Martin Maranja Masese@IAMartin_
JE, TUMESAHAU OKTOBA 29 HARAKA HIVI?
Leo ni Machi 29, 2026. Ni jumla ya siku 152. Wastani wa miezi mitano tangu mauaji ya kinyama ya raia kufanywa na Serikali kwa raia waliokuwa wanaandamana.
Hakuna ambaye anahusika na kutoa na kutekeleza amri amewajibika/amewajibishwa. Ni wazi hawajutii kwa kilichotokea. Leo najadili na wananchi wenzangu.
Ndugu zetu walipoteza maisha wakipigania haki. Wasanii wengi waliamua kusimama upande wa watawala na kuwapa sifa/utukufu wakati damu ilipomwagika.
Leo tunashangilia nyimbo zao siku nzima. Je, hii ndiyo ile “cancel culture” tuliyokesha na kujadili usiku kucha? Je, zile zilikuwa hasira za muda tu, na sasa zimepoa?
Tuliahidi kutozika kumbukumbu zao, lakini tumeshazika utu wetu kwenye “playlists” za wasanii waliochagua vipande vya shilingi kuliko uhai wa mashabiki wao.
Hao wasanii huwezi kuwatenga na uovu. Wakati wa maandamano, risasi zikirindima, hofu ikitawala. Wao walichagua kuimba sifa na kuachana na ukweli.
Ukishabikia na kueneza kazi za wasanii wanaotumika na Serikali ya CCM, utakuwa umesaliti kumbukumbu ya wale waliofia ardhi, haki, na mustakabali wetu.
Kususa kazi za wasanii lilikuwa hitaji la kimaadili, wito wa uwajibikaji (accountability). Tulihitaji kuwaona wasanii wakitambua wajibu wao kwa jamii/mashabiki.
Hii si kuhusu kuupenda au kutoupenda muziki. Ni kuwakumbusha usanii si burudani tu. Ni sauti ya jamii. Wakati wa shida, sauti hiyo itumike kwa niaba ya watu
Ni suala la hekima na uwajibikaji wa kijamii. Wasanii wana sauti yenye nguvu. Wanaweza kuwa sauti ya watu wakati wa shida, au kuwa zana ya propaganda.
Wakati damu ilipomwagika na hofu ilipotawala, kuchagua kuimba sifa tu (bila kutambua maumivu ya watu) kulionekana kama kuwatelekeza mashabiki.
Kabla ya kubishana nani msanii mkali, tukumbuke Oktoba 29, 2025. Damu ya ndugu zetu zisipuuzwe. Maisha yaliyopotea hayafai kufutwa na melody nzuri.
Tusiwape promo waliotupa kisogo wakati wa mateso. Tusipagawe na midundo na kuwaneemesha wale ambao hawaoni tatizo lao na bado hawajajirekebisha.
Hakuna muziki mzuri unaoweza kuzima kilio cha wanawake wajane na watoto yatima. Hakuna muziki unaoweza kufuta damu ya ndugu zetu iliyomwagika.
Wakati kodi zetu zilinunua risasi zilizowatoa roho ndugu zetu, wasanii hawa walitunga beti za sifa kwa watawala. Huwezi kutenganisha sanaa yao na uovu.
Kila mara unapocheza, ku-share, au kusifia kazi ya msanii aliyewapa kisogo wakati wa dhiki, unawazomea wajane na mayatima walioachiwa viti wazi mezani.
Unacheza dansi juu ya makaburi ya wale ambao hawakupata hata fursa ya kuzikwa. Wengine maiti zao hazikupatikana. Ndugu wamezika picha na nguo.
Msanii wa kweli ni kioo cha jamii, si pazia la kuficha ukatili. Msanii anayesimama na adui wa shabiki wakati wa mateso, amepoteza sifa ya kuwa sauti ya watu.
Usikubali ‘melodi’ nzuri iwe kilema cha kumbukumbu yako. Haki haijapatikana, na damu bado mbichi. Tusiwashangilie waliotusaliti kwa vipande vya fedha.
Let us never forget October 29, 2025. 💔