Charles Masud
635 posts


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, Bw. Nathan Belete ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Miradi wa Benki hiyo, Kanda ya Afrika, pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe Bw. Firas Raad mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2026.



Indonesia

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya uchunguzi wa Kijinai wa Matukio ya Ghasia ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambapo amemteua Shabani Ally Lila, Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Kamishna na Mwenyekiti wa Tume hiyo.
Rais ameunda Tume hiyo ikiwa ni utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025 na kwa kuzingatia mamlaka aliyonayo chini ya Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32.
Rais Samia amewateua pia Makamishna wa Tume hiyo ambao ni Gad John Mjemmas, Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Awadh Mohamed Bawazir, Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Aishieli Nelson Sumari, Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
#MillardAyoUPDATES

Indonesia

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, amewataka viongozi wa Serikali hususa ni Vijana pindi wanapopata madaraka kufanya kazi kwa weledi na kuacha kiburi ili kuendeleza maono ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Kihongosi amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni mfano wa kiongozi anayewatumikia Wananchi kwa kuyaishi maono hayo ya mwanzilishi wa Taifa la Tanzania.
Ameyasema hayo leo baada ya kutembelea na kuweka maua katika kaburi la Hayati Mwalimu Nyerere lililopo Butiama, Mkoani Mara, kama ishara ya heshima na kumbukumbu kwa Baba wa Taifa.
“Mwalimu Nyerere alipinga ukabila, udini na ukanda, Dunia inamheshimu kwa misingi yake ya uongozi, amani, umoja na utu na kila tunapofika hapa tunapata moyo wa kuendeleza dira yake ya kujenga Taifa linalosimamia maslahi ya Mwananchi wa kawaida,” alisema Kihongosi.
Aidha, amesema ziara hiyo ni sehemu ya kuenzi maadili ya Mwalimu Nyerere na kusisitiza kuwa CCM itaendelea kusimamia misingi ya uongozi bora, haki na usawa iliyoasisiwa na Baba wa Taifa.
#MillardAyoUPDATES
Indonesia

KIHONGOSI: MAAMUZI YA VIKAO YAHESHIMIWE
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Kenani Kihongosi amesema msingi wa uhai na uimara wa chama ni kuheshimu vikao na maamuzi yake.
Akizungumza Tarime, Kihongosi amesisitiza kuwa viongozi na wanachama walioiva kiitikadi hutambua kuwa maamuzi ya mwisho ya vikao ndiyo maamuzi rasmi ya chama, kwani huko ndiko mipango hujadiliwa, hukubaliwa na kupewa mwelekeo wa pamoja.
Ameeleza kuwa CCM itaendelea kujengwa na wanachama watiifu, wazalendo na wanaoweka maslahi ya chama mbele kuliko makundi au maslahi binafsi.
“Chama kwanza, watu baadaye. Tukipenda chama chetu, tukalinda umoja, mshikamano na nidhamu ya vikao, tutajenga CCM imara na yenye kuendelea kuaminiwa na wananchi,” amesema Kihongosi.
Aidha, amewataka viongozi kuachana na migawanyiko na kuhakikisha Tarime inabaki kuwa mfano wa umoja, upendo na mshikamano ndani ya Chama Cha Mapinduzi.




Indonesia

TARIME - MARA MKUTANO WA HADHARA WA MWENEZI WA CCM TAIFA NDG KENANI LABAN KIHONGOSI
#KaziNaUtuTunasongaMbele




Indonesia

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi, Kenani Kihongosi amesema Chama hicho hakijawahi kukosea na kwamba maamuzi yote yanayofanywa ndani ya Chama yanapaswa kuheshimiwa na Wanachama pamoja na Viongozi wake.
kihongosi amesema hayo leo Mei 14, 2026 Mkoani Mara katika Wilaya ya Musoma wakati akizungumza na Wanachama na Viongozi wa chama hicho, ambapo ameongeza kuwa heshima waliyonayo Viongozi ndani ya Chama hicho imetokana na CCM, hivyo hakuna anayepaswa kujiona kuwa mkubwa kuliko Chama kwani kufanya hivyo ni kujidanganya.
“Kwanza ni Chama, Watu baadaye, haya maneno nayaongea mimi kama Mwenezi wa Chama, tofauti na hapo wewe unataka kukiharibia Chama,” amesema Kihongosi.
Aidha, amewaomba Viongozi wa CCM kuendelea kusimamia umoja na nidhamu ndani ya Chama huku akisisitiza kuwa Chama kina uwezo wa kumshughulikia Mtu yeyote atakayekiuka misingi yake bila kuangalia cheo, umri wala umaarufu wake. #MillardAyoUPDATES
Indonesia

