
Mshua_G27
1.6K posts





6X9HXB





Napoli 🇮🇹 2:1 Torino 🇮🇹 Wolves 🏴 1:2 Liverpool 🏴 Celta 🇪🇸 1:2 Real Madrid 🇪🇸



@Sativa255 Code imetoka na umeshachanika timu3







VIDEO: Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameibua madai kuwa wamebaini uwepo wa wachochezi na wanaharakati wanaolipwa ili kuvuruga amani ya nchi, akidai kwamba baadhi ya vijana wanaoishi nje ya Tanzania wamepokea dola milioni mbili (sawa na shilingi bilioni 4.5) kwa ajili ya kuchochea vurugu. Ametoa kauli hiyo akiwa katika ziara yake mkoani Arusha, leo Novemba 30, 2025 ambapo amesema uchochezi mwingi unatoka kwa watu waliopo nje ya nchi na kwamba malengo yao yamejikita kwenye rasilimali za taifa. Ameeleza kuwa juhudi za kujaribu kuwavuruga Watanzania zinatokana na rasilimali zinazogunduliwa nchini, ikiwemo uranium ambayo Tanzania sasa inakadiriwa kuwa na tani 890,000 za ujazo, na hivyo kuwa nchi ya tisa duniani na ya kwanza Afrika. “Wanalenga tupigane ili wachukue rasilimali. Tumeshuhudia hili likiharibu mataifa mengi ya Afrika,” amesema. Amani ikitoweka, hata karoti na nyanya za Ngarenanyuki haziwezi kuuzwa,” ameonya. Ametoa wito kwa Watanzania kukataa kurudishwa katika vurugu, akisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa kupambana na umaskini na kukuza ajira nchini.

























