawake
@JaneRithe
#MachoziYaMamaDeniLaTaifa
@ACTwazalendo
Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi

It’s not over till justice🙏🇹🇿
semafor.com/article/05/19/…
English
MR BEBERU JR retweetledi
MR BEBERU JR retweetledi

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimesisitiza kuwa haki ya kutoa maoni ya kisiasa, kuikosoa serikali, kueleza msimamo wa Chama kuhusu masuala ya Kitaifa pamoja na haki ya wananchi kushiriki katika mijadala ya kisiasa ni haki zinazolindwa moja kwa moja na Katiba ya Tanzania hivyo haki hizo haziwezi kufutwa kwa tafsiri banifu, ya kisiasa au ya kibaguzi inayolenga kukandamiza vyama vya ushindani Nchini.
Kauli hiyo imetolewa katika barua ya Chadema iliyosainiwa na Katibu Mkuu wake Bw. John Mnyika leo Mei 20, 2026 kwenda kwa Msajili wa Vyama vya siasa Nchini, akisema Chama hicho pia kimekwazwa na kushangazwa na jinsi Msajili alivyowataka kuwasilisha maelezo kuhusu utekelezaji wa sheria ya Vyama vya siasa kutokana na mfululizo wa matukio ya uvunjifu wa sheria yanayofanywa na Chama hicho.
"Ni kanuni ya wazi kabisa kuwa barua ya Msajili ya Mei 07, 2026 ina kasoro kubwa sana ya duplicity kwani inataka vitu viwili tofauti vyenye matokeo tofauti. Kutudai maelezo juu ya kile ulichokiita ni matukio ya uvunjifu wa sheria na baada ya hapo kutaka tutoe utetezi wa kwanini chama kisifungiwe au kusimamishwa kufanya shughuli zake ni kutotenda haki na ni kukiuka misingi ya haki." Imesema barua hiyo.
Chadema imesisitiza pia kwamba Katiba ya Tanzania inatoa haki ya kusajiliwa kwa Vyama vya siasa Nchini na kuwa katika masharti hayo hakuna ambapo kuna kipengele au katazo la kile kilichosemwa na Msajili kuwa ndicho kinachompa nguvu ya kuthibiti maneno na kauli za vyama vya siasa kufuatia madai ya maneno ya uchochezi yanayodaiwa kutolewa na Viongozi wa Chadema.
Chama hicho pia kimemkumbusha Msajili kuwa mtu yeyote anayetoa kauli za kichochezi, kisasi au lugha za matusi zipo sheria zinazoweza kumuadhibu mtu huyo, ikiwa ni pamoja na sheria ya kanuni za adhabu na sheria ya huduma za habari- Chadema ikibainisha kuwa sheria hizo zinayafanya matendo hayo kuwa ni makosa ya jinai na kuipa Mahakama madaraka ya kusikiliza kesi dhidi ya mtuhumiwa na kuamua kama ana hatia au hana.

Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi

"Samia, kesi ya uhaini dhidi ya Tundu Lissu imekushinda na hamna ushahidi wowote wa kuuthibitishia umma. Tafuta njia nyingine ya ushindani wa kisiasa badala ya kutumia mahakama. Muachieni Tundu Lissu sasa hivi! #FreeTunduLissu"
Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi
MR BEBERU JR retweetledi

#FreeTunduLissu
Tundu Lissu hastahili kuwa ndani hata kwa dakika moja!
Kwa sasa focus ni Tundu Lissu aachiwe mengine yatafuata!
Kiongozi wa wananchi, rais wa kweli wa watanzania tunamhitaji mara moja aje kuongoza mapambano!
Let there be only one cry from East to West, from North to South 👉🏽 #FreeTunduLissu
Focus!

Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi
MR BEBERU JR retweetledi
MR BEBERU JR retweetledi

‼️🚨MALISA IS FREE‼️
After a fake charge of treason Pastor Malisa has been released and all charges dropped!
He expressed gratitude to @TanganyikaLaw for legal defence
Mchungaji Malisa hatimaye amefutiwa kesi ya uongo ya uhaini
Heko @TanganyikaLaw kwa kumtetea - hii ndo kazi ya section 4 asemayo @Mwabuk2Boniface kila siku!
Na nyie madhulmat MKOME! Sasa mwachieni Tundu Lissu
#FreeTunduLissu

Filipino
MR BEBERU JR retweetledi

Msikilize Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA @godbless_lema akielezea kwa nini Viongozi wa Serikali ya CCM hawataki kuongerea habari ya HAKI.
Nepotism ni ya kiwango kikubwa sana Nchi hii.
#KatibaMpya
#FreeTunduLissu
Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi

