乔瑟夫
6.8K posts
























VIDEO: Akiwakilisha kundi la Wabunge walio wachache bungeni katika msiba wa Hayati Edwin Mtei, Mbunge wa Viti Maalum kupitia CHAUMMA, Sigrada Mligo, amesema busara na hekima za Mzee Mtei ni nguzo muhimu ambazo wanasiasa wanapaswa kujifunza. “Mimi binafsi huwa natamani nipate hata robo tu ya busara za huyu mzee, nikiziangalia hata theluthi za busara za mheshimiwa Mbowe niwe nazo, lakini nimeshindwa. Sisi kama wabunge tulio wachache bungeni, tunamuahidi kwenda kupigania demokrasia ya kweli katika nchi hii, kwenda kuhakikisha nchi hii inarudi kwenye kuheshimiana, tunajadili jambo la kitaifa kwa pamoja. Ameendelea kusema, "Wanyonge wanatakiwa kuungana kupambana na wenye nguvu, nashangaa sana pale tunapoona wanyonge wanafinyana wenyewe.”




VIDEO: Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ambaye pia ni mwanafamilia wa marehemu Mzee Edwin Mtei, amejibu hoja mbalimbali zilizoibuliwa mitandaoni zikidai kuwa CHADEMA haijapewa nafasi na hadhi inayostahili katika taratibu za kumuenzi muasisi wa chama hicho kabla ya mazishi yake. Akizungumza na waandishi wa habari, Mbowe amesema anasikitishwa na taarifa hizo akizitaja kuwa ni za uongo na zenye nia ya kuuchafua msiba huo, huku akisisitiza kuwa hakuna mtu wala kundi lililotengwa katika maandalizi ya mazishi ya marehemu Mzee Mtei. Mbowe amesema familia inapenda kuona mwili wa marehemu ukipumzishwa kwa amani bila malumbano yoyote, akibainisha kuwa CHADEMA imepewa nafasi kubwa katika taratibu zote kuanzia zoezi la kuuchukua mwili Mochwari hadi shughuli za kumuaga na kumuenzi marehemu. Ameongeza kuwa watu wengi waliopo msibani hapo ni wanachama na viongozi wa CHADEMA, jambo linalothibitisha kuwa chama hicho kimehusishwa kikamilifu katika kila hatua ya maandalizi ya msiba huo. “Ninasikitishwa na baadhi ya watu wanaotaka kuuchafua msiba huu kwa kutoa taarifa za uongo. Hakuna aliyebaguliwa wala kutengwa. Kila mtu amepewa nafasi ya kumuenzi Mzee Mtei,” amesema Mbowe. Mazishi ya Mzee Edwin Mtei yanatarajiwa kufanyika kesho, Jumamosi, katika makaburi ya nyumbani kwake Tengeru, jijini Arusha.



