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mahmoud Thabit Kombo (@mahmoudkombo ), amewasilisha ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa Rais wa Jamhuri ya Djibouti, Ismail Omar Guelleh.
Ujumbe huo umewasilishwa Mei 9, 2026 Jijini Djibouti wakati wa sherehe za kuapishwa kwa Rais Guelleh, ambapo Waziri Kombo amemwakilisha Rais Samia katika hafla hiyo rasmi ya Kitaifa. #MillardAyoUPDATES

Indonesia

Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili Tanganyika TLS chini ya Mwenyekiti wake Wakili Boniface Mwabukusi amesema moja ya changamoto kubwa ya Tume ya kuchunguza matukio ya ghasia za Oktoba 29, 2025 ni pamoja na kutoa maelezo yasiyokuwa na uthibitisho wa kutosha kuhusu masuala nyeti kama utekaji, upotevu wa watu na mauaji na badala yake wametegemea zaidi taarifa za vyombo vya dola bila ya kufanya uchunguzi huru.
"Moja ya jambo hili ni kusema watu wamekufa, wapo mochwari halafu wakapotea. Tume inaishia hapohapo bila kufafanua au kwenda zaidi ba kutuambia nini kilijiri, nini kifanyike, walitokaje mochwari, nani alikuwepo mochwari.? Hili ni eneo ambalo lilitakiwa lipewe majawabu kwasababu kuna watanzania ambao kufuatia ndugu zao kuuwawa, kuonekana mochwari na baadaye kupotea mpaka leo hawajapata haki ya kuwasitiri ndugu zao kwa heshima.
Kuna suala la watu kutekwa na kupotea pia, huwezi kusema watu wanatekwa kimapenzi, mtu kama Humphrey Polepole huwezi ukaniambia ni mtu ambaye ameanza mapenzi ukubwani kiasi ya kwamba anaweza akadanganywa, akafichwa chumbani mpaka leo asimuone mama yake anamtafuta, haya Mdude Nyagali, ugomvi wa mapenzi yapi? Kwenye mazingira kama haya tunahitaji majibu ya kina na yenye tafiti." Amesema Mwabukusi leo Mei 11, 2026 kwenye Mkutano na wanahabari Makao Makuu ya TLS Dar Es Salaam.
Katika hatua nyingine, Mwabukusi amezungumzia haki za binadamu, akisema Tume ya Rais imedogosha madai ya utesaji ilihali TLS imebaini kuwa watuhumiwa wengi wa Oktoba 29, 2025 waliteswa, kunyimwa haki zao na kushikiliwa kinyume cha sheria, ikiwemo baadhi ya watu walioteswa, kuvunjwa mikono na kupandishwa mahakamani wakiwa hawajajisitiri maungo yao, suala ambalo Tume hiyo haijazungumza lolote kuhusu matukio hayo.
Indonesia

#TANZANIA: TLS YATAKA SERIKALI IKIRI KOSA NA WALIOHUSIKA WACHUKULIWE HATUA ILI KUELEKEA KWENYE MARIDHIANO YA KWELI
Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (@TanganyikaLaw), Wakili Boniface Mwabukusi leo Mei 11, 2026 amesema ili kuelekea kwenye maridhiano ya kweli serikali inapaswa kukiri makosa ya yaliyotokea kabla, wakati na baada ya uchaguzi wa 2025.
Aidha, @Mwabuk2Boniface amesema kwenye swala hili hakuna kufunika kombe mwanaharamu apite, kuwe na uwajibikaji kwa waliofanya makosa na ifahamike waliotekwa wako wapi pamoja na miili ya waliofariki kwenye maandamano wakati na baada ya uchaguzi ipatikane ili ndugu zao wakazike kisha waelekee kwenye maridhiano.
Zaidi: youtu.be/H2Iy07gde-Y

YouTube
Indonesia

Kuna crisis kubwa sana ya Barabara Nchi hii…
Kuna ujambazi unafanyika kwenye aina ya ujenzi wanaofanya wachina! Barabara inajengwa nusu mwaka imeisha kabisa imekua kama mashimo ya ng’ombe..
Watu wanahongwa kuhujumu uchumi wa Nchi na kuhujumu wananchi.
Barabara ya Tarime - makutano imejengwa miaka ya 90’s bado ina uafadhali kuliko barabara ya Singida to Babati au Dodoma - Iringa za juzi tu..
Ukitoka Mwanza mpaka Bunda unaweza kulia, alafu eti kuna Waziri, makatibu wakuu, wakurugenzi, wakuu wa mikoa , Tanroads sijui na nani!!!
Utawala dhalimu umefitinika.

Indonesia

Mhe. @HecheJohn, amewasili Mkoa wa Mara katika Jimbo la Bunda, ambapo amepokelewa na Katibu wa Kanda hiyo, Jackson Mnyawami, pamoja na viongozi wa chama Wilaya ya Bunda.
Mhe. Heche leo anatarajiwa kuongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa Ofisi ya Chama Jimbo la Bunda Mjini.



Indonesia