MRISHO GAMBO MBIONI KUHAMIA CHADEMA
Halitakuwa jambo la kushangaza ukisikia Mwanasiasa Mrisho Gambo aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia CCM akihamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Taarifa zilizotolewa na watu wake wa karibu zinaeleza kuwa, *GAMBO* ni kiongozi mwenye tamaa ya madaraka, asiyeaminika kwa sababu mara baada ya kutupwa nje ya Serikali na kutopendekezwa na Kamati Kuu ya CCM Taifa kugombea Ubunge wa Jimbo la Arusha mjini mwaka 2025, alianza kujisogeza kwa GODBLESS LEMA na kuanza harakati za kushirikiana na CHADEMA kwa siri.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa,GAMBO ameahidiwa kupewa nyadhifa ya ndani ya CHADEMA Kanda ya Kaskazini na huenda akatumia Mkutano wa hadhara unaotarajiwa kufanywa na CHADEMA katika viwanja vya relini Arusha mjini tarehe 22/05/2026 kuhamia CHADEMA.
Itakumbuwa pia, kuwa hivi karibuni GAMBO alisifu kukua kwa Demokrasia baada ya LEMA kuongoza kufanyika kwa Mkutano wa CHADEMA hivi karibuni. #UkweliUlibainika
#TumeYaUchunguziReport
Ripoti Ya Tume

Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimesema madai ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa kuwa kauli za Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. John Heche zimekuwa na uchochezi na tishio kwa usalama wa Nchi hayana msingi wowote wa kisheria na badala yake yanaakisi tafsiri potofu isiyoendana na misingi ya demokrasia na vyama Vingi na inayopoka Mamlaka ya Mahakama ya kuwa ndiyo muamuzi wa kesi za aina kama inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Taifa Bw. Tundu Lissu na si Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa.
Chadema imetoa kauli hiyo katika barua yake kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa ya leo Jumatano Mei 20, 2026, barua ikisainiwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Bw. John Mnyika, ikiwa ni majibu kwa Ofisi hiyo iliyoitaka Chadema kueleza kwanini kisisitishiwe usajili wake kutokana na kukiuka sheria ya Vyama vya siasa na kuhatarisha amani na usalama wa Nchi.
Kulingana na barua ya Msajili, Ofisi ya Msajili ilieleza kuwa Matamshi ya Heche kuhusu uwezekano wa maandamano ya wananchi kushinikiza kuachiwa kwa Lissu kunahatarisha amani na usalama wa Nchi, kulingana na sheria ya Vyama vya siasa, Kifungu cha 19.
"Kauli ya kisiasa inayozungumzia maandamano ya amani si sawa na uchochezi wa vurugu. Katika mazingira ya kidemokrasia, maandamano ya amani ni nyenzo halali ya kisiasa inayotambulika kitaifa na Kimataifa. Barua yenu haijataka mahali popote ambapo Mhe. Heche alihamasisha wananchi kufanya vurugu, kutumia nguvu, kufanya uharibifu au kuivamia Mahakama." Imesema Barua ya Chadema kwa Msajili.
"Aidha kama ni kweli kuwa Mhe. Heche ametenda kosa la kuingilia Mahakama basi Mahakama ina mamlaka kamili kuweza kuamuru kushikwa kwake na kushtakiwa kwa kosa la kudharau Mahakama (contempty of Court). Aidha DPP kama anaona ametenda kosa hilo angeweza kufungua mashtaka dhidi yake." Barua hiyo imesema.
Kulingana na Chadema, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa haina mamlaka ya kisheria ya kufungua na kuendesha mashtaka juu ya makosa yanayodaiwa kufanywa na Heche, hivyo kujitwika madaraka hayo ni kutenda kazi Ofisi hiyo ikiwa imevuka madaraka yake.
Chadema kando ya kusisitiza kuwa kesi ya Lissu ni ya kisiasa, kimesema kudai haki, kuhoji mwenendo wa mashauri yenye maslahi ya umma au kutoa maoni kuhusu mwenendo wa dola si kosa la jinai wala ukiukwaji wa sheria ya Vyama vya siasa, wakisema uhuru wa Mahakama haulindwi kwa kuwanyamazisha wananchi au vyama vya siasa bali hulindwa kwa mahakama kutenda haki kwa mujibu wa sheria bila kuingiliwa, Mnyika akisema hakuna sheria inayokataza wananchi au Chama cha siasa kueleza maoni yake kuhusu kesi yenye maslahi ya umma, mradi Mahakama isidharauliwe kisheria.

Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi
MR BEBERU JR retweetledi

Kwa hapa tulipofika kuna mambo madogodogo hayawezi kunisumbua au kunitoa kwenye focus! Na sote tusimame imara! Lissu ana hii LASER FOCUS that is why we need him out!
Ushindi umekaribia na huu ndo muda wa kuweka focus!
It’s simple
#FreeTunduLissu
#SamiaMustGo
#CCMmustgo
#KatibaMpya
In this order!

Filipino
MR BEBERU JR retweetledi
MR BEBERU JR retweetledi

Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi amesema Viongozi wa Vyama Siasa ni wadau muhimu wa amani.
Jaji Mutungi amesema hayo wakati wa kikao cha Viongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa lilifofanyika Mkoani Morogoro
#KitengeUpdates
Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi

🚨 WAKATI wowote usishangae wala kushtuka kumwona kiungo Aziz KI akirejea nchini na kujiunga na Yanga, kwani pande hizo mbili bado zinahitajiana na kuna ishu kati yao inaendelea chinichini.
Taarifa za ndani kutoka Yanga zinaeleza kuwa, Aziz KI, anafikiria kurejea Tanzania kufanya mazungumzo na Yanga ili ajiunge tena na timu hiyo ambayo ilimpa umaarufu mkubwa.

Indonesia
MR BEBERU JR retweetledi

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimesema kulingana na kifungu cha 46 cha sheria ya Vyama vya siasa Nchini, mwanachama au Kiongozi anayekiuka sheria hiyo anatakiwa kujieleza mwenyewe, ikiwa itahitajika kufanya hivyo kwa Msajili wa Vyama vya siasana baadae Chama chake kushirikishwa kabla ya muhusika kupewa adhabu ya kutoshiriki katika siasa kwa kipindi kisichozidi miezi sita.
Chadema kupitia kwa Katibu Mkuu wake Bw. John Mnyika, kimetoa ufafanuzi huo leo Jumatano Mei 20, 2026 katika barua yake kwa Msajili wa Vyama vya siasa, akiinyooshea kidole Ofisi hiyo kwa kutaka kusimamisha usajili wa Chadema ama kutozwa faini kwa makosa yanayodaiwa kufanywa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema bara John Heche na Mwenyekiti wa Chadema Korogwe Ndugu Oliver Kisaka.
"Hata kama ndugu Kisaka na Makamu Mwenyekiti Heche wangekuwa wamekosea, kifungu cha 46 cha sheria ya Vyama vya siasa inatoa muongozo wa nini kifanywe dhidi ya mwanachama au Kiongozi aliyekiuka sheria hiyo. Yeye ndiye angetakiwa ajieleze na kama hajatimiza chama chake ushirikishwa kabla ya kupewa adhabu ya kutoshiriki katika siasa kwa kipindi kisichozidi miezi sita. Sasa inakuwaje kosa hilo lisukumiwe chama wakati kuna njia ya kushughulikia kosa lililotendwa na mwanachama au Kiongozi?" Amehoji Mnyika katika barua ya Chama hicho kwa Msajili.
Maelezo ya Chadema yamekuja kufuatia Ofisi ya Msajili kuyatafsiri maneno ya Kisaka kuwa ni uchochezi au kuhamasisha matumizi ya nguvu, Chadema ikisema kauli ya Mwanachama wake huyo ilikuwa ni maoni ya kisiasa kuhusu msimamo wa wananchi katika mazingira ya kisiasa yaliyokuwepo na ni kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania.
"Hakuna sehemu yoyote katika kauli ya Kisaka iliyohamasisha matumizi ya silaha, vurugu, uvunjifu wa amani au matumizi ya nguvu dhidi ya dola. Kutumia maneno kama "mageuzi makubwa" si kosa la jinai wala si ushahidi wa uchochezi. Mageuzi ya kisiasa yanaweza kuwa Kikatiba, kidemokrasia na ya amani." Imenukuliwa barua ya Chadema.
Chadema imesisitiza kuwa tafsiri ya Msajili wa Vyama vya siasa kuhusisha moja kwa moja mageuzi na vurugu ni tafsiri yenye madhara kwa demokrasia, uhuru wa kisiasa na uhuru wa mawazo na inayokiuka kwa uwazi ibara ya 18(1) na ibara ya 29(1)-(2) za Katiba ya Tanzania.
Katika barua hiyo, Chama hicho pia kimebainisha kuwa Sheria ya Vyama vya siasa haiwezi kutumika kuzuia mijadala ya kisiasa, ukosoaji wa dola au maoni kuhusu mwelekeo wa Taifa, kikisema kufanya hivyo kutakuwa ni kugeuza sheria hiyo kuwa chombo cha kukandamiza ushindani wa kisiasa badala ya kusimamia mazingira huru na yenye haki kwa vyama vyote vya siasa.

Indonesia







